Monday, November 30, 2015

AZANIA BANK TAWI LA MOSHI YAKABIDHI VIFAA YA KUFANYIA USAFI KWA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOSHI

Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi, Hajira Mmambe akisalimiana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,Jeshi Lupembe alipofika ofisini kwake kuitikia wito wa rais John Magufuli ya kufanya usafi Desemba 9 kwa kuchangia vifaa vya kufanyia usafi. 
Afisa afya mkuu wa manispaa ya Moshi,Mgeta Sebastian akisalimiana na Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi ,Hajira Mmambe alipotembelea ofisi za halmashauri hiyo kutoa msaada wa vifaa vya kufanyia usafi. 
Meneja wa Azania Bank ,Hajira Mmambe akitia saini katika kitabu cha wageni ofisini kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi.Jeshi Lupembe (kulia). 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,Jeshi Lupembe akipokea rasmi msaada kutoka benki ya Azania uliowasilishwa na Meneja wa benki hiyo ,Hajira mmambe kwa ajili ya kufanyia usafi. 
Wafanyakazi wa Azania Bank tawi la Moshi,wakishusha mifagio ,iliyotolewa na benki hiyo kwa ajili ya shughuli za usafi zitakazofanyika Desemba tisa mwaka huu,kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya manispaa ya Moshi ,Jeshi Lupembe. 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,Jeshi Lupembe akiwa ameongozana na Afisa afya mkuu wa manispaa hiyo,Mgeta Sebastian wakati wa kupokea msaada a vifaa vya kufanyia usafi kutoka Benki ya Azania tawi la Moshi. 
Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi ,Hajira Mmambe akikabidhi vifaa vya kufanya usafi kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ,Jeshi Lupembe ,vifaa hivyo vimetolewa kwa ajili ya kutekeleza agizo la rais Magufuli la kufanyika wa usafi siku ya Desemba 9.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.


RC KILIMANJARO AKUTANA NA WATENDAJI WA SERIKALI KATIKA KIKAO CHA UTENDAJI KAZI

Mkuu wa mkoa wa Kilimajaro,Amosi Makala akizunumza na wakuu wa wilaya ,wakurugenzi,Wakuu wa taasisi mbalimbali za umma katika kikao cha utendaji kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa. 
Wakuu wa wilaya za mkoa wa Kilimanjaro wakiwa katika kikao hicho,kutoka kuslia ni Mkuu wa wilaya ya Hai,Anthony Mtaka, Helman Kapufi (Mkuu wa wilaya ya Same) Novautus Makunga (Mkuu wa wilaya ya Moshi) na Lembris Kipuyo (Mkuu wa wilaya ya Rombo). 
Baadhi ya wakurugenzi wakiwa katika kikao hicho. 
Watendaji wengine wa serikali wakifuatilia hotuba ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro alipokutana nao . 
Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro,Severine Kahitwa akizungumza katika kikao hicho. 
Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Kilimanjaro. 
Baadhi ya watendaji wa taasisi za umma,kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi,Joyce Msiru. 
Badhi ya watumishi katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii kanda ya kaskazini.

KATIKA kutekeleza kauli mbiu ya Rais wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,John Magufuli ya “Hapa Kazi tu” Serikali mkoani Kilimanjaro imetangaza kusitisha likizo na ruhusa zote kwa watumishi wake katika kipindi cha siku kuu za Krismasi na mwaka mpya.

Agizo hilo linakuja wakati tayari baadhi ya watumishi wa Serikali kuanza taratibu za kuomba likizo na ruhusa kwa ajili ya kwenda kushiriki siku kuu za mwisho wa mwaka za Krismasi na mwaka mpya.

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Amos Makala alitangaza uamuzi huo jana wakati wa kikao cha kazi alichoitisha na wakuu wa wilaya zote za mkoa, wakurugenzi, kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na watendaji wengine wa serikali.

“Mh Rais ametoka kwenye kampeni hajapumzika,Makamau wa rais ametoka kwenye kampeni hajapumzika ,Waziri mkuu pia vivyo hivyo sasa sisi ni nani twende kwenye mapumziko ya siku kuu ya Krismasi.”alihoji Makala.

“Kwa maana hiyo ili haya tunayotaka ya elimu bure ,kukabiliana na Kipindupindu ,kwa madaraka niliyopewa kama mkuu wa mkoa nasitisha likizo zote,kwa Wakuu wa wilaya ,Wakurugenzi na wakuu wote wa idara ili mambo haya yaweze kutekelezwa,tumesema Hapa ni kazi tu”aliongeza Makala.

Alisema utekelezaji wa agizo la rais la kufanya usafi siku ya sikuu ya Uhuru inayofanyika Desemba 9 kila mwaka ,mapambano ya ugonjwa hatari wa Kipindupindu ambao umeendelea kusambaa sehemu kubwa ya nchi hayawezi kusubiri hadi watusmishi wa serikali watoke likizo.



TOVUTI YA NAFASI ZA AJIRA YAZINDULIWA JIJINI LEO

  Mkurugenzi Mtendaji wa tofuti ya ajira ya Owbaz, Barbara Butter (kushoto) akimpa maua balozi mpya wa Owbaz, Abernego Damian Nyamoga ‘Belle 9’ katika hafla ya uzinduzi rasmi wa tovuti hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wa pili kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Cosmos,  Muhammad Owais Pardesi na Mkurugenzi Rasilimali Watu wa kampuni ya bima ya Aris, Paritosh Bajaria.
 Mkurugenzi Mtendaji wa tofuti ya ajira ya Owbaz, Barbara Butter (kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa tovuti hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto kwake ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Cosmos,  Muhammad Owais Pardesi, balozi wa Owbaz, msanii wa muziki wa kizazi kipya Abernego Damian Nyamoga ‘Belle 9’  na Mkurugenzi Rasilimali Watu wa kampuni ya bima ya Aris, Paritosh Bajaria.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Cosmos, na mwanzilishi wa tovuti mpya ya Owbaz, Muhammad Owais Pardes (kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa tovuti hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Abernego Damian Nyamoga ‘Belle 9’ (wa tano kushoto) ambaye ni balozi wa tovuti ya Owbaz, akipozi kwa picha pamoja na baadhi ya wageni waalikwa katika hafla ya uzinduzi wa tovuti hiyo jijini Dar esSalaam mwa wiki.

 Baadhi ya wageni waalikwa wakipiga picha ya kumbukumbu na  msanii wa muziki wa kizazi kipya, Abernego Damian Nyamoga ‘Belle 9’katika hafla ya uzinduzi wa tovuti hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

BREAKING NEWWWWWWS!!!!! SHEKH ISSA PONDA AACHIWA HURU

MAHAKAMA ya hakimu mkazi Morogoro imemuachia huru leo Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda aliyekuwa akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi baada ya mahakama kutoridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka na hivyo kuonekana hana hatia.

********
Historia ya kesi ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda.

Hati ya Mashitaka ya Kesi hiyo ilikuwa na jumla ya Mashitaka matatu  lakini Julai 22 mwaka 2015, Hakimu Mkazi Mary Moyo  alitoa  uamuzi wa kumfutia shitaka la kwanza kwasababu lilishatolewa uamuzi na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, na hivyo mahakama hiyo ya Morogoro siku hiyo ilitoa uamuzi wa kumuona ana kesi ya kujibu  katika mashitaka mawili yaliyosalia ambalo ni kosa la pili na la tatu .


Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro  ilimfungia dhamana Sheikh Ponda baada ya kukubaliana na hati ya aliyekuwa  Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), wakati huo Dk.Eliezer Feleshi ambaye kwasasa ni Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam liloomba Mahakama hiyo imfungie dhamana mshitakiwa huyo chini ya Kifungu cha 148(4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya jinai ya Mwaka 2002.

Hatua hiyo ya kufunguliwa kesi katika Mkoa wa Morogoro ilikuja ikiwa ni muda mfupi baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, Agosti 19 Mwaka 2013 saa Tatu asubuhi,  kumfutia kesi ya jinai  Na.144/2013 katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano baada ya DPP kudai kuwa hana nia ya kuendelea kumshitaki katika kesi hiyo No.144/2013  kwa mujibu wa kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002.

Hata hivyo baada ya hakimu Liwa kumwachilia huru,Ponda ambaye aliletwa mahakamani hapo saa 12 asubuhi na wanausalama wa polisi na magereza chini ya ulinzi mkali, alikamatwa tena na kupakizwa kwenye magari ya wanausalama hao ambapo baadhi ya wanausalama hao waliliambia gazeti hili kuwa wanampeleka Ponda mkoani Morogoro kwaajili ya kufunguliwa makosa matatu ya uchochezi, kufanya mkusanyiko haramu na kisha akarejeshwa gereza la Segerea Dar es Salaam , lakini baadae Uongozi wa Jeshi la Magereza uliamua kumuamisha Ponda kutoka Gereza la Segerea na kumuamishia Katika Gereza Moja Mkoani Morogoro.

Sheikh Ponda alifikishwa mahakamani hapo akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi, baada ya kuwasili kwa helikopta ya Jeshi la Polisi katika uwanja wa gofu mjini Morogoro.

Akisoma mashitaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro, Richard Kabate, Mwanasheria Kiongozi  wa Serikali, Bernard Kongola, alidai  kuwa Agosti 10, mwaka 2013, katika eneo la Uwanja wa Ndege, Manispaa ya Morogoro, Ponda aliwaambia Waislamu wasikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za misikiti, kwa madai kuwa zimeundwa na BAKWATA, ambao ni vibaraka wa CCM na serikali.

Alidai kuwa Sheikh Ponda ambaye anatetewa  na wakili wa kujitegemea Juma Nassor aliwaagiza waumini hao kuwa endapo watu hao watajitokeza kwao na kujitabulisha kwamba ni kamati za ulinzi na usalama za misikiti, wafunge milango na madirisha wawapige.

Ilielezwa kuwa kauli hiyo ni kinyume cha agizo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliyotolewa na Hakimu Victoria Nongwa Mei 9, mwaka 2010, ambayo ilimtaka Ponda ndani ya mwaka mzima kuhubiri amani na Kuwa Raia Mwema.

Katika shitaka la pili, Kongola alidai kuwa Agosti 10, mwaka huu, katika eneo la Uwanja wa Ndege, Morogoro, Ponda aliwaambia Waislamu kuwa serikali ilipeleka jeshi Mtwara kushughulikia suala la vurugu iliyotokana na gesi ili kuwaua, kuwabaka na kuwatesa wananchi, kwa sababu asilimia 90 ya wakazi hao ni Waislamu.

Kwamba, Ponda aliwaambia wafuasi wake kuwa serikali haikufanya hivyo kwa wananchi wa Loliondo walipokataa Mwarabu asipatiwe kipande cha ardhi ya uwindaji baada ya kudai ni mali yao, kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wa huko ni Wakristu.

Shitaka la tatu ambalo linafafana na lile la pili, ambalo nalo linadaiwa kutendwa Agosti 10, mwaka huu, ambapo kauli ya Ponda inadaiwa kuumiza imani za watu wengine kinyume cha kifungu cha sheria namba 390 na kanuni ya adhabu namba 35 cha mwaka 2002.

Oktoba 18 mwaka 2012, Ponda na wenzie 49 walifikishwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa Mara ya kwanza   wakikabiliwa na makosa matano, kosa la kwanza ni la kula njama, kujimilikisha mali, kuingia kwa jinai katika kiwanja cha Chang'ombe  Markas,wizi wa malighafi zenye thamani ya Sh. Milioni 59 na kosa la uchochezi ambapo katika kesi hiyo Jamhuri ilikuwa ikiwakilishwa na wakili Mwandamizi wa Serikali , Tumaini Kweka .Mahakama pia iliwafunga dhamana ya Ponda na mshitakiwa wa pili tangu 0ktoba 18 Mwaka 2012 hadi siku Kesi hiyo iliyotolewa hukumu Mei 9 Mwaka 2013.

Mei 9 mwaka 2013 Hakimu Mkazi Victoria  Nongwa akitoa hukumu yake katika kesi hiyo ya Ponda na wenzake alisema anawaachiria huru washitakiwa 49  kwasababu upande wa jamhuri  umeshindwa kuthibitisha kesi dhidi yao na kwamba anamtia hatiani Ponda kwa kosa moja tu  la kuingia kwa jinai na kwamba na anamuachiria huru katika makosa manne yaliyosalia kwasababu pia jamhuri ilishindwa kuthibitisha mashitaka hayo dhidi ya Ponda.

Sheikh Ponda alikataa rufaa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kupinga hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mei 9 mwaka 2013 ambapo alishinda rufaa yake.

Hata hivyo siku Chache baada ya Kufungwa Kifungo hicho cha nje Mei 9 mwaka 2013, Ponda alikwenda Mkoani Morogoro na kufanya mkutano ambao alidai wa Kutenda makosa ya jinai ambao alikamtwa  Agosti Mwaka 2013 na kuwekwa chini ya ulinzi na kufunguliwa Kesi Mahakama ya Kisutu Na.144/2013 ikafutwa na DPP na ndipo akafunguliwa kesi hiyo Mkoani Morogoro ambayo imetolewa hukumu Leo na kuachiwa huru.

MAHAFALI YA13 YA CHUO KIKUU CHA KUMBUKUMBU YA HUBRT KAIRUKI YAFANYIKA LEO JIJINI DAR.

 Makamu Mkuu wa Chuo cha kumbukumbu ya Hubet Kairuki Profesa, Kito Mshigeni akizugumza na wanafunzi  juu ya kutumia elimu waliyoipata  kuwasaidia, kuwainua, na kuwaletea  matumaini  mapya wote wenye uhitaji katika jamii, kwa kadri ya uwezo wao, ameyazungunza hayo katika mahafali ya 13 ya chuo kuu cha kumbukumbu ya Hubert Kairuki Jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Chuo  Kikuu, Balozi Dk. Salim Ahmed Salim wa kwanza (kushoto) akiwa na uongozi wa chuo kikuu cha kumbukumbu ya Hubert Kairuki kabla ya kuanza kutunukia elimu zao wanazo hitimu  wahitimu wa elimu ya juu,  katika mahafali ya 13 ya chuo kikuu cha kumbukumbu ya Hubert Kairuki leo Jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Chuo  Kikuu, Balozi Dk. Salim Ahmed Salim akimkabidhi cheti cha shahada ya kwanza ya Uuguzi  mhitimu, Nyawawa Wawa  leo katika mahafali ya 13 ya chuo kikuu cha kumbukumbu ya Hubert Kairuk Jijini Dar es Salaam.
Brass Band ikiendelea kutumbuiza katika mahafali ya 13 ya chuo kikuu cha kumbukumbu cha Hubert Kairuki leo Jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya wahitimu wa Kozi ya cheti cha Uuguzi wakila kiapo, leo Jijini Dar es Salaam.
Sehemu  ya  wahitimu na wazazi waliohudhuria katika mahafali ya 13 ya chuo kikuu cha kumbukumbu ya Hubert Kairuki leo Jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu  ya jamii).

Wafanyakazi Benki ya NMB washerehekea 'Family Day'

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker (kushoto) akimkabidhi kikombe mmoja wa washindi katika mchezo wa kuogelea kwenye maadhimisho ya Siku ya Familia iliyofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana.Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker (kushoto) akimkabidhi kikombe mmoja wa washindi katika mchezo wa kuogelea kwenye maadhimisho ya Siku ya Familia iliyofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana.Baadhi ya washindi wa mchezo wa kuogelea wakipata picha ya kumbukumbu na viongozi waandamizi wa NMB baada ya kukabidhiwa zawadi zao kwenye maadhimisho ya Siku ya Familia yaliyofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker (kulia) akizungumza na wafanyakazi wa NMB pamoja na familia zao kabla ya kuzinduwa rasmi maadhimisho ya Siku ya Familia (family day) kwa wafanyakazi wa benki hiyo yaliofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana. Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni Tusherehekee pamoja mafanikio ya Miaka 10 ya NMB.Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker (kushoto) akizungumza na wafanyakazi wa NMB pamoja na familia zao kabla ya kuzinduwa rasmi maadhimisho ya Siku ya Familia (family day) kwa wafanyakazi wa benki hiyo yaliofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana. Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni Tusherehekee pamoja mafanikio ya Miaka 10 ya NMB.Baadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakiingia katika maadhimisho ya Siku ya Familia (Family Day) iliofanyika jana Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park Jijini Dar es Salaam.Baadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakitambuliwa kabla ya kuingia katika maadhimisho ya Siku ya Familia iliyofanyika jana Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park Jijini Dar es Salaam.Baadhi ya viongozi wa Benki ya NMB, na wanafamilia zao wakipata maelekezo kabla ya kuingia kwenye ukumbi wa maadhimisho ya Siku ya Familia (family day) kwa wafanyakazi wa benki hiyo yaliofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana. Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni Tusherehekee pamoja mafanikio ya Miaka 10 ya NMBBaadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakipewa utaratibu kabla ya kuingia kwenye maadhimisho ya Siku ya Familia yenye kauli mbiu ya tusherehekee Miaka 10 ya mafanikio ya benki ya NMB yaliofanyika jana Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park Jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakiwa katika michezo mbalimbali na familia zao kwenye maadhimisho ya Siku ya Familia (Family Day) na iliyofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana.Baadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakiwa katika michezo mbalimbali na familia zao kwenye maadhimisho ya Siku ya Familia (Family Day) iliyofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana.Baadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakipata huduma mbalimbali ndani ya Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park katika maadhimisho ya Siku ya Familia iliyofanyika jana Jijini Dar es SalaamMalaika Bandi wakiwaburudisha wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB katika maadhimisho ya Siku ya Familia iliyofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana.Baadhi ya huduma za kibenki za Benki hiyo pia zilipatikana.Baadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakifuatilia burudani anuai katika maadhimisho ya Siku ya Familia iliyofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana.Baadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakipata huduma mbalimbali ndani ya Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park katika maadhimisho ya Siku ya Familia na kusherehekea Miaka 10 ya benki hiyo iliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam.Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker (katikati) akizunguka kubadilishana mawazo na baadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki hiyo kwenye maadhimisho ya Siku ya Familia na kusherehekea Miaka 10 ya benki hiyo iliyofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam janaBaadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakiwasili eneo la Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park katika maadhimisho ya Siku ya Familia iliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam.Mmoja wa viongozi wa NMB (kulia) akizungumza na wanafamilia na wafanyakazi wa Benki hiyo kabla ya uzinduzi wa maadhimisho ya Siku ya Familia iliyofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker.Baadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakiwa katika michezo mbalimbali na familia zao kwenye maadhimisho ya Siku ya Familia (Family Day) iliyofanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana.Baadhi ya wanafamilia na wafanyakazi wa Benki ya NMB wakiwa katika michezo mbalimbali na familia zao kwenye maadhimisho ya Siku ya Familia (Family Day) hafla hiyo ilifanyika Kunduchi Wet 'n' Wild Water Park ya Jijini Dar es Salaam jana.