Saturday, March 31, 2012

Mzee Mkapa afunga kampeni za CCM jimbo la Arumeru mashariki kwa kishindo leo




 Rais Mstaafu wa awamu ya tatu,Mh. Benjamin William Mkapa akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kwa tikeki ya CCM,Sioi Sumari kwenye Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo hilo uliofanyika leo katika kijiji cha King'ori kata ya Leguruki.
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu,Mh. Benjamin William Mkapa akihutubia kwenye Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo Arumeru Mashariki uliofanyika leo katika kijiji cha King'ori kata ya Leguruki.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowasa akisalimia wananchi wa kijiji cha King'ori kata ya Leguruki wakati wa Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo Arumeru Mashariki leo.
Makamu Mwenyekiti wa CCM - Bara,Mh. Pius Msekwa akisalimia wananchi wa kijiji cha King'ori kata ya Leguruki wakati wa Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo Arumeru Mashariki leo.
Katibu Mkuu wa CCM,Mh. Wilson Mukama akisalimia wananchi wa kijiji cha King'ori kata ya Leguruki wakati wa Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo Arumeru Mashariki leo.
Mgombea  Ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kwa tiketi ya CCM,Sioi Sumari akihutubia kwenye Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo Arumeru Mashariki uliofanyika leo katika kijiji cha King'ori kata ya Leguruki.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye akisalimia wananchi wa kijiji cha King'ori kata ya Leguruki wakati wa Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo Arumeru Mashariki leo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - Mahusiano na Uratibu,Stephen Wassira akisalimia wananchi wa kijiji cha King'ori kata ya Leguruki wakati wa Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo Arumeru Mashariki leo.
Wabunge toka sehemu mbali mbali ambao wapo Arumeru Kumsaidia Kampeni Mgombea Ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki wakisalimia wananchi wa kijiji cha King'ori kata ya Leguruki wakati wa Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo Arumeru Mashariki leo.
Waziri Mkuu Mstaafu,Mh. Edward Lowasa akiwasili kwenye  viwanja vya kijiji cha King'ori kata ya Leguruki wakati wa Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo Arumeru Mashariki leo.
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu,Mh. Benjamin William Mkapa akisalimiana na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kwa tikeki ya CCM,Sioi Sumari wakati akiwasili kwenye Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo hilo uliofanyika leo katika kijiji cha King'ori kata ya Leguruki.
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu,Mh. Benjamin Mkapa pamoja na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kwa tikeki ya CCM,Sioi Sumari wakisalimia wananchi wakati wakiwasili kwenye Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo hilo uliofanyika leo katika kijiji cha King'ori kata ya Leguruki.
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu,Mh. Benjamin Mkapa akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu,Mh. Edward Lowasa wakati akiwasili viwanjani hapo.
Mama Mzazi wa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki,akisalimia wananchi wa Kijiji hicho.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowasa akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Simanjiro,Mh. Christopher Ole Sendeka mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo Arumeru Mashariki uliofanyika leo katika kijiji cha King'ori kata ya Leguruki.
Mh. Mkapa akiagana na Mh. Peter Serukamba.
Mh. Edward Lowasa akijadiliana jambo la Mh. January Makamba.
Mh. Lowasa akiagana na wananchi wa kijiji cha King'ori kata ya Leguruki.
Meza kuu.

WATEULE NA WASHINDI WA TUZO YA WANAHABARI BORA 2011

Rais Jakaya kikwete katika picha ya pamoja na meza kuu pamoja na washindi wa Tuzo ya Wanahabari Bora wa Mwaka 2011 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam

ORODHA YA WATEULE NA WASHINDI
TUZO YA MPIGA PICHA BORA
Wateule ni :   
1.      Abdallah Bakari – Mwananchi, Dar es Salaam
2.      Khalifan Said – The Guardian , Dar es Salaam
3.      Khamis Said Hamad – Uhuru, Dar es Salaam
Na Mshindi ni: Khamis Said Hamad kutoka gazeti la Uhuru,  Dar es Salaam . Picha iliyomfanya kuwa mshindi ilihusiana na mazishi ya watu waliopata ajali katika basi la  Delux.  
Atakayekabidhi zawadi ni: Aggrey Marealle, Mkurugenzi Mtendaji, Executive Solutions Limited. Kampuni hii inashughulika na masuala mbalimbali yanayohusiana na mambo ya habari.

TUZO YA MCHORAJI BORA WA VIBONZO
Wateule ni: 
1.      Said Michael –  Tanzania Daima, Dar es Salaam 
2.      Nathan Mpangala – Majira, Dar es Salaam
3.      Samuel Mwamkinga –The Citizen, Dar es Salaam
Na Mshindi ni: Nathan Mpangala wa gazeti la Majira, Dar es Salaam. Kibonzo kilichomfanya ashinde kinahusiana na jitihada za Wabunge kujiongezea posho huku wananchi wakiteseka.
Atakayekabidhi zawadi atakuwa ni Hellen Kijo Bisimba, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu. Mwaka 2008 alishinda Zawadi ya Mwanamke Jasiri iliyotolewa na Ubalozi wa Marekani.


TUZO YA HABARI ZA UTAWALA BORA –MAGAZETI 
Wateule ni:
1.      Joseph Zablon  – Mwananachi , Dar es Salaam
2.      Neville Meena – Mwananchi , Dar es Salaam
3.      Fredrick Katulanda – Mwananchi, Dar es Salaam

Na Mshindi ni: Neville Meena kutoka gazeti la Mwananchi, Dar es Salaam. Habari iliyompa ushindi inasema “Tuhuma za Rushwa wizara ya Nishati na Madini”

Atakayekabidhi zawadi ni: Afisa Mtendaji Mkuu wa Serengeti breweries Limited. Serengeti wamekuwa mstari wa mbele kutoa misaada ya kijamii katika Nyanja za michezo, elimu, habari na hifadhi za taifa. Serengeti Breweries Limited pia ni wahisani wa EJAT.

TUZO YA HABARI ZA UTAWALA BORA – TELEVISHENI  
Wateule ni:
1.      Jamaly Said – TBC , Dar es Salaam
2.      Emmanuel Buholela – ITV, Dar es Salaam
Na Mshindi ni: Emmanuel Buholela, wa ITV, Dar es Salaam. Habari iliyompa ushindi ni “Migogoro ya Ardhi inayoweza kuleta uhasama katika jamii.
Atakayekabidhi zawadi ni: Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya EXIM. EXIM ni mojawapo ya benki ambazo zimekuwa zikitoa misaada kwa wanajamii. EXIM imeahidi kushirikiana na EJAT katika kuandaa Tuzo za mwaka ujao

TUZO YA HABARI ZA UTAWALA BORA –RADIO  
Wateule ni:
1.      Latifu Said Matimbwa  – TBC Taifa, Dar es Salaam
2.      Noel Thomson – Radio Afya , Mwanza
Na Mshindi ni: Noel Thomson wa Afya Radio – Mwanza. Habari iliyompa ushindi ni “Kutowajibika kwa viongozi na kusababisha hali mbaya ya choo shuleni
Atakayekabidhi Zawadi ni Ernest Sungura. Sungura ni Mkuu wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF). TMF ni mfuko uliobuniwa kwa lengo la kuongeza ubora na uhuru katika vyombo vya habari hasa kwa kuweka mkazo katika habari za uchunguzi na habari zenye mvuto kwa jamii.

TUZO YA HABARI ZA MALARIA – MAGAZETI
Wateule ni:  
1.      Audax Mutiganzi – Rai – Bukoba
Na Mshindi ni: Audax Mutiganzi wa  gazeti la Rai, Bukoba. Habari iliyompa ushindi ni “Dawa ya Ukoko ilivyopunguza maambukizi ya malaria Bukoba
Atakayekabidhi Zawadi ni Rob Ainslie, Mkuu wa COMMIT, Commit ni mpango wa kupambana na Malaria nchini Tanzania. Mpango huu unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la USAID. Mpango huu pia ni washirika wa EJAT.

TUZO YA HABARI ZA MALARIA  – TELEVISHINI  
Hakuna Wateule, Hakuna Mshindi

TUZO YA HABARI ZA MALARIA  – RADIO
Wateule ni :
1. Noel Thomson – Afya Radio, Mwanza 
2.      Gervas Hubile – TBC Taifa, Dar es Salaam
Na Mshindi ni:  Gervas Hubile  wa TBC Taifa. Habari iliyompa ushindi ni “Ukubwa wa tatizo la malaria vijijini na namna ya kukabiliana nalo.”
Atakayekabidhi  Zawadi ni Andrew Rebold. Rebold ni Naibu Mkuu wa Timu ya Masuala ya Afya katika Shirika la Misaada la Marekani (USAID).

TUZO YA HABARI ZA MICHEZO NA UTAMADUNI – MAGAZETI 
Wateule ni:
1.      Abdallah Msuya – Daily News, Dar es Salaam
2.      Iman Mani – Daily News, Dar es Salaam
Na Mshindi ni Iman Mani wa Daily NewsDar es Salaam. Habari iliyompa ushindi ni “Staging community theatre challenges.”
Atakayekabidhi Zawadi ni Leonard Thadeo. Bw. Thadeo ni Mkurugenzi wa Michezo, wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

TUZO YA HABARI ZA MICHEZO NA UTAMADUNI –TELEVISSHENI  
Wateule ni :
1.      Anuary Mkama – Mlimani TV, Dar es Salaam
Mshindi ni Anuary Mkama wa Mlimani TV, Dar es Salaam. Habari iliyompa ushindi ni  “Sababu za kuzorota mpira wa miguu mkoani Arusha.”
Atakayekabidhi Zawadi ni Dioniz Malinzi .Bw. Malinzi ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT).

TUZO YA HABARI ZA MICHEZO NA UTAMADUNI –RADIO 
Wateule ni:
1.      Adeladius Makwega – TBC Taifa , Dar es Salaam
2.      Dorice Kaunda –TBC Taifa, Dar es Salaam
3.      Abdallah Majura – Sport FM – Dodoma
Na Mshindi ni Abdallah Majura wa  Sport FM – Dodoma . Habari iliyompa ushindi ni “Tanzania kushindwa kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika kwa miaka 30.”
Atakayekabidhi Zawadi ni Atakayekabidhi zawadi ni : Absalom Kibanda- Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF). Jukwaa hili linawaunganisha wahariri wapatao 85 kutoka vyombo vyote vya habari.

TUZO YA HABARI ZA WATU WENYE WENYE ULEMAVU – MAGAZETI  
Wateule ni: 
1.      David Azaria – Habari Leo – Mwanza
2.      David Azaria – Habari Leo –Mwanza (He had two stories which entered the final)
3.      Joas Kaijage – The Citizen – Kagera
Na Mshindi ni:  David Azaria wa Habari Leo, Mwanza. Habari iliyompa ushindi ni  “Albino alivyokataa kutoka hospitali kwa kuhofia kuuawa.”
Atakayekabidhi Zawadi ni:  Reginald Mengi. Mengi ni Mwenyekiti wa IPP Media. Pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT). MOAT piani washirika wa EJAT.   Bw. Mengi ni amekuwa akitoa misaada mingi kwa watu wenye ulemavu. Kwa sasa ni Mwenyekiti wa Mfuko wa Watu wenye Ulemavu Tanzania.

TUZO YA HABARI ZA WATU WENYE WENYE ULEMAVU – TELEVISHENI   

Wateule ni:
1.      Stanley Ganzel – TBC, Dar es Salaam
2.      Lekoko Piniel Ole Levilal – Channel 10, Dar es Salaam

Na Mshindi ni : Lekoko Piniel Ole Levilal  wa Channel 10, Dar es Salaam. Habari iliyompa ushindi ni  “Sababu za kuwatenga na kuwanyanyasa walemavu.”
Atakayekabidhi zawadi ni : Haika Mawala, Naibu  Afisa Mtendaji Mkuu wa  CCBRT. CCBRT  imekuwa ikijishughulisha na utoaji wa huduma ya afya  na huduma nyingine kwa watu wenye ulemavu.


TUZO YA HABARI ZA WATU WENYE WENYE ULEMAVU – RADIO   
Wateule ni :
1.      Mwamini Andrew – TBC Taifa , Dar es Salaam
2.      Tuma Dandi – Radio Mlimani , Dar es Salaam

Na Mshindi ni:  Tuma Dandi wa Radio Mlimani, Dar es Salaam. Habari iliyompa ushindi ni “Wagonjwa walemavu wa akili na mimba, ubakaji na ukimwi.”
Atakayekabidhi zawadi ni : Dk. Bohela Lunogelo,  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utafiti wa  Uchumi na masuala ya kijamii.


TUZO YA HABARI ZA JINSIA – MAGAZETI   
Wateule ni :
1.      Nasra Abdallah – Tanzania Daima, Dar es Salaam

Na Mshindi ni Nasra Abdallah wa Tanzania Daima, Dar es Salaam. Habari iliyompa ushindi ni “Kazi za ndani ndizo zilizonifikisha hapa nilipo.”
Atakayekabidhi  zawadi ni Bibi Mwanahamisi Salumu Singano kutoka Oxfam.




TUZO YA HABARI ZA JINSIA  – TELEVISHENI    
Hakuna Wateule, Hakuna Mshindi

TUZO YA HABARI ZA JINSIA  –RADIO
Hakuna Mteule, Hakuna Mshindi

TUZO YA HABARI ZA UKIMWI /VVU  – MAGAZETI 
Wateule ni: 
1.      Abdallah Bakari – Mwananchi , Dar es Salaam
2.      Elias Msuya – Mwananchi, Dar es Salaam
Na Mshindi ni: Elias Msuya wa  gazeti la Mwananchi, Dar es Salaam. Habari iliyompa ushindi ni “Sipati picha maisha haya ya ukimwi. Napiga moyo konde kuishi na ukimwi.”
Atakayekabidhi zawadi ni: Dr. Fatma Mrisho, Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Ukimwi (TACAIDS). Tume hii ndiyo inayotoa miongozo na mikakati kuhusu namna ya kupambana na ukimwi.

TUZO YA HABARI ZA UKIMWI /VVU  – TELEVISHENI  
Hakuna Wateule, Hakuna Mshindi

TUZO YA HABARI ZA UKIMWI /VVU  – RADIO  
Wateule ni:
1.      Rehab Fred – Radio Free Africa – Dar es Salaam
2.      Beatrice Nangawe – Sunrise Radio,  Arusha 
Na Mshindi ni: Beatrice Nangawe wa  Sunrise Radio, Arusha. Habari iliyompa ushindi ni “Ukimwi ni huu: jinsi biashara ya ukahaba inavyoshamiri wilayani Karatu na jamii isivyojali afya zao.”

Atakayekabidhi Zawadi ni: Ernest Shumashike- Mkurugenzi Mtendaji wa ECOPRINT. Ecoprint ndiye aliyechapa ratiba ya Sherehe za Utoaji wa Tuzo hizi na hotuba ya Katibu Mtendaji wa MCT. Amefanya hivyo bila malipo. Na maekuwa akifanya hivyo tangu 2009.

TUZO YA HABARI ZA AFYA  – MAGAZETI 
Wateule ni: 
1.      Fredy Azzah – Mwananchi, Dar es Salaam
2.      Sharifa Kalokola – The Citizen, dare s Salam
3.      Lilian Rugakingira – Mwananchi- Kagera

Na Mshindi ni: Sharifa Kalokola wa gazeti la The Citizen Newspaper, Dar es Salaam. Habari iliyompa ushindi ni  “ Abortion pills sold over the counter.”

Atakayekabidhi zawadi ni: Jaji Thomas Mihayo. Jaji Mihayo ni Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu Tanzania. Ni Rais wa Chama cha Majaji Wastaafu. Ni Mjumbe wa Bodi ya Baraza la Habari Tanzania. Ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Baraza la Habari Tanzania (MCT).

TUZO YA HABARI ZA AFYA – TELEVISHENI 
Hakuna Wateule, Hakuna Mshindi

TUZO YA HABARI ZA AFYA  – RADIO  
Wateule ni:
1.      Catherine Nchimbi – TBC Taifa, Dar es Salaam 
2.      Secilia Ndabigeze – Afya Radio- Mwanza
3.      Faraja John Sendegeya – Afya Radio – Mwanza

Na Mshindi ni: Secilia Ndabigize wa  Afya Radio, Mwanza. Habari iliyompa ushindi ni “Utoaji wa meno kwa watoto na mila na desturi zilizojengeka.”

Atakayetoa zawadi ni: Dr. Marina Njelekela. Dk. Njelekela ni Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili. Dk. Njelekela alipata umaarufu baada ya kuongoza chama cha Madaktari wanawake katika kampeni za kuwaelimisha watu na kupima kansa ya maziwa.


TUZO YA HABARI ZA MAZINGIRA  – MAGAZETI
Wateule ni: 
1.      Mary Mahundi – Mwananchi, Dar es Salaam
2.      Felix Mwakyembe – Raia Mwema, Mbeya
3.      Lucas Liganga – The Citizen, Dar es Salaam
Na Mshindi ni: Lucas Liganga wa gazeti la The Citizen, Dar es Salaam. Habari iliyompa ushindi ni: “Illegal fishing in Lake Victoria threatens to wipe out Nile Perch affecting jobs of hundreds of thousands of people.
Atakayekabidhi zawadi ni: Dk. Emmanuel Nchimbi (MB). Dk.  Emmanuel Nchimbi ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Kwa maana hiyo yeye ndiye waziri ambaye anahusika zaidi na masuala ya EJAT.

TUZO YA HABARI ZA MAZINGIRA  –TELEVISHENI 
Hakuna Wateule, Hakuna Mshindi


TUZO YA MAZINGIRA - RADIO 
Hakuna Wateule, Hakuna Mshindi

TUZO YA HABARI ZA UCHUMI NA BIASHARA – MAGAZETI  
Wateule ni:
1.      Happy Severine - Mtwara
2.      Polycarp Machira – The Citizen, Dar es Salaam 
3.      Edith Karlo – Mtanzania - Kigoma 

Na Mshindi ni: Polycarp Machira wa The Citizen, Dar es Salaam. Habari iliyompa ushindi ni  “Chinese show rae business acumen in Dar es Salaam

Atakayetoa Zawadi ni :  Afisa Mtendaji Mkuu wa FINCA.  Finca ni mmojawapo wa wahisani wa EJAT. Wao walidhamini Tuzo za Habari za Uchumi na Biashara. Finca imeanzisha mradi wake wa kuwatoa mikopo kwa wanawake vijijini kwa lengo la kuwawezesha wanajamii kiuchumi na katika masuala ya kujiptia huduma ya afya, elimu na huduma nyingine.

TUZO YA HABARI ZA UCHUMI NA BIASHARA – TELEVISHENI I  
Wateule ni:
1.      Aneth Andrew – TBC , Dar es Salaam

Na Mshindi ni: Aneth Andrewwa  TBC, Dar es Salaam.  Habari iliyompa ushindi ni  “Faida za zao la zabibu na changamoto zinazowakabili wakulima.”
Atakayekabidhi Zawadi ni:  Afisa Mtendaji Mkuu wa Barclays Bank .

TUZO YA HABARI ZA UCHUMI NA BIASHARA – TELEVISHENI I  
Hakuna Wateule, Hakuna Mshindi

TUZO YA HABARI ZA ELIMU – MAGAZETI
Wateule ni:
     1.Frank Leonard – Habari Leo
     2.Erick Kabendera – The Citizen, Dar es Salaam
3.Angela Sebastian – Uhuru, Dar es Salaam

Na Mshindi ni: Erick Kabendera wa gazeti la The Citizen. Habari iliyompa ushindi ni “Wards Secondary Schools : A lost generation in science and technology.”

Atakayekabidhi zawadi ni:   Elizabeth Missokia, Mkurugenzi Mtendaji wa  wa  HakiElimu.   HakiElimu ni mshirika wa EJAT Partner.  HakiElimu inalenga kuleta usawa, ubora, haki za binadamu na demokrasia katika kuleta  magezi katika mfumo wa shule na sera za elimu.


TUZO YA HABARI ZA ELIMU – TELEVISHENI 
Wateule ni:
1.      Victoria Patrick – TBC, Dodoma
Na Mshindi ni: Victoria Patrick wa  TBC, Dodoma. Habari iliyompa ushindi ni “ Elimu ya watu wazima wasiojua kusoma na kuandika.”
Atakayekabishi zawadi ni : Sabasaba K. Moshingi, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB). Benki ya Posta ni mojawapo ya wahisani wa EJAT.

TUZO YA HABARI ZA ELIMU -RADIO 
Wateule ni:
1.      Grace Kiondo- Zenj FM, Zanzibar
2.      Mwamini Andrew – TBC Taifa, Dar es Salaam
Na Mshindi ni:  Grace Kiondo  wa Zenj FM,  Zanzibar. Habari  iliyompa ushindi ni  “Watoto na changamoto za elimu.”

Atakeyekabidhi zawadi ni Prof. B. Killian.  Prof Killian ni Mkuu wa Shule Kuu ya Uandishi wa Habari , Chuo Kiku cha Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendajiwa Mlimani TV, Radio Mlimani and the Hill Observer.

TUZO YA HABARI ZA WATOTO –  MAGAZETI 
Wateule ni :
1.      Fredy Azzah –Mwananchi, Dar es Salaam
2.      Nashon Kennedy – Habari Leo, Mwanza

Na Mshindi ni: Nashon Kennedy wa Habari Leo, Mwanza. Habari iliyompa ushindi ni “Mtoto aliyeolewa na kukeketwa.”

Atakayekabidhi zawadi ni:  James Marenga kutoka Nola. Nola ni taasisi ambayo imekuwa ikitoa msaada wa kisheria na kutoa elimu ya sheria.

 TUZO YA HABARI ZA WATOTO  – TELEVISHENI  
Wateule ni :
1.      Anganile Mwakyanjala – TBC , Dar es Salaam
Na Mshindi ni:  Angenile Mwakyanjala wa TBC . Habari iliyompa ushindi ni “Matatizo ya Watoto wa Mitaani”

Atakayekabidhi zawadi ni:  Ussu Mallya Usu Mallya ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) .
TUZO YA HABARI ZA WATOTO - RADIO  
Wateule ni : 
1.      Mulhat Said- Chuchu Radio, Zanzibar
2.      Sempanga Zawadi Mchome – Sauti ya Injili - Kilimanjaro

Na Mshindi ni : Sempanga Zawadi Nchome wa Sauti ya Injili, Kilimanjaro  Habari iliyompa ushindi ni  “Watoto na viboko shuleni – Viendelee au vitolewe”

Atakayetoa Zawadi ni Johnson Mbwambo. Johnson Mbwambo ni Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira.

TUZO YA HABARI ZA HIFADHI ZA TAIFA – MAGAZETI    
Wateule ni:
       1. Iman Mani – Daily News, Dar es Salaam
       2. Joseph Zablon – Mwananchi, Dar es Salaam
3.      Paul James Sarwatt – Raia Mwema –Arusha
Na Mshindi ni: Paul James Sarwatt wa Raia Mwema . Habari iliyompa ushindi ni “Ufisadi Maliasili.”
Atakayekabidhi zawadi ni : Modestus Lilungulu, huyu  ni Mwenyekiti  wa Bodi ya Tanzania National Parks Authority (TANAPA).  TANAPA ni shirika linalojihusisha na uangalizi na udhibiti wa Mbuga za Taifa kwa ajili ya matumizi ya sasa na vizazi vijavyo.

TUZO YA HABARI ZA HIFADHI ZA TAIFA  – TELEVISHENI    
Hakuna Wateule, Hakuna Mshindi 

TUZO YA HABARI ZA HIFADHI ZA TAIFA  – RADIO    
Wateule  ni:
1.      Alex Magwiza – TBC Taifa , Dar es Salaam

Na Mshindi ni: lex Magwiza from TBC Taifa,  Dar es Salam. Habari iliyompa ushindi ni “Faida za hifadhi za Taifa- Mkomazi na Arusha kwa wananchi waishio jirani nazo.”
Atakayekabidhi zawadi :  Simon Kivamwo, Mwenyekiti wa Association of Journalists Against Aids (AJAAT). AJAAT is EJAT’s partner.

TUZO YA HABARI ZA UTALII WA NDANI – MAGAZETI 
Wateule ni: 
1.      Albano Midelo – Nipashe –Songea
2.      Monica Luwondo – The Guardian – Arusha
3.      Gordon Kalulunga – Mtanzania – Mbeya

Na Mshindi ni: Monica Luwondo wa the Guardian, Arusha. Habari iliyompa ushindi ni “ Wazawa wanavyobadilika na kuanza kutembelea vivutio vya ndani.”
The Presenter of the Award is: Dk. Marcelina Chijoriga, Mjumbe wa Bodi ya TANAPA.

TUZO YA HABARI ZA UTALII WA NDANI – TELEVISHENI  
Wateule ni:
1.      Cassius Mdami – Channel 10, Dar es Salaam
2.      Juma Nugaz – Clouds TV, Dar es Salaam
Na Mshindi ni:  Juma Nugaz wa  Clouds TV  Dar es Salaam . Habari iliyompa ushindi ni “Maisha na Utamaduni wa Wahadzabe.”

Atakayekabidhiwa Zawadi ni : Ananilea Nkya,  Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA). TAMWA ni mmojawapo wa washirika wa EJAT

TUZO YA HABARI ZA UTALII WA NDANI – RADIO  
Hakuna Wateule, Hakuna Mshindi 

TUZO YA HABARI ZA MAAFA NA MIGOGORO – MAGAZETI 
Wateule ni:
1.      Tom Masoba – The Citizen , Dar es Salaam
2.      Bernard James –  The Citizen , Dar es Salaam
3.      Daniel Mbega – The Citizen, Dar es Salaam
Na Mshindi ni is: Daniel Mbega from The CitizenDar es Salaam . Habari iliyompa ushindi ni: “Technical error to blame for land conflict in Kapunga Rice Project

Atakayekabidhi Zawadi ni : Afisa Mtendaji Mkuu wa Regalia Media Limited. Regalia Media Limited ni kampuni inayojihusisha na masuala ya habari na mahusiano ya jamii. Regalia Media Limited ni mojawapo ya Wahisani wa EJAT.

TUZO YA HABARI ZA MAAFA NA MIGOGORO – TELEVISHENI  
Hakuna Wateule, Hakuna Mshindi


TUZO YA HABARI ZA MAAFA NA MIGOGORO – RADIO