Wednesday, March 4, 2015

Waziri Membe akutana kwa mazungumzo na Balozi wa China hapa nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akizungumza na Balozi wa China nchini Mhe. Lu Youqing alipofika Wizarani kwa ajili ya mazungumzo  ya kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na China 
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya (kushoto), akiwa na  Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia Balozi Mbelwa Kairuki (wa pili kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano,  Bi. Mindi Kasiga na  Afisa Mambo ya Nje, Bw. Imani Njalikai (kulia) wakifuatilia mazungumzo kati ya Waziri Membe na Mhe. Lu Youqing ambao hawapo pichani.
Balozi Lu Youqing akizungumza na Mhe. Membe
Maafisa walioambatana na Balozi Lu wakinukuu mazungumzo akiwemo Kaimu Mkuu wa masuala ya Siasa katika Ubalozi huo, Bw. Li Xhuhang (kulia).   
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Nathaniel Kaaya (kulia)  na Katibu wa Waziri, Bw. Thobias Makoba nao wakisikiliza mazungumzo hayo.
Mazungumzo yakiendelea
WaziriMembe akiagana na Balozi Lu Youqing mara baada ya mazungumzo yao.
Picha na Reginald Philip.

No comments: