Tuesday, January 13, 2015

Mh. Mahiza Apania kuokoa miradi ya vijana na wanawake lindi

Na Abdulaziz Video,Globu ya Jamii - Lindi

Mkuu wa mkoa wa Lindi,Mwantumu Mahiza ameitaka halmashauri ya wilaya Ruangwa na halmashari nyingine za wilaya,miji,manispaa zilizopo mkoani Lindi ambazo hazijachangia na zisizo kamilisha kuchangikia mifuko ya vijana na wanawake zikamilishe kuchangia michango hiyo haraka.Mahiza alitoa agizo hilo mjini Ruangwa baada ya kupokea taarifa ya kazi za maendeleo katika wilaya hiyo iliyosomwa na kaimu mkuu wa wilaya hiyo,Regina Chonjo.

Mahiza alisema halmashauri za wilaya zinawajibu wa kuchingia mifuko hiyo kwa mujibu wa sheria badala ya kutafuta visingio vinavyosababisha kutimizwa nia njema ya serikali kwa makundi hayo maalum ya kijamii.Mkuu huyo wa mkoa ambaye yupo katika wilaya hiyo kwa ziara ya siku mbili ili kukagua na kuhimiza utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo.

Alibanisha kuwa suala la halmashauri za wilaya kutenga asilimia kumi ya mapato yake ya ndani ili kuchangia mifuko hiyo siyo jambo la hiari bali ni lazima.Hivyo halmashauri hiyo na nyingine zilizopo katika mkoa huu ambazo hazijachingia au zisizokamilisha michango hiyo zikamilishe michongo yake haraka."

mnatakiwa mtambue kuwa vijana na wanawake kupewa fedha hizo siyo zawadi bali ni haki yao,na ndiyo nia ya serikali wajiendeleze kiuchumi," alisema Mahiza.

Awali akisoma taarifa hiyo kaimu mkuu wa wilaya ya Ruangwa,Regina Chonjo alisema halmashauri ya wilaya ya Ruangwa katika mwaka wa fedha 2014/2015 imechangia shilingi 20,000,000.00 kutoka katika mapato yake ya ndani yaliyokusanywa hadi sasa,yenyejumla ya shilingi 946743451.72.

Ambapo katika kipindi hicho(2014/2015) imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi 6000000.00,kwa vikundi 16 vya wanawake vyenye wanachama 80.Huku ikiendelea kupokea maombi ya mikopo kutoka kwa vikundi mbali mbali vya vijana na wanawake
Mkuu wa Mkoa wa Lindi,Mh. Mwantumu Mahiza (wa pili kushoto) akiangalia namna ya kushuka kwa usalama baada ya kukagua mradi wa Umwagiliaji katika kijiji cha Chinokole wilayani Ruangwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa,Ruebern Mfune akimsaidia kupanda Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea ambae anakaimu wilaya ya Ruangwa,Mh. Regina Chonjo katika banio la umwagiliaji mara baada ya mkuu wa mkoa kutembelea kukagua mradi huo utakaosaidia jamii kwa kilimo cha umwagiliaji wilayani Ruangwa
Ujenzi ukiendelea katika jitihada za kuendeleza kituo cha umwagiliaji Chinokole wilayani Ruangwa.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi,Mh. Mwantumu Mahiza akipata maelezo juu ya kusimama kwa mradi wa ujenzi  wa ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Ruangwa toka kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi Bw Abdallah Chikota na alie kushoto ni Kaimu mkuu wa wilaya ya Ruangwa ambae pia ni Mkuu wa wilaya ya Nachingwea,Mh. Regina Chonjo.
Baadhi ya madiwani,wakuu wa Idara katika Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi wakisiliza Maagizo yaliyokwa yakitolewa na mkuu wa mkoa wa Lindi,Mh. Mwantumu Mahiza(Hayupo pichani)mara baada ya kumaliza ziara ya siku 2 wilayani humo kukagua shughuli za maendeleo.

No comments: