Monday, March 30, 2015

Balozi Mulamula azungumza na wanaDiaspora katika kongamano la mapambano dhidi ya gojwa la saratani duniani


Mhe.Liberatus Mulamula

Balozi wa Muungano ya Jamhuri ya Tanzania nchini Marekani, Mhe. Liberatus Mulamula, alipozungumza  katika kongamano  la mapambano dhidi ya gojwa la saratani duniani, aliwataka wanaDiaspora wa nchi za kiAfrika kuwa mstari wa mbele kwa kushirikiana na watalaamu wa vitengo vya afya duniani ili kuboresha upatikana wa huduma za afya barani Afrika. Mhe. Balozi Mulamula, ambaye pia ndie aliyekuwa mgeni rasmi katika kongamano hilo alizungumzia faida za kutumia Teknolojia  ili kuboresha mawasiliano kati ya wataalam, utafiti na  elimu . 
Nia mojawapo ya  kongamano la Global Health Catalyst Cancer Summit 2015 ni kuboresha huduma mahiri za saratani barani Afrika kwa  kutumia ( Information and Communication Technologies (ICTs);Teknolojia ya mawasiliano kati ya wataalam wa gojwa la saratani wa nchi za nchi za ng'ambo  na wataalam waliopo barani Afrika.Mhe. Balozi L. Mulamula, alikabidhi Tunzo Maalum kwa Bigwa wa Tiba ya Saraatani Dr. Twalibu Ngoma. Dr.Ngoma ni miongoni mwa wataalam wa kuigwa ambaye amepata elimu ya juu nje ya nchi na kureja nyumbani ili kuboresha upatikanaji wa huduma na elimu ya saratani nchini Tanzania
 Dr.Twalibu Ngoma
Proffesor na Mkuu wa Kituo cha Kliniki ya Mafunzo ya Sarataani kilichopo University ya Muhimbili Dar es salaam nchini Tanzania
       Mhe.Balozi Mulamula na waTanzania wanaDiaspora wakimpongeza Dr.Ngoma kwa furahaa

Uniting Africans in Diaspora (AID)  Against Cancer;
Sehemu ya pili  ya kongamano la Global Health Catalyst cancer  Summit ilijumuisha wanaDiaspora waafrika  ambao ni nguvu kubwa na rasilimali endelevu kwa katika nchi zao za kuzaliwa. Ripoti ya utafiti uliofanywa kwa baadhi ya viongozi wa  USA Afrikan Diaspora imedhihirisha kuwa karibu asilimia 90 % ya wanadiaspora wana nia na malengo ya kuleta mabadiliko katika nyanja mbali mbali nchini mwao ukiwemo uwanja wa afya  barani afrika.
Dr. Doyin Oluwole
      Mkurugenzi wa Taasisi ya Pink Ribbon Red Ribbon, jitihada zilizoanzishwa na   Rais  Mstaafu 
                                                              Mhe. George W. Bush 
Mashirika mbalimbali yalionyesha  mipango ya ujenzi wa vituo vya kutoa tiba ya saratani nchin Tanzania

Rais wa Jumuiya ya waTanzania DMV, Mhe. Iddi Sandaly alieleza nia ya wanaDaspora kuwa mstari wa mbele katika kuboresha upatikanaji wa huduma za afya  nchini Tanzania na malengo ya kupeleka huduma ya afya kwa jamii zenye uhitaji  hivi karibuni.

Mabigwa wa Saaratani mbalimbali duniani wakijadili njia bora  za kuborehsa huduma za saratani.

Ukosefu wa Elimu Afya kwa jamii ni kati ya changamoto zinazopelekea ongezeko la vifo vya gojwa la saratani barani Afrika. Saratani nyingi huweza kutibika endapo zimegundulika mapema na kupata utafiti na huduma sahihi.


Mwanzilishi wa http://www.nesiwangu.com/ ; mtandao unahusika na utoaji wa Elimu Afya kwa lugha ya kiswahili  Bi. harriet Shangarai, alizungumzia faida za kutoa Elimu Afya kwa kutumia lugha ya asilia na  kusema kuwa baadhi ya wasomaji wake walitafuta huduma ya haraka baada kujisomea na  kuelewa dalili  zenye kuashiria hitilafu katika mifumo mbali mbali mwilini. Bi. Harriet alizungumzia faida zitokanazo na Teknolojia ya mawasiliano ambayo ni fursa kubwa kwa Wanadiaspora kutoa mchango wao wa kielimu kwa jamii na kujenga mawasilino ya karibu na wataalam wa afya nchini mwao ili kwa pamoja waweze kushirikiana katika  kuziba  mapengo yaliyomo kwenye uwanja wa huduma na elimu ya afya.

Wataalam wa afya katika diaspora walipata fursa ya kujadili njia mbali mbali zitakazowawezesha kushirikiana  na kupata  fafanuzi za huduma za afya nchini mwao.


        Taasisi binafsi na vyombo mbali mbali vinavyotumika kuboresha huduma za saratani barani Afrika
                                Afrikan Women cancer Awareness association (AWCAA)


Mkurugenzi na Mwanzilishi wa African Women Cancer Awearness association NGO ( AWCAA)
Mrs.Ify Nwobuke (kushoto) na Mwakilishi wa AWCAA (kulia),  walizungumzi huduma za saratini ya matiti  mbazo wamekuwa wakizitoa barani Afrika. Mrs Ify alisema saratani ya matiti yaweza kutibika iwapo imegunduika mapema hivyo elimu kwa jamii ni muhimu katika mapambano ya saratani.

Shukrani;
Waandalizi wa Global Health Catalyst Cancer Summit @ Harvard Medical School, 2015
Kwa maelezo zaidi pitia


No comments: