Sunday, July 5, 2015

WAKAZI WA KIGOMA WANUFAIKA NA KAPU LA PAMOJA NA VODACOM RAMADHAN

Mkuu wa Taasisi ya Vodacom Foundation Tanzania Renatus Rwehikiza (mwenye Shati jeusi aliyeinama) na Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation Doris Mollel (aliyechuchuma) wakikabidhi msaada wa vyakula kwa Ashura Sanno mkazi wa kata ya Kasimbi Kigoma Ujiji ambaye alinufaika na msaada huo kupitia kampeni ya Pamoja na Vodacom kwa watu wenye kipato cha chini kwa ajili ya mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Mkuu wa Taasisi ya Vodacom Foundation Tanzania Renatus Rwehikiza (wa tatu kushoto) na Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation Doris Mollel (wa tatu kulia) wakikabidhi msaada wa vyakula kwa Mwanne Hamisi mmoja wa wananchi aliyenufaika na misaada huo kupitia kampeni ya Pamoja na Vodacom Ramadhan kwa watu wenye kipato cha chini wa kata ya Kasimbi Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma kwa ajili ya mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Meneja wa Vodacom Tanzania mkoa wa Kigoma,Nathan George (kulia) akikabidhi msaada wa vyakula vya aina mbalimbali kwa familia ya Tamasha Jumanne msaada huo uliotolewa na Taasisi ya Vodacom Foundation kupitia kampeni yake ya Pamoja na Vodacom kwa watu wenye kipato cha chini wa kata ya Kasimbi Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma kwa ajili ya mwezi mtukufu wa Ramadhan.

No comments: