Tuesday, March 31, 2015

BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MILIONI 10 UJENZI WA KANISA LA KKKT USHARIKA WA MATOSA

 Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Matosa Kimara jijini Dar es Salaam, Rabisante Lema akimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei baada ya kukabidhi hundi ya sh. milioni 10 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa miundombinu ya kanisa hilo wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa. Jumla ya shilingi milioni 50 zilipatikana katika harambee hiyo. (Picha na Francis Dande)
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia) akimkabidhi hundi ya sh. millioni kumi Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Matosa Kimara jijini Dar es Salaam, Mhandisi Simon Kihunzi kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya kanisa hilo, wakati wa harambee iliyofanyika kanisani hapo, ambapo jumla ya shillingi milioni 50 zilipatikana. 
Godwin Semunyu akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charls Kimei baada ya kutoa mchango wake. Kulia ni Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Rabisante Lema.
Baadhi ya wazee wa kanisa wakiwa katika ibada hiyo.
Dk. Kimei akipiga mnada kikombe kilichoandikwa.
Martin Mmari akinunua kikombe kilichoandikwa jina lake, kikombe alikinunua kwa shilingi milioni moja.
Mfanyabiashara wa jijini Dar es Salaam, John Kyaruzi akipokea kikombe baada ya kukinunua kwa shilingi milioni moja katika harambee hiyo.
Ibada ikiendelea.
Waumini.
Waimbaji wa Kwaya Kuu.
Waumini.
Dk. Charle Kimei akiteta jambo na Lucy Naivasha (kulia).
Waumini wakishiriki kuimba nyimbo za injili.
Mchungaji Kiongozi Rabisante Lema akitoa mahubiri.
Dk. Charles Kimei akiteta jambo na Martin Mmari.
Waumini wakiwa katika ibada hiyo.
Dk. Charles Kimei akitoa neno.

Mayai yakisubiri kuuzwa katika harambee hiyo.

Asante kwa mchango wako wa sh. laki tano, Dk. Kimei akimshuru mchangiaji.
Lucy Naivasha akitoa neno la shukrani baada ya kutoa mchango wake.
Lucy Naivasha akipeana mkono na Dk. Charles Kimei.

No comments: