Friday, August 7, 2015

BENKI YA NIC YATOA MADAWATI 25 SHULE YA MSINGI CHAMANZI

 Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Ancent Shayo akiwa na wafanyakazi wa shule ya msingi chamanzi wakizungumza na wafanyakazi wa NIC hawapo pichani katika ofisi ya mkuu wa shule ya msingi chamanzi jijini Dar es Salaam leo.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
 BENKI ya NIC imetoa msaada wa madawati 25 katika shule ya msingi Chamanzi yenye thamani ya Sh.Milioni tatu kutokana na shule hiyo kukabiliwa na changamoto ya madawati.

Akizungumza baada ya kukabidhi  madawati  hiyo, Mkuu wa Biashara za Kibenki,Rahim Kanjii amesema kuwa shule hiyo waliona ina umhimu wa kusaidiwa sehemu ya madawati katika kupunguza idadi ya wanafunzi wanaokaa chini ardhi wakiwa darasani.

Amesema shule hiyo inatakiwa kusaidiwa kwa kila hali kwani watoto wanaoandaliwa hao ni taifa la leo hivyo wanatakiwa kuandaliwa mazingira bora ya kupata elimu.

Kanji amesema kuwa ameguswa sana na benki itaendelea kadri ya uwezo wake kusaidia shule katika kuweza kuondokana na chagamoto ya madwawati  katika kujenga mazingira bora ya kusomea watoto kwani wanaandaliwa kuja kuwa wanataaluma mbalimbali.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo,Ancent Shayo amesema kuwa shule ina wanafunzi 3200 lakini vyumba vya madarasa 11 na kufanya kila darasa kukaa wanafunzi 150.

Amesema madawati hayo ni kwa ajili ya wanafunzi wa darasa la nne kutokana na upungufu wa madwati 175 ambapo NIC imepunguza imetoa madawati 25 hivyo kwa darasa hilo linahitaji madawati 150 ili waweze kukaa katika siku ya mtihani wa taifa.

Shayo amesesema hitaji katika shule licha ya madawati wanaupungufu wa vyumba vya madarasa  kutokana na idadi ya wanafunzi hao.
 Wanafunzai wa shule ya msingi Chamanzi wakiwa darasani wakiwa wamekaa chini kwa kutokuwa na madawati ya kutosha katika chumba cha darasa la tatu walipotembelewa na wafanyakazi wa Benki ya NIC leo jijini.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Chamanzi, Ancent Shayo akizwa na wafanyakazi wa Benki ya NIC walipowatembelea wanafunzi wa Shule ya Msingi Chamanzi jijini Dar es Salaam walipotembelea chumba cha darasa la kwanza katika shule hiyo. 
Wafanyakazi wa Benki ya NIC akifungua meza na viti walivyotoa msaada katika shule ya Msingi Chamanzi ikiwa meza 25 na viti 25.
 Wafanyakazi wa Benki ya NIC waliosimama wakiwa wanafunzi wa shule ya msingi Chamanzi waliokaa baada ya kutembelewa na wafanyakazi wa Benki hiyo jijini Dar es Salaam leo.
 Picha ya pamoja ya wanafunzi wa shule ya msingi Chamanzi na wafanyakazi wa Benki ya NIC baada ya kutoa msaada wa meza 25 na viti 25 vya plastiki katika shule hiyo jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Biashara za Kibenki, Rahim Kanjii akipeana mkono na Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Chamanzi, Ancent Shayo  mara baada ya kutoa msaada wa meza 25 na  viti 25.
Wanafunzi wa shule ya Msingi Chamanzi wakiwa wamekaa kwenye viti na meza walivyopewa msaada na Beni ya NIC jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

No comments: