Monday, June 2, 2014

MGOMO BARIDI WA USAFIRI DAR ES SALAAM BAADA YA DALADALA KUZUIWA KUTUMIA KITUO CHA MWENGE NA KUTUMIA CHA MAKUMBUSHO

 Abiria wakiwa wanashangaa Daladala zinapita kituo cha Mwenge jijini Dar es salaam bila kusimama, ikiwa ni siku ya kwanza wasafirishaji hao kuamriwa kutumia kituo cha Makumbusho ambacho inaelekea hawaafiki.
 Daladala zikiwa zinapita bila kusimama sehemu yoyote
 Kituo cha kwenda Tegeta , Kawe na Mbezi kikiwa Kitupu Muda huu
 Kituo cha Mabasi Mwenye Cheupe hakuna hata Daladala hata moja
 Bajaji ndizo zimegeuka kuwa daladala na ni Tsh 1000 tu kwa mtu mmoja mpaka Mwenge
 Eneo ambalo Daladala zilikuwa nyingi sasa hakuna tena mabasi hayo

 Bajaji zikiendelea na Kazi
 Upande wa Mwenge kwenda Morocco Pia hakuna mabasi na kama yapo basi hayasimami
 Hali ya utulivu Mwenge
 Peupe hakuna Mabasi
 Abiria wakingoja Magari
 Wafanya Biashara Wadogo wadogo wakiwa wanajikusanya kwa ajili ya kujadili jinsi ya kuanza Mgomo na kushinikiza waanze kuweka meza zao pia hawataki ushuru
 Wafanya Biashara wakiwa wanaendelea kukusanyika ili kuandaa Mgomo wao
 Kushoto ni Meza moja ya Biashara ikiwa imeinuliwa ishara ya kuweka Meza na Kuanza Mgomo rasmi na kushinikiza kuwa waanze Biashara zao hapo kama kawaida na kutotaka ushuru wa kulipia pesa nyingi. Endelea Kufuatilia hapa... Mpaka tunaondoka eneo la tukio Polisi walikuwa wamesha wasili kwa kuanza Doria  na kuangalia usalama. Picha na Dar es salaam yetu blog

No comments: