Wednesday, April 1, 2015

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI CHARLES KITWANGA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (Kushoto) na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava (kulia) wakiingia kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar es salaam kwa ajili ya kufungua mkutano wa baraza la wafanyakazi wa wizara ya nishati na madini unaoanza tarehe 01 hadi tarehe 02, Aprili 2015 wenye lengo la kujadili mafanikio na changamoto katika utendaji kazi wa Wizara pamoja na taasisi zake.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Afya na Serikali Kuu (TUGHE) Wizara ya Nishati na Madini, Marcelina Mshumbusi akisoma hotuba ya kumkaribisha Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava (hayupo pichani) katika mkutano huo. Kushoto ni Katibu wa TUGHE Wizara ya Nishati na Madini, Assa Mwakilembe.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini wakifuatilia kwa makini hotuba iliyokuwa inatolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (hayupo pichani).
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava (kulia) akisoma hotuba ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (wa kwanza kushoto). Katikati ni Katibu wa TUGHE Wizara ya Nishati na Madini, Assa Mwakilembe.
Sekretarieti inayoratibu mkutano wa baraza la wafanyakazi la Wizara ya Nishati na Madini wakisikiliza kwa makini na kunukuu mada zilizokuwa zinawasilishwa katika mkutano huo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga akifungua mkutano wa baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini.
Baadhi ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini wakiimba wimbo wa kuonyesha mshikamano ujulikanao kwa jina la “solidarity forever”.
Baadhi ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi kutoka Wizara ya Nishati na Madini wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa katika mkutano huo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (kushoto) akisalimiana na Mhasibu Mkuu Mfawidhi wa Wizara ya Nishati na Madini, Michael Marandu (kulia) mara baada ya kuwasili kwenye ukumbi wa mikutano ili kufungua mkutano huo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Kitwanga (katikati, waliokaa mbele) na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava ( wa pili kutoka kushoto, waliokaa mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi, Wizara ya Nishati na Madini.

No comments: