Sunday, July 5, 2015

MKUTANO WA DHARURA WA BARAZA LA MAWAZIRI WA AFRIKA MASHARIKI WAFUNGULIWA DAR ES SALAAM

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb.) akifungua Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki ambao pamoja na mambo mengine utapokea na kujadili taarifa ya ziara ya Mawaziri nchini Burundi kuhusu hali ya kisisasa nchini humo. Mkutano huo ambao ni maandalizi ya Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi utakaofanyika tarehe 06 Julai, 2015, umefanyika kwenye Hoteli ya Serena, Jijini Dar es Salaam tarehe 05 Julai, 2015.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Dkt. Richard Sezibera naye akizungumza wakati wa mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kulia) akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Joyce Mapunjo wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki uliokuwa ukiendelea katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam
Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nao wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Mkutano huo
Waziri wa Afrika Mashariki nchini Rwanda, Mhe. Valentine Rugwabiza (wa pili kushoto)  pamoja na wajumbe wengine waliohudhuria Mkutano huo. 
Balozi wa Tanzana nchini Burundi Mhe. Rajab Gamah (Kushoto) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda, Mhe. Henry Okello Oryem 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundara (Kushoto) akiwa na  Afisa Mwandamizi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Burundi, Bi. Victoria Mwakasege wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri.
Maafisa Mambo ya Nje nao wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri. Kutoka kushoto ni Bw. Ally Ubwa, Bi. Grace Martin na Bw. Mudrick Soraga
Mkutano ukiendelea
                                         Picha na Reginald Philip

No comments: