Tuesday, December 23, 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA RASMI MAJENGO YA TAASISI YA MAFUNZO YA UANASHERIA KWA VITENDO TANZANIA.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mbunge wa Ubungo Mhe. John Mnyika, wakati alipowasili kwenye viwanja vya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania kwa ajili ya kuzindua Taasisi hiyo iliyopo Ubungo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Waziri wa Sheria na Katiba Mhe Angelah Kairuki,
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa tatu kushoto) akikata utepe kuzindua rasmi Majengo ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Tanzania Law School) , wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam, leo Desemba
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki, walipoingia katika chumba maalum cha mafunzo ya Uanasheria kwa vitendo wakati wa uzinduzi wa Majengo ya Taasisi hiyo ya  Mafunzo ya Sheia
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki, kwa pamoja wakifunua kitambaa kuweka Jiwe la Msingi katika Majengo ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania, wakati wa hafla ya uzinduzi wa majengo hayo

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la viwanja vya Majengo ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania, baada ya kuzindua rasmi majengo hayo yaliyopo eneo la Ubungo, jijini Dar es Salaam
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya viongozi na wanafunzi wa Taasisi hiyo, baada ya uzinduzi.

 Baadhi ya wafanyakazi Viongozi na wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uzinduzi huo, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akihutubia, katika uzinduzi huo
 Sehemu ya wanafunzi kwenye uzinduzi huo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akizindua rasmi Majengo ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania, katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam
 Baadhi ya Viongozi na wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uzinduzi huo, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akihutubia, katika uzinduzi huo
 Wageni waalikwa kwenye uzinduzi huo
Baadhi ya  wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uzinduzi huo, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akihutubia, katika uzinduzi huo.
Picha na OMR

No comments: