Thursday, February 5, 2015

DKT. MAGUFULI AANZA ZIARA MKOANI TABORA

Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwahutubia wananchi wa Sikonge mkoani Tabora wakati alipopita kukagua barabara za mkoa huo. Dkt. Magufuli aliwaahidi wananchi hao wa Sikonge kuwa Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mpanda-Tabora kupitia Sikonge yenye zaidi ya kilomita 359 itakayofadhili na Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiagana na wananchi wa Sikonge mara baada ya kuwahutubia.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ludovick Mwananzila kushoto akizungumza na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli kabla ya kuhutubia mkutano kwa wananchi wa Tabora. Waziri Magufuli aliwaeleza wananchi kuwa Wizara ya Ujenzi itawasimamia kikamilifu Wakandarasi wanaojenga barabara katika mkoa huo na kuhakikisha miradi yote inakwisha kwa wakati.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwahutubia wakazi wa Tabora kuhusu ujenzi barabara za mkoa huo.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akisalimiana na wananchi mara baada ya mkutano wake alioufanya Tabora mjini.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ludovick Mwananzila akihutubia wananchi katika mkutano huo.
Mkuu wa Wilaya ya Mlele Col.Ngemela Eslom Lubinga akimuonesha Waziri wa Ujenzi ramani ya Wilaya ya Mlele katika sehemu linapojengwa daraja la Kavuu lenye urefu wa mita 84 litakalounganisha Kijiji cha Kibaoni na makao makuu ya Wilaya hiyo Inyonga.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwahutubia wananchi wa Inyonga Wilayani Mlele ambapo barabara ya Mpanda-Tabora itapita.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Col.Ngemela Eslom Lubinga mara baada ya kukagua ujenzi wa nyumba ya Mkuu huyo wa wilaya inayojengwa na Wakala wa Majengo (TBA) Wilayani Mlele mkoani Katavi.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiagana na wananchi wa Tabora mara baada ya kukugua mradi wa barabara ya Sikonge-Tabora.Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Ujenzi.

No comments: