Monday, August 3, 2015

FILAMU YA AISHA YAZINDULIWA KWA KISHINDO WILAYANI PANGANI

1- moja
Filamu iliyopewa jina la AISHA imezunduliwa rasmi siku ijumaa ya tarehe 31/7/2015 wilayani Pangani chini ya shirika lisilo la kiserikali la UZIKWASA.
Aisha ni filamu ya tatu katika mfululizo wa filamu za UZIKWASA zikiangazia aina mbali mbali za unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto wa kike. Filamu hizi ni ni sehemu mojawapo tu ya njia za mawasiliano katika kampeni shirikishi-jamii ya mabadiliko ya tabia inayofahamika kama 'BANJA BASI'!, Pangani, Tanga.
Kabla ya filamu ya Aisha iliyozinduliwa kwa kishindo hivi karibuni, shirika la UZIKWASA tayari limeshatengeneza filamu nyenigne mbili ambazo ni FIMBO YA BABA na CHUKUA PIPI, wengi wa waigizaji waliomo ni wasanii wa vijijini.
Pia filamu hizi zinatokana na maisha halisi na utafiti wa kina katika jamii. Kwa nji hii UZIKWASA inahakikisha filamu zake zinaeleweka na zinafanya kazi kama kioo wka jamii. Lengo ni tuone, tuguswe na hatimaye tuchukue hatua ili kuleta mabadiliko.
Filamu ya AISHA inamhusu mwanamke anayeishi mjini na kuamua kurudi kijijini kwao kuhudhuria harusi ya mdogo wake. Wakati anajikumbusha maisha yake ya zamani, na kukutana na familia yake pamoja na marafiki, kunatokea mkasa wenye athari kubwa katika maisha yake.
Watu wangefumbia macho mkasa huo, lakini Aisha anaamua kupambana nao vikali ili kupata haki yake.
Filamu hii inahusu unyanyaa, aibu na wahanga kulaumiwa, na namna gani inazuia wanawake na wasichana kusema wazi. Pia inahusu baadhi ya mamlaka na viongozi kusita kufatilia ukiukaji wa haki za binadamu.
AISHA imeongozwa na mtaalamu maarufu Chande Omar, imetayarishwa kwa ushirikiano na Kijiweni Production, imefadhiliwa na A. Schindler na Swiss Development Cooperation (SDC) na kusimamiwa na shirika la UZIKWASA.
Filamu ya aisha ni kwa heshima ya wanawake wote waliopitia mikasa ya namna hii.
8- nane
Mkuu wa wilaya ya Pangani Bi Regina Chonjo ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi, nae alipata nafasi ya kutoa hotuba yake.
6- sita
Producer wa filamu ya Aisha Bwana Emil Shivji akizungumza na wananchi waliohudhuria viwanja vya Bomani.
7- saba
Mkurugenzi wa shirika la UZIKWASA Dokta Vera Piroth akitoa hotuba yake ya kipeke ambayo ilikuwa katika mtindo wa hadithi pamoja na maswali, Ilipendeza sana.
2- mbili
Shamra shamra za ngongoti zikikaribisha wageni waalikwa kwenye uwanja wa Bomani wilayani Pangani palipofanyika uzinduzi wa flamu ya Aisha.
3- tatu
Msanii maafuru wa mashairi Ndugu Mabwingo akitoa burudani jukwaani.
4- nne
Wananchi wakiendelea kufatilia uzinduzi wa filamu ya Aisha.
5- tano
Msanii mahiri katika uimbaji, Vitalis Maembe alikuwepo kwenye uzinduzi wa filamu ya Aisha, alitoa burudani ya kipekee.
9- tisa
Wasanii waliocheza filamu ya Aisha wakiwa katika picha ya pamoja wakati wakipokea zawadi zao za ushiriki.
11- kumi na moja
Washereheshaji katika uzinduzi wa filamu ya Aisha, Mohammed Hammie maarufu kama Anko Mo (kati kati), Nickson Lutenda aliyevaa koti la bluu pamoja na Pili Mlindwa.
12- kumi na mbili
Mkurugenzi wa shirika la UZIKWASA akiteta jambo na mkuu wa wilaya ya Pangani Bi Regina Chonjo.
10- kumi
Msanii Godliver Gordian ambaye amecheza kama Aisha katika filamu hiyo, akifanya mahojino na kituo cha luninga cha TBC ambao walikuwepo katika uzinduzi huo.
13- kumi na tatu
Msanii Vitalis Maembe akiwa na Godliver Gordian (Aisha), wakati wa utambulisha wa wimbo uliotumika kama soundtrack katika filamu hiyo.
14- kumi na nne
Godliver Gordian ama Aisha akiwa na mshumaa mara baada ya wananchi kuitazama filamu ya AISHA- lengo la mshumaa huo ni kumulika unyanyapaa, pamoja na aibu wanayoipata wanawake na wasichana wanapotendewa matendo maovu.
15- kumi na tano
Wageni waalikuwa wakiongoza na mkuu wa wilaya Pangani Bi Regina Chonjo nao waliwasha mishumaa katika kumuunga mkono Aisha katika harakati za kufichua maovu.
16- kumi na sita
Wananchi wengine pia waliwasha mishumaa kuashiria kuunga mkono harakati hizo.

No comments: