Friday, January 30, 2015

ZIARA YA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII KWA SOKO LA MAREKANI YAENDELEA LOS ANGELES

Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii (TTB) Bi. Devota Mdachi akiongea katika hafla maalum ya kutangaza vivutio vya utalii kwa soko la Marekani katika Hoteli ya Four Seasons jijini Las Vegas.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dk. Adelhelm Meru (kulia) akiwa pamoja na Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii na Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa katika hafla maalum ya kutangaza vivutio vya utalii nchini kwa soko la Marekani.
Ujumbe wa Tanzania unaoshiriki ziara maalum ya kutangaza vivutio vya utalii kwa soko la Marekani.
Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii (TTB) Bi. Devota Mdachi akiwasilisha mada inayohusu vivutio vya utalii nchini katika hafla maalum ya kutangaza vivutio vya utalii kwa soko la Marekani katika Hoteli ya Four Seasons jijini Las Vegas.
Mwakilishi kutoka Kampuni ya Ndege ya Emirates Ndg. Akbar Hussein akiongea juu ya namna gani unaweza kufika Tanzania kwa kutumia usafiri wa Emirates.
Mwakilishi kutoka Kampuni ya Ndege ya Ethiopian Airlines akiongea juu ya namna gani unaweza kufika Tanzania kwa kutumia usafiri wa Ethiopina Airline.
Baadhi ya washiriki wa hafla maalum ya kutangaza vivutio vya utalii kwa soko la Marekani iliyofanyika katika Hoteli ya Four Seasons jijini Las Vegas.
Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii (TTB) Bi. Devota Mdachi akiongea na baadhi ya wageni waalikwa katika hafla maalum ya kutangaza vivutio vya utalii kwa soko la Marekani iliyofanyika katika Hoteli ya Four Seasons jijini Las Vegas.
Mwakilishi wa Ethiopian Airline (kati) akiongea katika hafla hiyo.Wengine pichani ni Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii na Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii (TTB) Bi. Devota Mdachi.

1 comment:

Kwa Imani said...


Naomba kufahamishwa vivutio vya utalii gani walivyotangaza.

Michuzi au yeyote aliyetoa habari hii, angeanisha vivutio walivyovitangaza huko Marekani.
ilikuwa ni kipindi kizuri kuvitangaza hivyo vivutio hata hapa nyumbani na kwingine vifahamike.