Friday, February 27, 2015

Hatua za mwisho za Maandalizi Mbio za Kilimanjaro Marathoni 2015

Maandalizi ya mwisho ya kukarabati maeneo mbalimbali ya uwanja wa Chuo kikuu kutakapofanyika mbio za kimataifa za Kilimanjaro Marathoni.
Mabango mbalimbali yakiwa yamewekwa maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi kuashiria kuanza kwa shamrashamra za mbio za Kilimanjaro Marathoni.
Baadhi ya wageni wakijiandikisha kukimbia mbio ndefu za kilometa 42 ambapo zoezi la uandikishaji linafanyika katika hotel ya Keys mjini Moshi.
Washiriki wa mbio za Kilometa 21 zinazodhaminiwa na kampuni ya mawasiliano ya Tigo wakijiandikisha kwa ajili ya kupata namba maalumu wakati wa kukimbia mbio hizo. 
Baadhi ya wakimbiaji wakijaza fomu kwa ajili ya kukimbia mbio ndefu za km 42.
Wale wa mbio za Km 5 fun run pia walihakikisha wanafanya usajili wa ndugu zao pia.
Katika eneo la kujiadikishia unapata kiburudisho cha Grand Malt mara baada ya kupatiwa namba kwa ajili ya kushiriki mbio hizo.
Na Dixon Busagaga wa Globu 
ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: