Sunday, March 1, 2015

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA AZINDUA HUDUMA ZA "DUTY FREE SHOP" MAGEREZA UYUI TABORA

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kushoto) akifunua kitambaa kwenye jiwe la msingi kuashilia uzinduzi rasmi wa "Duty Free Shop" ya Magereza Mkoani Tabora leo februari 28, 2015. Kamishna Jenerali Minja amesema kuwa Huduma hiyo itatolewa pia kwa Maafisa na Askari wa Vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama Mkoani Tabora(kulia) ni Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Transit Military Shop, Bw. Sadrudin Virji.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kushoto) akiangalia bidhaa mbalimbali zinazouzwa katika "Duty Free Shop" ya Magereza Mkoani Tabora mara tu baada ya uzinduzi rasmi leo februari 28, 2015 katika Viwanja vya Gereza Kuu Uyui, Tabora.
Muonekano wa Jengo la "Duty Free Shop" ya Magereza Mkoani Tabora ambalo limzunduliwa leo februari 28, 2015 na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani).
Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi katika uzinduzi rasmi wa "Duty Free Shop" ya Magereza Mkoani Tabora.
Kikundi cha ngoma za asili ambacho kinaundwa na Maafisa wa Jeshi la Magereza Mkoani Tabora kikitumbuiza katika hafla ya "Duty Free Shop" ya Magereza Mkoani Tabora.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Tabora(wa pili kulia) ni RPC Tabora, ACP Suzani Kaganda(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Shinyanga, SACP. Anet Laurent(wa pili kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Tabora, SACP. Rajab Mbilo(wa tatu kushoto) ni Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Transit Military Shop, Bw. Sadrudin Virji(wa tatu kulia) ni Katibu Tawala Mkoani Tabora, Bi. Kudra Mwinyimvua.(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments: