Tuesday, October 15, 2013

MTEMVU AMWAGIWA SIFA LUKUKI KWA KUWA KINARA WA MAENDELEO TEMEKE

 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (kulia), akihutubia katika mkutano wa jimbo uliofanyika eneo la Lumo, Kata ya Yombo Vituka, Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine alielezea miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM jimboni humo.
 Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Adam Kimbisa akihutubia katika mkutano wa Jimbo la Temeke eneo la Lumo, Yombo Vituka, Dar es Salaam , ambapo pamoja na mambo mengine aliwataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali kuwajali vijana kwa kuzipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali zinazowakabili. Kutoka kulia ni Mbunge wa jimbo hilo, Abbas Mtemvu, Meya wa Ilala, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Jerry Silaa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida.
Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Zungu (kushoto),  akihutubia na kummwagia sifa Mbunge wa Jimbo la Temeke, ambaye pia ni Mwenyekiti wa wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu (kulia),  kwa tabia yake ya kuwa karibu na jamii na kutetea maendeleo ya Temeke na Dar es Salaam jana katika mkutano wa jimbo hilo wa kuelezea miradi mbalimbali iliyotekelezwa jimboni humo kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM uliofanyika eneo la Lumo, Kata ya Yombo Vituka, wilayani humo.
 Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, Dk. Faustine Ndugulile akihutubia katika mkutano huo, ambapo naye alimmwagia sifa Mtemvu na kwamba yupo tayari kufuata nyayo zake.
 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (kulia), akihutubia katika mkutano wa jimbo uliofanyika eneo la Lumo, Kata ya Yombo Vituka, Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine alielezea miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM jimboni humo.
 Wasanii wa kikundi cha TMK Family, wakitumbuiza wakati wa mkutano wa Jimbo la Temeke, uliofanyika Lumo, Kata ya Yombo Vituka, Dar es Salaam . Katikati ni Mbunge wa jimbo hilo, Abbas Mtemvu (wa pili kushoto) akingana kucheza nao.
 Mtemvu akiendelea kusakata muziki
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida akihutubia katika mkutano huo
 Maofisa wa Kampuni ya Bravo inayosaidia kuwatafutia ajira wananchi wa jimbo hilo nje ya nchi, wakiwa kazini wakati wa mkutano huo
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, ambaye pia ni Meya wa Ilala, Jerry Silaa akimsifu Mtemvu kuwa ni mtu wa watu hivyo wana temeke wasije wakampoteza katika chaguzi zijazo.
 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (kulia), akihutubia katika mkutano wa jimbo uliofanyika eneo la Lumo, Kata ya Yombo Vituka, Dar es Salaam juzi, ambapo pamoja na mambo mengine alielezea miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM jimboni humo. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida, Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Jerry Silaa.
 Baadhi ya viongozi wa CCM wakiwa katika mkutano huo
 Baadhi ya viongozi wakisikiliza kwa makini wakati wa mkutano huo
 Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dar es Salaam,Mariam Kisangi akihutubia katika mkutano huo wa Jimbo la Temeke, uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CCM  pamoja na maofisa wa Manispaa ya Temeke.
 Mchumi wa Manispaa ya Temeke, Eric Kilangwa, akielezea kuhusu miradi mbalimbali iliyotekelezwa katika wilaya ya Temeke.
Mtmvu akijadiliana jambo na baadhi ya maofisa wa Manispaa ya Temeke.

No comments: