Tuesday, November 19, 2013

MKUTANO WA TAWI LA CCM NEW YORK CITY

Meza kuu ya viongozi wa matawi ya CCM New York na DC wakimsikiliza msimamizi na msemaji mkuu wa mkutano huo bwana Isaac Kibodya. Mkutano wa CCM tawi la New York ulifanyika kwa mafanikio makubwa. Na hii ni mara ya kwanza kwa New York kuwa na tawi na kuweza kufanyika mkutano kama huu. Dhumuni la mkutano huo ni kuhamasisha Watanzania kujiunga na chama na kuchukua kadi hili mchakato wa kuchagua viongozi wapya watakao tambulika kichama na kiserikali.
Msimamizi wa mkutano huo Bwana Isaac Kibodya akizungumza, maneno muhimu ambayo bwana Kibodya alisisitiza katika mkutano huo ni kwanza ni mshikamano na umoja wa watanzania, pili ndiyo chama. Kwa sababu bila mshikamano kama watanzania hakuwezi kuwa na chama imara.
Katibu wamuda wa tawi Bwana Mseba akizungumza mbele ya wanachama katika mkutano huo. Bwana Mseba ndiyo mwimili mkubwa wa tawi la CCM New York.
Professor Lwiza Kamazima kati ya watu walikuwa bega kwa bega na Bwana Isaac Kibodya kufanikisha mkutano huo wa CCM kufanyika. Moyo wa kujitolea wa Profesa Lwiza ndiyo mafanikio ya kuwepo kwa mkutano huu kwa mara ya kwanza ndani ya jiji la wasiyo lala NYC.
 Loveness Mamuya au (Iron Lady) akiongea katika mkutano huo. Loveness kutoka DC ndiyo chanzo na chimbuko cha matawi yote ya CCM Marekani. Licha ya zengwe na kalinjekalinje alizokumbana nazo kwenye harakati za kufanisha kuwepo kwa matawi ya CCM Marekani lakini hakutetereka na kurudisha moyo wake nyuma. Loveness kasimama kidete kama mwanamke jasiri na kuyashinda majaribu yote.
Mwenyeketi wa muda wa tawi la CCM New York Bwana Mafutah akiongea jambo kwenye mkutano huo. Bwana Mafutah alikuwa Tanzania na alipata fursa ya kukutana na viongozi mbalimbali wa CCM.
Mzee Sebo mwenyekiti wa tawi la CCM DC akiongea machache katika mkutano huo. Kushoto kwake na Iron Lady Loveness na kulia kwa Mzee Sebo na Mafutah.
Mwanamusic wa kizazi kipya anaetamba na ngoma yake mpya inayojulikana kwa cheza cheza bila kukunja goti MwanaFA alikuwepo pia kutoa hamasa katika mkutano huo.
Watanzania waliojitokeza kwenye mkutano huo wakisikiliza kilichokuwa kinaendelea.
Mwenyekiti wa New York Tanzania Community Bwana Hajji Khamis alikuwepo pia kusikiliza kinachojili mkutanoni hapo
Wanachama wa CCM kutoka Springfield waliwepo pia kwenye mkutano huo 
Mkuu wa wilaya ya Springfield Bwana Isaac Kibodya akipata ukodac na Dullar wa Brooklyn.
Mweka hazina wa CCM tawi la DC kushoto akipiga ukodac na Bwana Mseba kulia
Dr Temba akipata ukodak na wageni kutoka DC.
Team kutoka DC ikipata ukodak.
Dr Temba akipata ukodak na mgeni kutoka DC.
Viongozi wa tawi la CCM DC wakipata ukodak wakiwa kwenye meza kuu.
 Dr Temba na rafikia yake Stanley
Mbuyu nao ulianza kama mchicha CCM Oyee 

1 comment:

KARIM said...

NIMEFURAHISHWA NA KUONA UWONGOZI MZURI WA TAWI HILO LA NEW YORK CITY NA VITONGOJI VYAKE.WALIO KUWA NA MICROPHONE NI WATU MAARUFU NA WANAWEZA UWONGOZI, KAMA VILE MAFTAH , KIBODYA NA KIONGOZI TOKA WASHINGTON AMBAE ALIKUWA MGENI RASMI. WOTE HAO WANAFAA KUONGOZA CCM UGHAIBUNI.
KARIM, LONDON