Friday, November 30, 2018

BURUNDI YAKWAMISHA MKUTANO 20 WA WAKUU WA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Na. Vero Ignatus, Arusha

Mkutano wa 20 wakuu wa nchi za jumuiya ya Afrika ya mashariki uliokuwa ufanyike leo Mkoani Arusha umeaihirishwa.

Akitaja sababu za kuahirishwa kwa mkutano huo Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika ya mashariki kutoka Uganda Kirunda Kivejinja amesema nchi ya Burundi imekwamisha mkutano huo kwa kitokutuma muwakilishi

Waziri wa mambo ya nje ya nchi ya Tanzania Mhe. Augustino Mahiga amesema marais wawili wa Sudan ya Kusini na Rwanda wametuma wawakilishi lakini Rais wa Burudi hakutuma muwakilishi yeyote kwenye vikao vyote

'' Kwenye mikutano kama hii kuna kuwa na maandalizi ya ngazi tatu kwanza ni maafisa wataalam,makatibu wakuu na mwisho ya mawaziri na hatimaye inakuwa mkutano wawakuu lakini Burundi haikuleta wawakilishi kabisa na hawakutoa maelezo hivyo hatujui ninini kiewapata''alisema Mahiga

Hivyo kutokana na sheria za mkataba wa Afrika ya Mashariki kikao cha mawaziri kilishindwa kuchukua maamuzi, kwani hata kikao cha maamuzi lazima kiwe na wawakilishi kutoka nchi zote sita ."Hivyo kikao cha mawaziri hakikutoa maamuzi yeyote, tulijadiliana tu hayo ni kutokana na kilichopo katika mkataba wetu"

Amesema kuwa Marais na mawaziri walipokuja walikuwa na matumaini kuwa pengine Burundi wangetuma taarifa ama wawakilishi lakini toka walipoanza mkutano asubuhi kulikuwa hakuna taarifa yeyote hivyo wakuu wa nchi walipokutana wakaona haitawezekana kuendelea na mkutano huo

"Na hata kama wangekuwa wanazungumza mazungumzo yao yasimgelikuwa na mashiko kisheria na maamuzi ya kisheria kwahiyo wakaamua huu mkutano uhairishwe ndiyo maana huo mkutano ukaahirishwa" alisema Mahiga. Hata hivyo Mahiga amesema itawalazimu kufanya mkutano mkuu wa Wakuu wa nchi zote sita na ni lazima iwe ndani ya mwaka huu, na ndani ya mwezi disemba 2018 kikatiba

Jumuiya ya Afrika Mashariki inaundwa na nchi sita ikiwemo Tanzani, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Sudani Kusini.Mkutano huo wa 20 wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliokuwa umebeba kauli mbiu isemayo kuhuisha utengamano wa kijamii, kisiasa na kiuchumi wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki


Mkutano wa 20 wakuu wa nchi za jumuiya ya Afrika ya mashariki uliokuwa ufanyike leo Mkoani Arusha umeairishwa.

Akitaja sababu za kuahirishwa kwa mkutano huo Mwenyekiti wa Baraza la  Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika ya mashariki kutoka Uganda Kirunda Kivejinja amesema nchi ya Burundi imekwamisha mkutano huo kwa kitokutuma muwakilishi

Waziri wa mambo ya nje ya nchi ya Tanzania Mhe. Augustino Mahiga amesema marais wawili wa Sudan ya Kusini na Rwanda wametuma wawakilishi lakini Rais wa Burudi hakutuma muwakilishi yeyote kwenye vikao vyote

'' Kwenye mikutano kama hii kuna kuwa na maandalizi ya ngazi tatu kwanza ni maafisa wataalam,makatibu wakuu na mwisho ya mawaziri na hatimaye inakuwa mkutano wawakuu lakini Burundi haikuleta wawakilishi kabisa na hawakutoa maelezo hivyo hatujui ninini kiewapata''alisema Mahiga

Hivyo kutokana na sheria za mkataba wa Afrika ya Mashariki kikao cha mawaziri kilishindwa kuchukua maamuzi, kwani hata kikao cha maamuzi lazima kiwe na wawakilishi kutoka nchi zote sita . "Hivyo kikao cha mawaziri hakikutoa maamuzi yeyote, tulijadiliana tu hayo ni kutokana na kilichopo katika mkataba wetu"

Amesema kuwa Marais na mawaziri walipokuja walikuwa na matumaini kuwa pengine Burundi wangetuma taarifa ama wawakilishi lakini toka walipoanza mkutano asubuhi kulikuwa hakuna taarifa yeyote hivyo wakuu wa nchi walipokutana wakaona haitawezekana kuendelea na mkutano huo

"Na hata kama wangekuwa wanazungumza mazungumzo yao yasimgelikuwa na mashiko kisheria na maamuzi ya kisheria kwahiyo wakaamua huu mkutano uhairishwe ndiyo maana huo mkutano ukaahirishwa" alisema Mahiga

Hata hivyo Mahiga amesema itawalazimu kufanya mkutano mkuu wa Wakuu wa nchi zote sita na ni lazima iwe ndani ya mwaka huu, na ndani ya mwezi disemba 2018 kikatiba.Jumuiya ya Afrika Mashariki inaundwa na nchi sita ikiwemo Tanzani, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Sudani Kusini

Mkutano huo wa 20 wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliokuwa umebeba kauli mbiu isemayo kuhuisha utengamano wa kijamii, kisiasa na kiuchumi wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.

No comments: