Monday, January 28, 2013

SEKRETARIETI YA CCM YATEMBELEA MRADI WA DARAJA LA MARAGARANI MKOANI KIGOMA LEO

Ujumbe wa Sekretarieti ya CCM,ukiongozwa na Katibu Mkuu,Ndg. Abdulrahman Kinana,Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro na Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye ukiwa katika matembezi ya kuangalia maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Maragarasi na Ujenzi wa Barabara ya kutoka Kidawe mpaka Uvinza kwa kiwango cha lami leo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana (kushoto) akizungumza na Meneja wa Kampuni ya HANIL ambao ni Wakandarasi wa ujenzi wa Daraja hilo,Bw. Jung-Sik You kutoka nchini Korea.
Meneja wa Kampuni ya HANIL ambao ni Wakandarasi wa Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Maragarasi na Ujenzi wa Barabara ya kutoka Kidawe mpaka Uvinza kwa kiwango cha lami,Bw. Jung-Sik You (kushoto) akitoa maelezo machache juu ya maendeleo ya ujenzi wa Daraja hilo kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana na kuahidi kuwa mpaka ifikikapo mwezi Septemba ama Oktoba,Daraja hilo litakuwa limeshakamilika na kulikabidhi kwa Serikali.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana (kulia) akizungumza na Meneja wa Tanroads Kigoma,Inginia Narcis Choma wakati Ujumbe wa Sekretarieti ya CCM ulipofanya ziara katika eneo la Mto Maragarasi ili kujionea hali ilivyo ya Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Maragarasi na Ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kidawe mpaka Uvinza.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Nguruka,Wilayani Uvinza mkoani Kigoma leo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akizungumza na Wazee wa Kijiji cha Nguruka,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo,wakati alipofanya ziara ya kutembelea vijiji viwili vya Wilaya hiyo ya Uvinza.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana (UVCCM),Martin Shigella akiwasalimia wananchi wa Kijiji cha Nguruka,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwasalimia wananchi wa Kijiji cha Nguruka,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nguruka,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo,waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza na pia kusikiliza shida zao wakati alipofanya ziara ya kutembelea vijiji viwili vya Wilaya hiyo ya Uvinza.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Uvinza,Wilayani Uvinza mkoani Kigoma leo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Uvinza,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo
Babu akitabasamu wakati akimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana (hayupo pichani) wakati alipokuwa akihutubia.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akijadiliana jambo na Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye.

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya,Dokii akiimba moja ya nyimbo zake alizozitunga kwa ajili ya CCM.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwa pamoja na Katibu wa CCM katika kata ya Nguruka,Asha Baraka wakati wa matembezi ya kuingia kwenye kijiji hicho cha Nguruka mkoani Kigoma leo.
Katibu wa CCM katika kata ya Nguruka,Asha Baraka akiwasalimia wananchi wake.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwasalimia wananchi waliokuwa wamejipanga barabarani kumuona.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwa na mmoja wa watoto wa kijiji hicho cha Nguruka.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiimba nyimbo na wananchi wa kijiji cha Nguruka.

TAMASHA LA USIKU WA MASTAA WA FILAMU DAR LIVE LAACHA HISTORIA

Kundi la Scorpion Girls likiongozwa na Isabela Mpanda (katikati) likiporomosha burudani wakati wa Tamasha la Usiku wa Mastaa wa Filamu lililofanyika Dar Live usiku wa kuamkia leo.
Mrembo Jacqueline Wolper akiwapa 'hi' mashabiki.
Jacob Steven 'JB' akionyesha umahiri wake wa kusakata rhumba wakati wa tamasha hilo.
Steve Nyerere naye akionyesha manjonjo yake stejini.
Mastaa wa filamu wakiwa jukwaani kuwasalimia mashabiki waliofurika ndani ya Dar Live.
Snura Mushi akiwapagawisha mashabiki.
Msanii Afande Sele akiwarusha mashabiki ndani ya Dar Live.
Tundaman akiwachizisha mashabiki.
...akizidi kuwapa raha mashabiki.
Kingwendu akifanya vitu vyake.
Richie naye akionyesha ufundi jukwaani.
Dk. Cheni na mwanadada wakienda sambamba.
Shamsa Ford akisema na mshabiki.
Bi. Mwenda akiwa kapagawa na shangwe za Dar Live.
Mrisho Mpoto akiwapa raha mashabiki.
Afande Sele akiwapa 'hi' mashabiki.
Mgeni rasmi katika tamasha hilo ambaye pia ni Meya wa Ilala, Mhe. Jerry Slaa akiwasabahi mashabiki.
Nyomi iliyohudhuria tamasha hilo.
Afande Sele akiwa amebebwa na mashabiki.
Bi. Mwenda akionyesha machejo yake stejini.
Ilikuwa ni full burudani ndani ya Dar Live.
Scorpion Girls wakizidi kupagawisha.
Snura na wanenguaji wake wakilishambulia jukwaa.
Bendi ya Twanga Pepeta ikitoa burudani katika Tamasha la Usiku wa Mastaa wa Filamu lililofanyika Dar Live usiku wa kuamkia leo.
Shilole akiwapa raha mashabiki.
Burudani zikiwa zimepamba moto mahali hapo.
Wanenguaji wa Shilole wakimpagawisha shabiki aliyepanda jukwaani.
Raha zikizidi kushamiri mahali hapo.
Baadhi ya mastaa wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi, Mhe. Jerry Slaa (katikati).
Sabrina Rupia ‘Cathy’ katika pozi.
Baadhi ya mastaa wa filamu wakiwa katika picha ya pamoja na rais wao Mwakifwamba (wa pili kulia).
Mrisho Mpoto akiwa katika pozi.
Tundaman akipozi katika Red Carpet.
Rais wa Shirikisho la Filamu nchini (TAFF), Simon Mwakifwamba katika pozi.
Jack Wolper katika pozi.
Mrembo Rose Ndauka katika pozi.
Kingwendu akipozi na watoto katika Red Carpet.
Tamasha la Usiku wa Mastaa wa Filamu lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam limeacha historia baada ya kutawaliwa na burudani za kila aina kutoka kwa wasanii wa filamu na wale wa Bongo Fleva. Pichani juu ni baadhi ya matukio yaliyochukua nafasi wakati wa tamasha hilo.
(PICHA ZOTE: ERICK EVARIST NA MUSA MATEJA/GPL)