Friday, September 4, 2015

BARUA YA WAZI KWA WATANZANIA NA VIONGOZI WA VYAMA SIASA.

  Na Yusef israel
Namshukuru mwenyezi Mungu kwa kutuweza kutufikisha hapa  toka tupate uhuru na toka nchi zetu mbili hizi zilizoweza kuungana na kuzaliwa taifa moja la jamhuri ya muungano  watu wa Tanzania,ni mambo mengi tumeshuudia mazuri  na mabaya natunapakaa na kuangalia nyuma  tunaona kweli kuna mazuri tumefanikiwa na kuna mambo ambayo tumeshindwa kuyatimiza au kuyatenda kwa sababu zetu wenyewe au makosa yetu wenyewe au sababu ya kutokuwa na uwezo wa kifedha.
Tanzania ya leo in wananchi waliozaliwa wakati nchi ikiwa inaitwa Tanganyika  na ikiwa haijapata uhuru na watanzania wa baada ya uhuru  na Wa Tanzania wa walio zaliwa nchi ikiwa inaitwa jamuhuri ya muungano wa Tanzania ,je wakati  nchi hizi zilizokuwa zinaungana Wazee wetu walifikiria nini au nini kilichowafanya wazee wetu hawa waamue nchi izi mbili ziungane  utakuta kuna mambo mengi yanayosemwa ,wengine ni kwa ajiri ya ulinzi wa visiwa hivyo visije vikachukuliwa tena na sultan wa oman wengine hiyo ni siri ya  Mwalimu na Mzee Karume kuna mambo mengi sana na baadhi ya viongozi wa siasa waliosomeshwa na serikali zilizokuwa zikiongozwa na wazee leo wamewaita majina mengi tu ya ajabu na kuwadharau.
 Tukiangalia kwa kirefu historia ya watu weusi wa Afrika mashariki utakuta tuna historia ndefu sana na baadhi ya historia kwa vizazi vya leo hawajui,kutokana na historia yetu ya kutawaliwa na kufanywa watumwa kwa zaidi ya miaka na miaka na waarabu walikuja na kuleta dini kutoka uarabuni mpaka congo waliweza kutufanya kuwa watumwa na kuwatumikia na kutuuza mpaka india ya kusini ndio maana ukienda india ya kusini utapata waafrika ambao wanaitwa sidi hawa asili yao ni msumbiji,Tanzania bara na visiwani  na Mombasa mpaka Somalia, ni hivyo  hivyo  katika dini ya wakristu Wazungu hawa walio tuletea dini ya ukristu utakuta katika sehemu zingine za Africa mchezo  ulikuwa ni huo huo kuanzia west Africa mpaka Africa ya kusini ndio maana leo wafrica wameajaa latin America na visiwa vya caribean ulaya ya magharibi na marekani.
Kwa kifupi kufatana na historia hiyo na baada ya kuwapokea hawa watu na dini walizo tuletea na kuzipokea na kupewa majina yasiyo yetu ya kiarabu na kizungu tumekuwa tukiishi kwa Amani na wakati mwingine tumeweza kugombana au kutokea michafuko ya kidini katika nchi zingine za ki Africa   au vita za ukabila .kwa kuangalia mbali wazee wetu waliamua kuangalia mbali sana kutokana historia ya yetu sisi waafrica  ndio maana wakaweka uzalendo na kujithamini kwanza kwamba sisi ni waafrika kwanza na sisi ni watu weusi kwanza ni lazima tuelewe hilo kwanza tuweke uzalendo na uafrica wetu mbele kwa kizungu( Value)kwanza na ndio walipo angalia na kusema tuungane tufanye taifa moja  na ndipo kuzaliwa Taifa laTanzania  nia yao hawa wazee ilikuwa ni nzuri sana na muungano ulifanyika katika kipindi kigumukwani dunia ilikuwa iko na sehemu mbili ya Urusi na upande wa Amerika.
Wakati wasomi hawakuwa wengi  lakini walisimama imara na kujenga taifa lenye lugha moja Kiswahili,taifa lisilo na udini bali taifa la watanzania taifa lisilo na ukabila taifa ambalo linaendeshwa na katiba yenye misingi binadamu wote ni sawa na serikali aina dini  bali dini ni yako wewe mwenyewe unaweza kuwa muislam au mkrisitu,au kuwa mtu ambaye auna dini.
Na ndiyo misingi mikubwa katika demokrasia  serikali aina dini na hiyo imetokana na jibu ambalo Yesu aliwajibu cha mfalme ni cha mfalme nacha Mungu ni cha Mungu na ndio ukawa ni mwanzo wa wa kuwa na serikali ambayo aina dini pamoja na kuwa na wafalme au tawala ambazo hazikuweza kuanza  kutenganisha utawala wa dini na serikali lakini  baadaye walikubali na kuanza kutenganisha dini serikali pamoja na hayo bado kuna nchi zinatawaliwa na udini uwezi kuwa au kupata cheo lazima wa dini hiyo kwa mfano uarabuni ,katika karne hii ya leo hili jambo ndio mojawapo ya nguzo za demokrasia,
Ndugu zangu tumefika aje hapa tulipo  imekuwa ni safari ndefu yenye milima na mabonde imekuwa ni safari  ya kupanda na kushuka na baadaye na baadaye kuja kuonekana ni safari ya matumaini au safari  itakayo kuwa na manufaa mwaka 1967 Azimio la Arusha lilikuwa ni azimio la kuifanya Tanzania iwe nchi ya kujitegemea sababu mwalimu alikuwa akiangalia mbali nchi aiwezi kuwa nchi ikiwa inategema vitu kutoka nje au misaada au nchi iwe inaongozwa lakini aina uchumi wa kujitegemea nasiyo kutegemea misaada na  kuweka miiko ya uongozi na ndio maana lilikuwa na mambo mengi mazuri na mambo mengine ambayo kama alikosea au walikosea leo kuna wasomi wengi ambao wange weza kuyarekebisha sababu hakuna mtu mtakatifu hapa duniani na hakuna kiongozi asiye kuwa na makosa au aliye weza kutekeleza yote anayokusudia au aliyo aahidi lakini utakuta kwamba kila kiongozi amechangia kitu Fulani katika maendeleo au kurekebisha  kilicho kuwepo na kukifanya kuwa boro zaidi na siyo kukivunja .
Mwaka 1979 mwalimu alisimamaimara katika  vita ya kumtowa Iddi Amini alipovamia Tanzania  na baada ya hapo ali ikawa si nzuri kutokana na serikali kuweza kutumia pesa nyingi  nawaliokuwepo wakati huo  watakumbuka tulikula unga wa njano  sukari ya mstari sabuni ya mstari lakini pamoja na hayo yote Mwalimu alisimama imara katika kuongoza nchi na chama mpaka mwaka 1985 alipoachia madaraka lakini alipondoka aliacha nchi ikiwa na viwanda vingi  shirika la ndege, shirika la reli ,shule hospitali nchi ambayo aina udini wala ukabila nchi ambayo haina  sisi ni wakusini sisi ni wa kaskazini au sisi ni wabara  lakini leo haya mambo yameoneka na udini umeingia katika siasa kama mlivyomsikia katibu mstaafu wa chadema alivosema juzi,
Je tunapokwenda tunapajuwa  ?ningependa sana katika wakati huu wa uchaguzi  naomba niwakumbushe mkumbuke ya kwamba kujenga ni ghali lakini kubomowa ni rahisi naomba sana viongozi wa siasa wa ukawa na wa vyama siasa na ccm  mkae makini sana msitumihe lugha zitakazo leta umwagaji wa damu nakumbuka kwenye bunge la Katiba Mheshimiwa lipumba aliwaita wana CCM itarahamwe ningependa sana wana ukawa mkumbuke hilo neno baadhi yetu tulifiwa na ndugu zetu na rafiki zetu kule Rwanda waliouliwa na hawa intarahamwe leo hii mnasema Mzee Mkapa kawaita watu wa ukawa eti wapumbavu  nawaomba sana muepuke lugha za kipumbavu kabisa asala ya ni kubwa mambo yanapoharibika wenye kupata shida huwa ni kina mama wazee na watoto hawa viongozi uwa wa kwanza kupanda ndege nakukimbia  naomba mufanye siasa zenye ustaarabu na zenye ukweli na sio kupotesha umma sababu baadhi ya wana siasa wamekuwa wana ukabila na wanaudini na waongo na wenye uchu ya madaraka.
Ndugu watanzania  najuwa mnataka mabadiriko na mimi pia nataka mabadiriko lakini mabadiriko nayoyataka ni mabadiriko  ya kiongozi amabaye ana makundi kundi lake ni Tanzania  kiongozi ambaye ni mchapa kazi, kiongozi mwenye msimamo,kiongozi ambaye ana ukabira ,kiongozi ataye chaguwa mawaziri wachapa kazi,mawaziri wenye uwezo wa kuongoza wizara zao kikamilifu ,kiongozi ambaye anauwezo wa kukemea kwa sauti ya ali ya juu kiongozi mwenye kuamua maamuzi magumu,kiongozi ambaye atazifanya taasisi za serikali ziweze kufanya kazi kwa ufanisi wa ali juu na bila kuingiliwa na kiongozi yoyote maana yake akuna aliye juu ya sheria,kiongozi atayelinda na kuakikisha mali asili inalindwa na inawanufaisha watanzania wote na kuirudia upya mikataba yote kwa manufa ya watanzania sababu hapa Europe kila mwaka wakati wa summer waarabu wankuja kupumzika kutoka hizo falme zote za kiarabu zenye mali asili ye mafuta na gesi na unaona vile hawa jamaa wanavyonufaika na mali asili unaona vile wanavyo sukuma watoto wa kuja kusoma  hapa ,kiongozi  ataye tegeneneza mifumo mizuri ya uwekezaji yaani miundo mbinu ,bara bara,umeme,maji,plan za miji na sehemu za kuweka viwanda  kiongozi atayejenga highways kutoka Dar mpaka boda ya Uganda ,Zambia,Burundi,Msumbiji,,Congo,
Kwa muda wote nimekaa nikitafari je baada ya pata shika ya bunge la katiba kuweza kuandika katiba yenye mawazo ya watu wote wa vyama vya siasa  je baada ya hao jamaa kutoka ndani ya bunge tunaweza kupata katiba yenye manufaa kwa taifa je raisi wa awamu ya tano hataweza kuwa mjasiri  na kusimama na kuangalia mbali au kuwa na vision kusema katiba hii iliyopendekezwa inatakiwa iangaliwe upya au irekebeshwe  ndipo hapo nilipoangalia kwa mbali na kuona kinachotusumbua au kutuvuluga ni maendeleo na njaa ya uchumi  na ndipo nikatapaza wazo hili hili muungano huu uwe imara kwa kizazi na kizazi je tunaweza kuwa na katiba ya namna hii
Kiongozi mkweli mpinga rushwa kiongozi atayeweza kukaa na kuangalia nchii inapashwa kuwa na katiba yenye maadili ya ukweli katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania  yenye serikari  moja na Raisi mmoja na makamu wa Raisi pamoja na mawaziri 8 na   mawaziri wakuu wawili waziri mkuu wa Zanzibar mwenye kuongoza wizara 14  na waziri mkuu wa serikali ya Tanzania bara mwenye kuongoza  mawaziri 14  yaani serikali yote ya jamhuri itakuwa na mawaziri 36 ukiweka Raisi na makamu wake ni serikali yenye watu38 tuu.
Mawaziri hawa wakuu watakuwa na asilimia 50 ya nguvu ya kuamua mambo ya ndani au ya sehemu wanazoongoza  katika maswala ya kiuchumi na kuakikisha sehemu wanazo toka zinapata maendeleo na wanauwezo wa kwenda nje na kuomba misaada  na siyo mikopo nawala si mambo ya ulinzi au mambo yanayousiana na uhusiano wa kimataifa watakuwa kutakuwa na bunge bara na bunge la Zanzibar halafu bunge la jamuhuri la muungano ambalo litakalo kuwa linakutana marambili kwa mwaka.
Kwa vile leo tuko na wasomi wengi waliosoma najuwa palipo na nia pana njia kamatukipata raisi mchapa kazi mwenye uchungu na nchi yake na siyo uchu wa madaraka raisi ambaye anajua mwafrika anasamani kama watu wengine mwafrika astaili kuitwa tumbili sababu ya rangi yake mwafrika apashwi kuuza mali yake bali wanaoitaka waje wajenge viwanda mwafrika anaitaji hospitali,maji,barabara,shule,nyumba bora,mwafrika anaitaji ulinzi na amani ,mwafrika anaitaji uongozi wenye maadili uongozi ambao hauna ukabila,udini wenye msimamo ,
Tutaweza kupata katiba ya haki naya ukweli namini watawezakukaa na kutengeneza katiba yenye kuleta maendeleo visiwani na bara itakayonufaisha watu wa jamuhuri  ya muungano wa Tanzania.
Ninamengi ya kusema lakini leo nataka niishihe hapa sababu unapotembea  nje ya nchi yako ndio unajuwa faida ya nyumbani au taifa unalotoka sisi wengine tumeitwa tumbili au nyani na hakuna kitu kinauma mtu kukuita sababu ya rangi yako au kukubagua sababu ya rangi yako  na wakati vitu walivyonao hawa wenzetu at kwetu vinawezekana kama tuna uongozi thabiti na imara,
Watanzania chagueheni kiongozi makini  chagueni kiongozi mwenye sifa za uchapa kazi  chagueni kiongozi atayeleta maendeleo mapya na kuweka kasi katika uwajibikaji chagueni kiongozi asiye na udini wala ukabila  na hao viongozi wa dini watoke kwenye siasa si ya kwao kabisa wakae pembeni kabisa,
Naomba vijana msindanganywe na baadhi ya wanasiasa kuwatumia mkumbuke Libya,Syria,Rwanda DRC ,Uganda kabla ya Museveni ,Burundi,Tunisia,Iraq maendeleo yanakuja kwa amani na si vurugu ninayasema haya sababu nimeshudia vita mbili uso kwa uso macho kwa macho 1984 up 1986 Uganda na 1992 1994Rwanda
Mwisho naomba Azam TV au Tbc au Itv watayarishe mdaharo wa watu wanowania uraisi na umakamu iliwaweze kujieleza mbele ya umma, nini watawafanyia waTanzania sababu tumeonaawamu zote nne kumekuwa na maendeleo lakini je wao watapo ingia madarakani nini watawafanyia waTanzania au umasikini wataufukuzavipi?sababu umasikini ndio adui mkubwa
Na mwisho tume ya uchaguzi tunaomba uchaguzi uwe wa wazi na amani na atayeshindwa akubali kwa uwazi,na kwa heshima,





No comments: