Wednesday, October 22, 2014

TANZANIA YAWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUU WA NNE WA MASWALA YA USALAMA MITANDAO

Na Yusuph Kileo
Kumekua na makongamano, Mikutano na warsha mbali mbali zihusuzo maswala ya usalama mitandao katika mataifa mbali mbali ambapo mijadala ya kina kuhusiana na maswala ya usalama mitandao hufanywa. 
Mijadala yenye nia na madhumuni ya kuangazia macho maswala ambayo hivi sasa yamekua yakiitikisa dunia. Tanzania kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia(COSTECH) kwa kushirikiana na Tume ya Sayansi na Teknolojia kwa Maendeleo ya nchi za Kusini(COMSAT) na taasisi nyingine wameweza kuandaa warsha ya nne ambapo imefanyika kwa mara ya kwanza nchini Tanzania. 
Taarifa zaidi juu ya tukio hili pamoja na viambatanishi vingine muhimu vinaweza kusomeka “HAPA” “http://ykileo.blogspot.com/2014/10/warsha-ya-maswala-ya-usalama-mitandao.html
 KATIBU MKUU WIZARA YA SAYANSI MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA PROF. PATRICK MAKUNGU AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI JUU YA WARSHA YA USALAMA MITANDAO AMBAPO TANZANIA IMEKUA MWENYEJI WAKE.
 MKURUGENZI MKUU WA COSTECH NCHINI  DR. HASSAN MSHINDA AKITOA MANENO MACHACHE KATIKA UFUNGUZI WA WARSHA HIYO.
 WASHIRIKI  KUTOKA KATIKA MATAIFA MBALI MBALI WAKIENDELEA NA WARSHA.
 WASHIRIKI  KUTOKA KATIKA MATAIFA MBALI MBALI WAKIENDELEA NA WARSHA.
 PICHA YA PAMOJA NJE YA UKUMBI WA MKUTANO
 JOPO LA WANANDAAJI KUTOKEA WA WARSHA YA USALAMA MITANDAO KUTOKEA COMSAT  WAKIBADILISHANA MAWAZO NA WATAALAM WA NDANI  KUPANGA MIKAKATI ENDELEVU NA RAFIKI KUONGEZA UWEZO KWA WATAALAM WA NDANI.
KATIBU MKUU WIZARA YA SAYANSI MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA PROF. PATRICK MAKUNGU  (KUSHOTO) AKITAMBULISHWA NA BWANA YUSUPH KILEO BAADHI YA WASHIRIKI WA WARSHA HIYO - MMOJA KUTOKA KENYA  DR. WAUDO SIGANGA - MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WATAALAM WA TEHAMA NCHINI KENYA PAMOJA NA BWANA. TAJAMMUL HUSSAIN - MSHAURI WA COMSAT

No comments: