Friday, July 3, 2015

NEC NA VIONGOZI WA VYAMA VYASIASA ,WAJADILI MAADILI YA UCHAGUZI WA RAIS,WABUNGE NA MADIWANI

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Jaji  Mstaafu Damiani Lubuva akizungumza wakati wa mkuato wa kujadili maadili ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani katika mkutano uliofanyika Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam leo.
  Mkurugenzi wa uchaguzi, Julius Mallaba akizungumza leo katika mkutano wa kujadili maadili ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani katika mkutano uliofanyika Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam leo. 
  Baadhi ya viongozi wa vyombo vya siasa wakifuatilia kwa umakini katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
 Kamishina wa Polisi, Mussa Ali Mussa akizungumza kuhusiana na usalama kipindi cha kampeni na uchaguzi mkuu katika mkutano wa kujadili maadili ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani katika mkutano uliofanyika Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam leo.
Katibu Mkuu wa chama cha Tanzania Labour Part(TLP), Nancy Mrikalia akichangia maada katika mkutano wa kujadili maadili ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani katika mkutano uliofanyika Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam leo.
 
Na Avila kakingo, Globu ya jamii.
TUME ya uchaguzi NEC  wakishirikiana na viongozi wa vyama  vya siasa wakutana kujadili  maadili ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ikiwa tunaelekea katika uchaguzi mkuu utakaofanyika  Oktoba mwaka huu.

 Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Jaji  Mstaafu Damiani Lubuva, Kwenye ufunguzi wa mkutano wa tume na viongozi wa vyama vya siasa kuhusu maadili ya uchaguzi leo jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Jaji  Mstaafu Damiani Lubuva amesema kuwa kupiga kura ni haki ya msingi na ya kikatiba kwa kira raia wa Tanzania hivyo uchaguzi unatakiwa uwe wa haki, uhuru, uaminifu na wakuaminika.

Lubuva amesema kuwa  maadili yanayojadiliwa yahahusu zaidi  vyama vya siasa, wagombea wote, serikali pamoja na tume ya uchaguzi pia  kila chama na wagombea wanatakiwa kuheshimu na kutekeleza sheria za uchaguzi,kanuni na maadili na sheria nyingine za nchi katika kipindi cha kampeni kuanzia siku moja baada ya uteuzi hadi siku ya uchaguzi Oktoba mwaka huu.

Pia ametoa wito  kwa wanasiasa wote kuwaelimisha wafuasiwao kuondoka vituoni nara  baada ya kupiga kura ili kuepusha msongamano wa vitendo vingine vinavyoweza kuchochea kuvunjika kwa amani.

Kwa upande wa jeshi la polisi wametoa wito kwa wagombea wote watakao wania nafasi mbalimbali wafanye kampeni zake kipindi wakati kuna mwanga na si usiku ili kuepuka matatizo mbalimbali yatakayojitokeza.

No comments: