Friday, January 31, 2014

MH. MIGIRO AITEMBELEA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA

 Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanazania,Mh. Jaji Aloysius Mujulizi (kushoto) akimpokea Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Dkt. Asha Rose Migiro wakati alipokuwa akiwasili kwenye ofisi za Tume hiyo na kukutana na Watumishi wa Tume,jijini Dar es Salaam.Anaefuata nyuma ya Mh. Migiro ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Angela Kairubi.
 Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Asha Rose Migiro (kushoto) akipokea maua kutoka kwa Afisa Tawala wa Tume Bi. Suzan Magoti.
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Asha Rose Migiro akipokea Ripoti zilizofanyiwa kazi na Tume kutoka kwa Katibu Mtendaji wa Tume Bi. Winfrida Korosso 
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Asha Rose Migiro akizungumza wakati wa kikao chake na uongozi wa Tume  
 Mwenyekiti wa Tume akizungumza wakati Waziri wa Katiba na Sheria  Mhe Asha Rose alipoitembelea Tume
 Baadhi ya Watumishi wa Tume wakiwa katika kikao na Mhe Waziri wa Katiba na Sheria.Picha Zote na Munir Shemweta, Ofisa Habari wa Tume.

Thursday, January 30, 2014

MKUTANO WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA AU WAFUNGULIWA LEO ADDIS ABABA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye Mkutano wa  Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) ambao  umefunguliwa  rasmi  leo tarehe 30 Januari, 2014 mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Mwenyekiti wa Kamisheni  ya Umoja wa Afrika (AU), Mhe. Dkt. Nkosazana Dlamini-Zuma akisoma hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja huo mjini Addis Ababa, tarehe 30 Januari, 2014. Katika hotuba yake Dkt. Dlamini-Zuma alisisitiza umuhimu wa matumizi ya Lugha ya Kiswahili kwani ni moja ya lugha kubwa Barani Afrika.
Jopo la Marais Wastaafu wakiwa kwenye mkutano huo. Kutoka kushoto ni Mhe. Olusegun Obasanjo, Rais Mstaafu wa Nigeria, Mhe. Thabo Mbeki, Rais  Mstaafu wa Afrika Kusini na Mhe. Festus Mogae, Rais Mstaafu wa Botswana.
Rais Mpya wa Madagascar, Mhe. Henry Rajaonarimampianina akitoa hotuba yake ya shukrani kwa nchi za Afrika kwa michango yao iliyopelekea uchaguzi wa amani na demokrasia nchini Madagascar na pia kwa  Madagascar kurejea AU.
Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. hailemariam Dessalegn akitoa hotuba kama Mwenyekiti wa AU  anayemaliza muda wake kabla ya kukabidhi nafasi hiyo kwa Rais wa Mauritania, Mhe. Mohamed Ould Abdel Aziz.
Rais wa Mauritania, Mhe. Mohamed Ould Abdel Aziz  akitoa hotuba kama Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa Afrika kwa kipindi cha mwaka mmoja hadi Januari 2015.
Picha ya Pamoja ya Viongozi wa AU.
Mhe. Membe akiongozana na Rais wa Zimbabwe, Mhe. Robert Mugabe mara baada ya hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa AU
Mhe. Membe akiteta jambo na Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Jacob Zuma nje ya Ukumbi wa Mikutano wa AU.

Kiswahili chazidi kupaa Umoja wa Afrika

Na Mwandishi wetu, Addis Ababa

Umoja wa Afrika umeitaja Lugha ya Kiswahili kuwa ndiyo lugha kubwa na rasmi Afrika na ndio Lugha inayofundishwa zaidi katika Vyuo Vikuu mbalimbali duniani kutoka Afrika.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU), Dkt. Nkosazana Dlamini-Zuma wakati akifungua Mkutano wa 22 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia leo tarehe 30 Januari, 2013.

Dkt. Zuma katika hotuba yake ya kusisimua ambayo ilielezea maendeleo yaliyofikiwa Afrika katika kipindi cha miaka 50 iliyopita, changamoto mbalimbali zinazolikabili Bara hili na matarajio alisema kwamba katika kipindi hiki ni muhimu kuitumia Lugha ya Kiswahili kuiunganisha Afrika.

“Wajukuu zetu waliona ni kichekesho tulivyokuwa tukihangaika na  tafsiri za Lugha za Kiingereza, Kifaransa na Kireno wakati wa mikutano ya AU, na vile tulivyokuwa tukizozana kwamba chapisho la Kiingereza halifanani na lile la Kifaransa au Kiarabu, sasa tunayo Lugha yetu pamoja na hizo lugha nyingine huo ndio ustaarabu wa sasa” alisema Dkt. Dlamini-Zuma.

Akizungumzia maendeleo yaliyofikiwa Afrika katika kipindi cha miaka 50 iliyopita, Mhe. Dkt. Dlamini-Zuma alisema  kuwa Afrika sasa imepiga hatua kubwa katika maendeleo ambapo kwa sasa Afrika ndio msafirishaji mkubwa wa chakula nje na pia imekuwa kituo cha viwanda na kituo cha maarifa na hivyo kuleta manufaa kwa maliasili zilizopo ikiwemo mazao ya kilimo kama kichocheo cha mapinduzi ya viwanda.

“Rafiki zangu, kwa hakika Afrika imepiga hatua kubwa katika maendeleo, kutoka usafirishaji wa malighafi katika kipindi kilichopita na kuwa msafirishaji mkuu wa chakula nje, hii itasaidia maliasili iliyopo Afrika kubaki na kuwa kichocheo cha mapinduzi ya viwanda” alisema Dkt. Dlamini-Zuma. Aidha aliongeza kuwa, Kampuni nyingi za Afrika kuanzia zile za madini, fedha, chakula, vinywaji, utalii, madawa, uvuvi na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ni miongoni mwa zinazoongoza duniani katika sekta hizo.

Dkt. Dlamini-Zuma alieleza kuwa Afrika sasa ni ya tatu duniani kiuchumi. Hata hivyo alisisitiza bado kuna umuhimu kwa nchi za Afrika kuchangia katika maendeleo. Vile vile, alisema kwamba njia pekee ya kuleta amani ni kuwekeza kwa watu hususan kuwawezesha vijana na wanawake. ‘Afrika inahitaji mapinduzi katika ujuzi kwa kubadilisha mfumo wa elimu ili kuwaandaa vijana ambao ni wabunifu na wenye mawazo ya ujasiriamali ili kuleta maendeleo katika Bara lao’ alisema Dkt. Zuma.

Kuhusu hali ya amani na usalama huko, Sudan Kusini na Jamhuri ya Afrika ya Kati, Dkt. Dlamini-Zuma alielezea kusikitishwa kwake na hali katika nchi hizo na kusisitiza umuhimu wa nchi za Afrika kufanya kazi kwa pamoja ili kuleta amani ya kudumu katika nchi hizi. 

"Tunavyouanza mwaka 2014 mioyo yetu ipo na watu wa Sudan Kusini na  wale wa Jamhuri ya Afrika Kati hususan wanawake na watoto hivyo ni muhimu tufanye kazi kwa pamoja ili nchi hizi zipate amani ya kudumu na kutimiza lengo letu la kuzima kabisa mitutu ya bunduki katika Bara letu" alisisitiza Dkt. Dlamini-Zuma.

Aidha, alimtangaza Bibi Binta Diop kuwa Mjumbe Maalum wa Amani na Usalama Afrika ambaye atakuwa na jukumu la kuhakikisha sauti za wanawake zinasikika katika masuala ya kujenga amani na utatuzi wa migogoro.

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika pia ulishuhudia ubadilishanaji wa Uenyekiti wa Umoja wa Afrika kutoka kwa Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Hailemariam Dessalegn kwenda  kwa   Rais wa Mauritania, Mhe. Mohamed Ould Abdel Aziz. Aidha, Mkutano huo ulimkaribisha  Rais mpya wa Madagascar, Mhe. Hery Rajaonarimampianina baada ya miaka minne ya kufutwa uanachama wa AU.

Akitoa hotuba yake kabla ya kukabidhi uenyekiti, Mhe. Dessalegn alizishukuru nchi zote za Afrika kwa ushirikiano na kusisitiza umuhimu wa kuweka vipaumbele vya maendeleo Barani Afrika katika Agenda ya Maendeleo ya Kimataifa baada ya mwaka 2015 na ile ya Malengo ya Maendeleo Endelevu.

Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa AU uliongozwa na Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambaye alimwakilisha Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

TAMKO ALILOLITOA MZEE JOHN MALECELA LEO

Ndugu zangu waandishi wa habari, awali ya yote naomba niwasalimie na niwapongeze kwa kufika -mwaka mpya 2014, pia naomba niwapongeze kwa kazi kubwa ambayo mmekuwa mkiifanya hasa kuhakikisha watanzania wanapata habari kwa kila jambo linaloendelea kila kona ya taifa letu la Tanzania.

Ndugu waandishi wa habari nimewaita hapa ili kuzungumza nanyi na mnisaidie kufikisha ujumbe kwa watanzania hasa kuhusu jambo hili ambalo limekuwa gumzo kwa watanzania wengi la mbio za urais 2015 kwa baadhi ya watu ndani ya chama changu cha mapinduzi (CCM), kilichonisukuma zaidi na kupata hamu ya kuongea nanyi ni baada ya kumsikia -na kumuona kijana wetu ndani ya chama cha mapinduzi bwana Paul Makonda akiwa na ujasiri wa kukemea vitendo mambo haya yanayofanywa na baadhio ya viongozi bila uwoga wowote naomba tuchukue fursa hii kumpongeza sana kijana huyu.

Nadiriki kusema nampongeza kijana huyu hasa kwa kauli zake nzito na za kijasiri kwa maslahi ya chama changu cha CCM ili chama kiendelee kupendwa na kuchaguliwa na watanzania.

Pia itakuwa si busara kama sitawapongeza vijana wangu katibu mkuu wa chama ndugu ABDULRAHMAN KINANA na NAPE NNAUYE kwa juhudi zao za dhati za kujenga chama na kuendelea kuwaeleza wananchi juu ya misingi bora ya chama cha mapinduzi (CCM) kwa kuwakemea viongozi wasiofaa bila kujali cheo na umaarufu wao ndani ya chama na serikali, nawaomba waendelee -na juhudi zao hizo nami naziunga mkono juhudi zao na kama kuna watru wanaowabeza naomba wasijali kwani kukemea viongozi wasiofaa ndani ya chama na serikali ni msingi wa chama chochote kilichounda serikali.

Aidha nawaomba watanzania wenzangu wazalendo wasikubali kukatishwa tama na kikundi cha watu wachache wasio na mapenzi mema na taifa letu ambalo limekuwa mfano wa kuigwa kwa amani, upendo, utulivu na mshikamano urithi tulioachiwa na baba yetu wa taifa mwalimu julias kambarage nyerere ndani na nje ya mipaka ya bara letu la afrika.

Ndugu zangu waandishi wa habari naomba niwaambie kuwa msemaji wa UVCCM kijana wetu Paul Makonda namuunga mkono kwa -kitendo chake cha ujasiri cha kumkemea ndugu EDWARD NGOYAI LOWASSA bila uwoga kwa jinsi anavyokivuruga chama chetu kwa lengo la kutaka urais 2015 huku secretariet ya chama ikiwa imekaa kimya wakati inajua kuwa muda wa kuanza mbio hizi bado na kufanya hivi kwa sasa ni kukiuka misingi na katiba -ya chama. Hapa najiuliza kuwa ile misingi imara ya uongozi ndani ya chama chetu cha mapinduzi iko wapi? Mpaka tumuachie mototo ndio akemee haya? Je, hapa chama kiko wapi?

Ukweli ni kwamba wanachama wetu na vijana wamekuwa njia panda huku wakitamani kusikia tamko au karipio la chama juu ya suala hili la harakati za urais 2015 bila mafanikio.

Naomba niseme kuwa bila kuwa na karipio au tamko la chama, hawa wanaotumia pesa zao hadharani kwa lengo la kutafuta umaarufu na ushawishi kwa vijana ili kupata madaraka wanaharibu misingi yetu bora ya uongozi iliyowekwa na waasisi wetu ndani ya chama.

Kinachonisikitisha zaidi ni kuona juhudu za uongozi wa sasa wa chama ngazi ya juu ikiwa ni pamoja na sekretarieti inayoongozwa na katibu mkuu ABDULRAHMANI KINANA na katibu mwenezi NAPE NNAUYE za kutetea chama hiki zinatiwa mchanga.

Ninaomba juhudi hizi zisibezwe na watu wenye nia njema na chama. Ukweli ni kwamba vijana hawa wamekuwa na juhudi kubwa sana ya kujenga na kuimarisha chama chetu -kwa wananchi kila pembe ya taifa letu kwa kukemea na kueleza misingi ya uongozi bora. Swali: Je! Chama hakioni haya mpaka vijana ndio waone?

Kwa hili ni lazima tubadilike ili kujenga chama chetu na naishauri -secretariet ya chama lazima ichukue hatua mara moja, kijana huyu paul makonda asingesema haya yote kama hana uhakika wa ushahidi wa wa haya aliyoyasema na nampongeza sana.

Vijana na wanachama wengi wa CCM wamekuwa na hamu kwa muda mrefu ya kutaka kujua msimamo wa chama chao bila mafanikio na ndio sababu ya baadhi ya-wengine kupoteza mwelekeo.

Sisi tulikijenga chama hiki kwa taabu sana hapakuwa hata mtu mmoja aliyediriki kutumia fedha zake kutaka madaraka. 

Nidhamu, busara na uchungu wa rasilimali za taifa hili kwa maslahi ya wananchi ndio vilituongoza kufuata misingi na maadili ya uongozi ndani ya chama na serikali, ndio maana tunaumia sana kuona chama sasa kinataka kutekwa na wenye fedha kwa uchu wa madaraka, mpaka tunashangaa na kujiuliza hizi pesa wanatoa wapi? Na haya madaraka wanayotaka kwa kununua ni kwa maslahi ya nani? Huku watanzania wakiendelea kuwa maskini.

Mfano hivi karibuni baadhi ya viongozi wa chama ngazi ya juu wamejibishana kwenye vyombo vya habari,vitendo hivi havina tija kwa chama na wala havileti umoja na mshikamano ambao umedumu ndani chama kwa muda mrefu.

Mwisho Ninaomba sekretarieti ichukue hatua haraka kama alivyoomba kijana wetu makonda na kweli kuchelewa kuchukua hatua jambo hili kumejionyesha wazi kwamba utaleta kutokuelewana ndani ya chama kusiko kuwa na lazima.

JOHN SAMWELI MALECELA
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

UNIC yaendelea kutoa mafunzo ya mateso ya kambi za wayahudi

DSC_0014
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi ya Diamond juu ya umuhimu wa kujifunza mauaji ya kimbari ya wayahudi ya mwaka 1933.

Na Mwandishi Wetu

Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) kimeendelea kutoa mafunzo na elimu juu ya umuhimu wa kukumbuka maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya ukombozi wa kambi za mateso ya Auschwitz kwa wanafunzi wa sekondari na shule za msingi nchini.

Akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi ya Diamond ya jijini Dar es Salaam leo asubuhi, Afisa habari wa kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama amesema kwamba ni muhimu kwa kizazi na kizazi kujifunza madhara ya mauaji na maangamizi ya moto dhidi ya wayahudi yaliofanywa na askari wa kinazi wa Ujerumani.

“Ni muhimu kutoa mafunzo kwa vijana wakitanzania wa shule za msingi na sekondari ili wajue kwamba tofauti za rangi na za kidini hazina nafasi ya kutugawa kama binadamu,” amesema Nkhoma.
DSC_0005
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Diamond na Mlezi wao wakimsikiliza Bi. Ledama (hayupo pichani).
DSC_0044
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama, akisoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataiafa katika siku ya kimataifa ya maadhimisho ya kuwakumbuka wahanga wa mauaji ya maangamizi ya moto.

Alisisitiza kwamba mauaji na mateso ya Auschwitz yalipoteza mamilioni ya watu wasio na hatia na mafunzo haya yanaonyesha chuki na ubaguzi dhidi ya wayahudi na chuki za aina nyingine yoyote hazina nafasi katika ulimwengu wa leo.

Nkhoma amesema kwamba binadamu wote ni sawa na tofauti za kipato au dini au rangi haziwezi tena kujenga chuki dhidi ya binadamu wengine kwa sababu wote kama binadamu tuna haki sawa mbele za mungu.
DSC_0051
Wanafunzi wa shule ya msingi ya Diamond jijini Dar es Salaam, wakifuatilia sinema maalum ya mauaji ya kambi za mateso ya wayahudi mwaka 1933.

Wakati huo huo, ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika siku ya kimataifa ya maadhimisho ya kuwakumbuka wahanga wa mauaji ya maangamizi ya moto amesema aliona makambi ambako wayahudi, waroma, wasinti, mashoga, wafungwa wa kivita na watu wenye ulemavu walitumia siku za mwisho katika hali ya kinyama.

“Umoja wa Mataifa ulianzishwa kuzuia kila aina hii ya fazaa kutokea tena, lakini bado misiba kuanzia Cambodia hadi Rwanda mpaka Srebrenica inaonyesha kuwa sumu ya mauaji ya kimbari bado inatiririka,” ilisema taarifa hiyo.
DSC_0082
Pichani juu na chini ni Wanafunzi wa shule ya msingi ya Diamond wakisoma baadhi ya machapisho ya Umoja wa Mataifa.
DSC_0077
DSC_0075

Wachimbaji wadogo watakiwa kuzingatia kanuni za usalama migodini

Mtaalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Mhandisi Dkt. Crispin Kinabo akiwasilisha mada juu ya utunzaji wa mazingira kwenye migodi wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika mapema leo katika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma. Mafunzo hayo yalishirikisha viongozi na watendaji wa wilaya, madiwani, wakuu wa vitongoji na wachimbaji wadogo lengo lake likiwa ni kuwapa uelewa wa kanuni za uchimbaji bora wa madini.
Mmoja wa wakilishi wa wachimbaji wadogo ambaye ni mmiliki wa mgodi katika eneo la Mhesi Mapinduzi lililopo wilayani Tunduru Bi Sofia Hamdan akichangia mada wakati wa mafunzo hayo.
Mpepo Ismail ambaye ni mmoja wa wachimbaji wadogo na mmiliki wa machimbo ya shaba Mbesa akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho. Ameitaka Serikali kuangalia uwezekano wa kuwasaidia wachimbaji wadogo kwa kuwakopesha vifaa vya kuchimba madini.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zinawasilishwa na watoa mada kwa nyakati tofauti (hawapo pichani).


Na Greyson Mwase, Tunduru

Wachimbaji wadogo wametakiwa kuzingatia kanuni za usalama migodini ili kuepuka majanga yanayoweza kujitokeza na kuleta athari kwa jamii kwa ujumla.

Hayo yalisemwa na Afisa Madini Mkazi Tunduru Mhandisi Frederick L. Mwanjisi alipokuwa akiwasilisha mada kwenye mafunzo yaliyoshirikisha wachimbaji wadogo, viongozi na watendaji wa wilaya, madiwani na wenyeviti wa vitongoji yanayoendelea wilayani Tunduru mkoani Ruvuma.

Mhandisi Mwanjisi alisema kuwa wachimbaji wengi wamekuwa wakithamini madini kwanza badala ya mazingira kwa jamii inayowazunguka jambo linalosababisha kujitokeza kwa majanga ya mara kwa mara kama vile kuanguka kwa vifusi na kemikali kuathiri binadamu ikiwa ni pamoja na wanyama.

“ Wachimbaji wamekuwa wakitanguliza msemo usemao “madini kwanza” kwa kufikiria maslahi yao binafsi badala ya kufikiria jamii inayowazunguka kwa kuweka mazingira katika hali ya usalama yaani msemo uwe “Usalama kwanza” Alisisitiza Mhandisi Mwanjisi.

Mhandisi Mwanjisi alibainisha athari zinazosababishwa na majanga yanayotokana na kutokuzingatia usalama migodini ni pamoja na mmiliki kupoteza fedha nyingi kwa ajili ya fidia, miundombinu kuharibika, kupoteza imani kwa wafanyakazi na umma kwa ujumla hali inayoweza kupelekea hata mgodi kufungiwa.

Aliendelea kutaja athari nyingine kwa upande wa wafanyakazi kuwa ni pamoja na kupoteza nguvu kazi, ulemavu wa maisha, kuathirika kisaikolojia ikiwa ni pamoja na kukosa furaha ya maisha.

Mhandisi Mwanjisi aliongeza kuwa jukumu la usalama kwenye migodi ni la wote kuanzia wamiliki wa migodi, wafanyakazi, serikali ikiwa ni pamoja na jamii inayozunguka migodi.

Mhandisi Mwanjisi aliainisha kanuni za usalama migodini ikiwa ni pamoja na uvaaji wa vifaa vya kujikinga na mazingira hatarishi, kuweka mgawanyo wa kazi kulingana na taaluma na uzoefu wa wafanyakazi migodini, kufukia mashimo ikiwa ni pamoja na kuwekea wigo maeneo hatarishi ndani ya migodi.

Aliongeza kanuni nyingine za usalama ni pamoja na kufanya ukaguzi wa maeneo ya machimbo kabla ya kuanza kazi ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwa mkaguzi wa migodi juu ya matukio ya hatari au ajali zinazotokea migodini.

Kanuni nyingine ni pamoja na kuwa na orodha ya wafanyakazi wote wa mgodi katika daftari maalumu, vifaa vya huduma ya kwanza na kutoshirikisha watoto wenye umri wa chini ya miaka 18 katika kazi za machimbo.

Aidha Mhandisi Mwanjisi aliwataka wachimbaji wadogo kuwa na mpango wa usalama kwenye migodi wenye kuainisha tahadhari zinazoweza kuchukuliwa pindi majanga yanapotokea katika migodi badala ya kutokuwa na mpango wowote hali inayopelekea ugumu katika kushughulikia kwa haraka majanga yanapojitokeza.

Wakati huo huo mtaalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Jiolojia Mhandisi Dkt. Crispin Kinabo aliongeza kuwa wachimbaji wadogo mbali na kuzingatia kanuni za usalama migodini wanatakiwa kufanya tafiti za kijiolojia kabla ya kuanza uchimbaji wa madini ikiwa ni pamoja na kusoma ramani za kijiolojia.

Dkt. Kinabo aliwataka wachimbaji wadogo kuachana na uchimbaji wa mashimo kiholela bila kusoma ramani za kijiolojia za maeneo husika hivyo kupelekea kuwa na mashimo kila mahali na hivyo kupelekea majanga ya kujitakia.

Aidha Dkt. Kinabo aliwataka wachimbaji kuzingatia kanuni za mazingira kwa kutunza vyanzo vya maji ikiwa ni pamoja na mpango wa kuotesha miti.

Mafunzo haya yaliandaliwa na Wizara ya Nishati na Madini lengo lake likiwa ni kuwapa uelewa wa kanuni za uchimbaji bora wa madini wachimbaji wadogo ikiwa ni pamoja na viongozi na watendaji wa wilaya, madiwani, wakuu wa vitongoji na wachimbaji wadogo.

SASENI MEDIA WAIBUKA NA CHANGAMOTO KWA WAIGIZAJI WA FILAMU TANZANIA

Mkurugenzi wa Kampuni ya Saseni Media, Bw. Issa Mbura akizungumza katika warsha hiyo kwa wasanii mbali mbali wa filamu hapa nchini.

Kampuni ya Saseni Media, kwa kupitia mpango wake wa kukuza vipaji vipya vya uigizaji na kuvisimamia, iliendesha kwa mafanikio makubwa zoezi la usaili kwa waigizaji wazoefu na wanaochipukia siku ya jumamosi, tar 25 Januari 2014.

Idadi kubwa ya watu ilijitokeza kujisajili na kufanyiwa usaili na kila mwigizaji alionekana kuwa ni mwenye shauku ya kutaka kupata fursa hiyo na hivyo kuonyesha umahiri wake katika uigizaji. Akizungumzia usaili huo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Saseni Media, Bw. Issa Mbura amesema

“Zoezi lilienda vizuri na pamoja na kupata vipaji kama lilivyokuwa kusudio letu, pia tumeshuhudia mambo kadhaa yakijitokeza kama changamoto kwa tasnia ya filamu inayotegemea sana waigizaji ili kufanya vizuri,” “Moja, ni kwamba Tanzania kuna waigizaji wengi wanaochipukia na kutafuta fursa za kuigiza kuliko wale wachache tuliozoea kuwaona kwenye luninga zetu,”anasema Mwl. Issa.

Wanachohitaji ni jukwaa la kuwawezesha kuonyesha vipaji vyao lakini mfumo na biashara ya filamu haujatoa fursa hizo hasa pale unapotumia zaidi waigizaji wanaofahamika (Stars). Hii inapelekea wao kutafuta kila namna ya kufanikiwa na kujikuta wanagharamika bila mafanikio. Mfano mmoja ya vijana tuliowafanyia usaili amesema ametumia takribani zaidi ya elfu hamsini kama ada ya kujiunga na vikundi vya sanaa bila mafanikio ya kuigiza kwenye TV au filamu mpaka sasa.

Mbili, idadi ya watu waliojitokeza kwenye usaili wametoka kwenye vikundi vya sanaa wakiwa wamejiunga kwa lengo la kujifunza na kupata uzoefu. Nilichokigundua ni kwamba Dar es salaam inaweza kuwa na idadi kubwa zaidi ya vikundi vya sanaa ukilinganisha na mikoa mingine mikubwa kama Dodoma, Mwanza, Mbeya nk. Hii ina maana vipaji tunavyopata kuvishuhudia mpaka sasa ni vipaji vya wazawa au wahamiaji wa Dar es salaam. Hii inapunguza ladha na changamoto katika uigizaji anasistiza Bw. Mbura.

Tatu, na mwisho, waigizaji wamekosa fursa rasmi za mafunzo katika ngazi ya cheti ama diploma. Katika ngazi ya digrii idara ya sanaa ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam imekuwa ikitoa mafunzo lakini waigizaji wengi hawana vigezo vya kusoma digrii. Hii inamaanisha waigizaji wengi hawana mafunzo rasmi na wanategemea kutazama wanachokifanya wengine na kuiga au kujiunga na vikundi kupata nafasi za kufanya mazoezi kujifunza. Hii imepelekea pia wengi kudhani uigizaji ni ule wa filamu tu na kusahau uigizaji wa tamthilia za TV, Michezo ya Radio, Filamu fupi, Matangazo ya Biashara nk. ambayo humpa fursa muigizaji kuweza kukuza kipaji chake na kufikia ubora wa ndani na wa kimataifa kabla ya kuigiza kwenye filamu.

Ukiacha yote hayo, Tanzania ina vipaji vya kutosha kuipa tasnia ya filamu thamani inayostahili. Marehemu Steven Kanumba anaonekana kuwapa hamasa vijana wengi kujiingiza kwenye tasnia ya filamu na hasa uigizaji kwani idadi kubwa ya watu waliokuja kwenye usaili wamemtaja yeye kama ndio muigizaji wanaempenda. Wengine waliotajwa ni JB na Jackline Wolper. 

Tunahitaji kuibua na kukuza vipaji vipya katika uigizaji na kujali ubora wa filamu zetu. Timu nzima ya Saseni media tunayo dhamira ya dhati kuona hilo linajitokeza. Pamoja na changamoto nyingi na uchanga wa kiwanda chetu kibiashara, kimfumo na kisera bado naamini kwamba tunayo nafasi ya kujenga msingi mzuri kwa vizazi vya watoto na wajukuu wa wajukuu zetu kama tukianza sasa.

Anaelezea Bw. Issa Mbura ambaye pia ni Mwandishi wa miswada, Mtayarishaji na Mwongozaji wa filamu hapa Tanzania.

MO plans to build a USD 5 billion empire out of Dar

942331_578714148840668_773339795_n
.At the age of 38, Mohammed Dewji employs 24,000 people and claims to contribute 3.5% to Tanzania's GDP. Within the next 5 years, he plans to build a $5 billion empire out of Dar es Salaam.
by Kristin Palitza
What most entrepreneurs don’t achieve in a lifetime, he did in just over a decade. Mohammed Dewji single-handedly turned his father’s trading business into Tanzania’s largest import-export group. He grew Mohammed Enterprises Tanzania (MeTL) 30-fold and increased revenues from $30 million to $1.1 billion by diversifying into a multitude of sectors, including manufacturing, distribution, logistics, financial services, real estate, cement, energy and mobile telephony.
It’s not surprising that many people have a hard time imagining the humble beginnings Dewji comes from. His family, which stems from Gujarat state in western India and was blown in the proverbial dhow across the Indian Ocean, started out with very little. His grandmother opened a small trading shop, which she runs out of their home in Singida, a poverty-stricken town in central Tanzania. In this simple house, built from sand and mud, Dewji was born with the help of a traditional midwife.
“That wasn’t very smart. My mother and I almost died because I had the umbilical cord wrapped around my neck,” he recalls. But from then on, his fortunes changed.
His father, Gulam Dewji, who had by the mid-70s turned his mother’s shop into a flourishing import-export business, was able to sent his six children to good schools, first in Tanzania’s third-largest city Arusha and later in capital Dar es Salam. In their free time, Dewji and his siblings played tennis and golf.
“My father spent a lot of money educating us. He also believed sport creates discipline. He didn’t want us to just play a sport for fun. He wanted us to push ourselves. We probably have a thousand trophies at home that we won,” he says.
Until this day, there is almost nothing Dewji undertakes purely as a hobby. He either aims for success, or he doesn’t bother with it. And so he ploughs millions of Dollars into Tanzania’s national soccer team, the Taifa Stars instead of being content watching the odd game or kicking around a ball on a Sunday.
“I have no moderation. My wife always complains. She says, ‘Mohammed, why don’t you do things in the middle?’ It’s either very much or nothing at all,” he laughs.
His favorite sport has always been golf. Dewji spent many afternoons on Dar es Salaam’s golf course, not only because he was good it – he had 3 handicap – but also because he realized from early on that many high-profile business deals are concluded on the world’s 18-hole-lawns.
“I already liked to network as a very young guy. I was told that the golf course is a good place to meet important people. So I started playing golf. At one time, I even wanted to become a golf professional,” he says.
When his father saw that his son showed potential, he enrolled him at the legendary Arnold Palmer Golf Academy in Orlando, Florida, where Dewji also attended Saddlebrook High School. A few years later, when it became clear that Dewji wasn’t going to make the cut as a professional golfer, he decided to study international business and finance with a minor in theology at Georgetown University, an elite tertiary institution in Washington D.C., which has a long list of notable alumni, including former US president Bill Clinton, former Philippines president Gloria Arroyo and Jordan's King Abdullah.
During his time at Georgetown, Dewji learned what he says were key lessons in leadership. “Georgetown really molded me. It took me a step forward. I understood that you need to be dreaming, but not daydreaming. You need to try to dream a reality. Then you have vision,” he explains.
Pietra Rivoli, deputy dean of Georgetown University’s school of business, who taught Dewji in international finance, remembers him as a student whose energy was boundless and whose positive enthusiasm was contagious.
“While other students tried to stay awake through discussions of exchange rates, Mohammed would stay after class to talk about how the readings might pertain to the Tanzanian Schilling, and how Tanzania could address its economic challenges. Even at the age of 20 or so, he was thinking about how to improve life in his country,” she remembers.
Dewji never questioned if he should return to Africa after his graduation in 1998. He joined his father’s business, which had by then become a million Dollar trade and transport group, as chief financial controller. Five years later, at the age of 29, he was promoted to managing director, expanding his father’s business hard and fast. “I went into manufacturing and value-addition. I built a distribution system and created branches,” he says.
Today, MeTL Group is buying and selling more than 200 commodities in east, central and southern Africa, from sugar to rice, salt, fertilizer, second-hand clothing, motorcycles, bubblegum, yeast and ballpoint pens. The group also distributes 50 of its own brands, taking advantage of the fact that Tanzania borders on eight countries and is thereby an ideal import-export gateway.
“The goods that I am mainly dealing in are FMCGs [fast moving consumable goods]. It’s goods that touch people’s lives, that are needed by the common man,” he says.
The distribution of FMCGs is not an easy task in a vast country like Tanzania, which measures a million square kilometers and where 80% of the population lives in remote, rural areas. But with more than a hundred trade outlets countrywide, MeTL Group has managed to undercut multi-national consumer goods giants like Unilever and drive them out of the east African nation.
“I have a big basket of goods. I have warehousing and logistics. I have over a thousand trucks. It’s all complimenting each other. It’s very difficult for people to come from the outside and compete with me,” Dewji explains.
He invests in whatever sector he sees opportunity and growth potential. Or to say it differently: the only two industries Dewji is not involved in are beer and tobacco.
Agriculture is another key sector for MeTL Group, which with a workforce of 24,000 people is also the country’s biggest employer, and with 50,000 hectares of arable land, the largest private landowner. Dewji’s sisal farms, tea gardens and cashew fields are the drivers of his FMCG export business. A good 99% of the cashew kernels he produces, for example, are shipped to the United States.
Always thinking two steps ahead, Dewji has been making plans for how to profit most from his land, while helping to solve the challenges of Dar es Salaam’s rapid urbanization, a city of 4.4 million people. He is busy turning a 17,000 acre plot he bought cheaply several years ago, just 25 kilometers outside of the capital, into a dry-port with an internal container depot and a railway connection that will feed into Dar es Salaam’s massive, natural harbor, which is slowly but surely running out of space. It will, of course, also generate huge profits.
Since MeTL Group already contributes 3.5% of Tanzania’s GDP, it is fast outgrowing national boundaries.
“If you compare, for example, Tata and the MeTL Group, we are like Mickey Mouse. But if you look at their contribution to India, vis-à-vis my contribution to Tanzania, mine is bigger. You end up competing with everybody in your own country, and I don’t think that’s healthy. It’s a risk area. It’s a good time for us to replicate what we are doing in Tanzania in other countries,” he explains his expansion plans.
A workaholic at heart, Dewji never thinks small. “Slowly, slowly, I am planning to take on the whole continent. I am very bullish,” he says about himself. His five-year-plan is to turn MeTL Group into a $5 billion empire.
“We have to constantly revisit our visions, because we are outgrowing them so quickly. Who would have thought we could turn our business from $30 million to $1.1 billion in only 12 years? I believe that by 2018, we will be a $5bn business. Easy. It’s a no-brainer. If you look at the business we are in and the growth potential that there is, it’s amazing. My philosophy as a businessman is not to be satisfied with what I have got, but to always work harder to achieve more,” he says.
It’s been quite some years now that MeTL Group, under Dewji’s helm, has expanded so drastically that it has outgrown the loan potential of Tanzania’s banks. Dewji has found a solution to this problem, too. He goes to one of the continent’s powerhouses, South Africa, to finance new ventures. Most recently, he secured a $100 million syndicated loan through a grouping of banks.
“If I think of a top African businessman, Mohammed comes to mind. He works very long hours, is always on the move, has an eye for opportunity and a very good business sense. He is levelheaded and pays extremely close attention to detail,” says Helmut Engelbrecht, head of Investment banking in Africa at Standard Bank, one of the financial institutions that has been working closely with MeTL Group.
Whatever venture Dewji pursues links closely into his country’s national policy framework. When Tanzania’s government launched a national strategy for economic growth and poverty reduction in 2005 that was geared, among other things, towards boosting entrepreneurship to achieve value addition and employment creation, Dewji immediately saw opportunity.
“I bought a lot of sick industries, including soap production, grain milling, rice and sugar blending. I also went into the edible oil business and the textile industry,” he says.
He first expanded MeTL Group’s edible oil refining capacity from 60 to 600 tons. This year, Dewji almost quadrupled the business when he purchased an additional 1,650-ton refinery, increasing his total output to 2,250 tons of edible oil. It comes as little surprise that he has caught the attention of some of Africa’s wealthiest investors.
“I am being approached by many big boys, by multi-national companies that want to partner with me or buy me out. But I am not ready to sell yet. I can see so much more opportunity for growth. I don’t want to be paid based on what I am earning today, because I can see the tremendous potential. I am always looking five, ten years ahead,” he explains.
Another ailing sector Dewji rescued is Tanzania’s textile industry. Knowing that the east African nation is the continent’s third largest cotton producer, he decided to buy and refurbish four run-down mills, three in Tanzania and one in Mozambique. His next step will be to move into Zambia and Malawi, he says, considering Ethiopia as a potential fifth standpoint.
“We were quite lucky. Tanzania’s previous, socialist government had invested hundreds of millions of Dollars in infrastructure to build textile mills. But under socialism everything collapsed. So we were able to acquire these industries very cheaply. Obviously the machinery was all run-down, the technology obsolete. We had to rehabilitate the mills by investing in top European and American machinery,” says Dewji.
He has turned MeTL Group into sub-Sahara Africa’s largest textile player, integrating the entire value-addition chain from ginning to spinning, weaving, processing and printing.
“This year, we are going to produce more than a hundred million meters of cloth. That is more than 2,500 times the circumference of the earth,” Dewji says with pride.
Due to his entrepreneurial vigor, Tanzania is able to compete with the world’s largest and cheapest textile producer, China – at least within its own borders where government policies, including import tariffs on textiles and a standard value added tax (VAT) of 18% help protect the industry.
“Today, overall textile production is cheaper in Tanzania than in China. Labor is competitive in terms of pricing. Tanzania’s big advantage is that we have cotton, while China has to import cotton. So they cannot compete with me in my market,” Dewji explains.
His success speaks for itself. This year alone, he will earn at least $85 million after taxes, he says. But he is far too humble to take credit for the entirety of his achievement.
“People often ask me: ‘Who is smarter, you or your father?’ I ask them back: ‘Is the person who goes from zero to ten smarter, or someone who goes from ten to a thousand?’ Obviously, it’s much easier to go from ten to a thousand than to start from zero. So I believe that my father is much smarter than me,” he says.
Nothing could be further from his mind than taking it easy, or even early retirement.
“People in Tanzania look at my wealth and think I must be sunbathing and playing golf all day. But I work really hard. I put in a hundred hours a week. It’s a never stopping game. You can never say, ‘I’ve worked hard enough now’,” says Dewji, who has 60 divisional board meetings every month, or two per day.
Every morning, Dewji, who lives in with his wife, daughter and two sons in one of Dar es Salaam’s best neighborhoods, starts work at 6AM, spending the first hour responding to emails and reading commodity reports. He then runs meetings until lunch, by which time he has already put in almost seven hours of work.
“When I feel my energy levels starting to drop, I drive to the gym near my house. Every day, I run three kilometers and lift weights. I like to keep fit,” says Dewji, who is of slender built and the proud owner of a ‘six-pack’.
After gym, he goes home for lunch and to play 15 minutes with his three children before he returns to the office until late at night. The only days he takes off are Sundays, he says, when he spends time with his family and totally shuts off from work.
“Until about four years ago, I also used to work on Sundays, until my wife almost divorced me,” he jokes.
Dewji is not only growing his own empire. He is putting Tanzania on the map, making sure the east African nation – which boasts the continent’s third largest gold reserves, recently discovered uranium and gas reserves as well as a flourishing tourism industry combined with long-term political stability – will become one of sub-Sahara Africa’s big economic players, together with South Africa, Nigeria, Ghana and Kenya.
Already, Dar es Salaam is the second fastest growing African city after Lagos. And Tanzania, which boasts an average of 7% national economic growth over the past decade, has become one of the fastest growing economies in the world. According to World Bank, Tanzania’s per capita GDP more than doubled from $730 in 2000 to $1,500 in 2012.
“There’s no doubt that the country’s purchasing power is increasing,” notes Dewji, who believes the whole of sub-Saharan Africa, which currently has an overall growth rate of 4.8%, could achieve double-digit growth figures if countries are well-governed, politically stable and create conducive environments to attract investment.
As if Dewji didn’t already have enough on his plate, he is also in politics. The decision was made when he visited Singida, the town and district he grew up in, after returning from the US. As he walked the city’s streets, he encountered an old man who was scooping yellowish water out of a dirty puddle. It was his family’s only access to drinking water.
“A lot of people die from water-born diseases in rural Tanzania. But every life has the same value. So I decided to run in the next elections to change the dire situation these people live in. I was 24 years old. My parents thought I was crazy,” he remembers.
Whatever Dewji sets his mind to, he turns into a success. In 2005, he was elected as a Member of Parliament in the National Assembly of Tanzania. Five years later, he was re-elected in a landslide victory with 80% of votes. Not being a fan of ‘politicking’, Dewji, who is fluent in both English and Kiswahili, says he decided to put his own spin on the role of an MP.
“I don’t really have time for politics. I don’t go to parliament, and I don’t get involved in national politics, because I don’t want it to conflict with my business interests. All I do is serve my constituency because I believe people see hope in me,” he explains.
He puts his money where his mouth is. Every year, he donates half a million Dollars of his own money to help the people of Singida, with focus on three areas: education, health care and water. And with tangible success. In years Dewji has been representing the central Tanzanian district, access to clean water has jumped from 23% to 75%, while the number of secondary schools increased from two to 18.
“I studied theology as a minor because I feel that religion is complimenting me. It makes you strive to become a better person. I am very conscious of everything I do. If you get too engrossed in making money, you lose focus on life. Life is very short. I don’t want to die with all this money,” he explains.
Even though he makes millions, he has little interest in living a life of utter luxury, employing only a driver, a butler and private security.
“You have to live well, but you don’t have to live lavishly to the extreme. You need to be humble. I could buy a plane, a Rolls Royce or a Bentley. But I don’t. If drilling a borehole costs $20,000, you tell me to buy a watch for $20,000? To make a decision that has an impact on people’s lives is a one-second decision for me. If you get too egocentric, you lose your vision. It deceives you.”

Wednesday, January 29, 2014

VODACOM PREMIER LEAGUE: KAGERA SUGAR 0 v MTIBWA SUGAR 0, HAKUNA MBABE!

Mgeni rasmi katika kipute hicho alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Misenyi na hapa akisalimiana na wachezaji kabla ya mtanange kuanza katika uwanja wa Kaitaba.Mkuu wa Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera, Kanali Mstaafu Issa Njiku (kulia) akisalimiana na mchezaji wa Mtibwa Sugar ambaye pia ndie aliyekuwa Mgeni rasmi kwenye mtanange huo ambao timu zote zimamaliza dakika 90 kwa sare ya kutofungana na kugawana pointi moja moja.
Timu zote mbili zikimsikiliza Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera, Kanali Mstaafu Issa Njiku, kabla ya mtanange kuanza.
Kikosi cha Kagera Sugar kilichoanza leo na Mtibwa Sugar
Waamuzi wa Matanange huo
Tayari kwa Kabumbu kuanza...
Muda...Tukalianzishe kati sasa!
Mchezaji wa Mtibwa Sugar akiendeleza mashambulizi kuelekea kwenye lango la Kagera Sugar.
Hapa hukatizi ndugu..
Kona ilipigwa kelekea kwenye lango la Mtibwa Sugar...wakiugombania mpira!
Kipindi cha kwanza timu zote zilienda mapumziko bila kufungana!
Mchezaji wa Kagera Sugar akiwa kawekwa kati.
Mashabiki
Leo Mashabiki walikuwa wachache kwenye uwanja wa Kaitaba
Fri kiki kuelekea kwenye lango la Mtibwa Sugar
Chupu chupu Mtibwa Sugar wafungwe! Kipa aliupangulia mpira huo nje
Nani zaidi!!
Mpira ni Furaha ....hapa ni kipa wa Mtibwa Sugar akimkumbatia kiongozi wa Kagera Sugar  Bw. Mohamed Hussein
Mohamed Hussein(kulia) akiteta na viongozi wa Mtibwa Sugar