Thursday, May 26, 2011

KAMATI YA MIUNDOMBINU YA BUNGE LA TANZANIA YATEMBELEA MAKAO MAKUU YA AIRTEL LEO

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya simu ya Airtel Tanzania,Sam Elangallor akitoa ufafanizu wa Kampuni yake kwa Wabunge wa Kamati ya Miundombinu (hawapo pichani) waliotembelea leo makao makuu ya Kampuni hiyo ili kufahamu mambo mbali mbali yafanyikayo hapo.Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh. Peter Selukamba akizungumza na Mkurugunzi wa Mahusiano wa Kampuni ya Simu ya Airtel,Beatrice Singano mara baada ya kumalizika kwa mkutano uliowakutanisha viongozi wa Kampuni hiyo na Kamati ya Miundombinu leo katika makao makuu ya kampuni hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel,Sam Elangallor pamoja na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Kampuni hiyo,Beatrice Singano wakizungumza na Mjumbe wa Kamati ya Miundombinu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini,Eng. Rambo Makani (kulia) mara baada ya mkutano wao uliomalizika mchana huu katika ukumbi wa mikutano wa Kampuni hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya simu ya Airtel Tanzania,Sam Elangallor akionyesha moja ya picha zilizokuwa zikionyeshwa kwenye Screen (hapo pichani) kwa Wabunge wa Kamati ya Miundombinu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waliotembelea leo makao makuu ya Kampuni hiyo.
Waheshimiwa Wabunge wakifatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pindi walipotembelea leo.
Baadhi ya Maafisa kutoka Wizara ya Miundombuni.
Wafanyakazi wa Airtel wakifatilia mkutano huo kwa makini.
Waheshimiwa Wabunge.
Mkutano ukiendelea.

Wednesday, May 25, 2011

MKE WA MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MAMA ASHA BILAL, AZINDUA MFUKO WA PAMOJA TUSHIKAMANE WA KUSAIDIA WAZEE WASIOJIWEZA

Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akizungumza wakati akisoma hotuba yake ya uzinduzi rasmi wa Mfuko wa kusaidia Wazee wasiojiweza wa ‘Pamoja Tushikamane’ ulio chini ya Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Tushikamane Pamoja Faundation. Hafla hiyo ya uzinduzi ilifanyika jijini Dar es Salaam jana Mei 24.
Mmoja kati ya wageni waalikwa, Bi. Eshe Sururu, akizungumza kutangaza kiasi alichotoa kuchangia mfuko huo jana, ambapo alitangaza kuchangia Sh. 500.000.
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal (katikati) na Mwenyekiti wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Tushikamane Pamoja Faundation, Rose Mwapachu (kulia) wakipiga makofi kuwashangilia watu waliojitolea kuchangia wakati wa hafla ya uzinduzi wa mfuko huo iliyofanyika kwenye Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam jana Mei 24.
Baadhi ya wageni walioalikwa kuhudhuria hafla hiyo.
Mtunza hazina wa mfuko huoakionyesha kidani cha Silver alichonunua kwa Sh. 750,000 baada ya kupigwa mnada, ambacho thamani yake halisi ilikuwa ni Sh. 150,000.
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akizungumza jambo na Balozi Juma Mwapachu, baada ya kuzindua rasmi mfuko wa Tushikamane Pamoja Faundation, iliyofanyika kwenye Hoteli ya New Africa jijini dare s Salaam.
Mama Asha Bilal (kushoto) akiongozana na Mwenyekiti wa mfuko huo kuingia ukumbini baada ya kuwasili kwenye Hoteli ya New Africa.
Mmoja kati ya wafanyakazi wa mfuko huo akibofya kitufye cha Kompyuta kuonyesha baadhi ya picha za watu waliofanikiwa kuwatembelea.
Baadhi ya Masister waliohudhuria hafla hiyo walioongazana na mmoja kati ya wazee wasiojiweza wanaomlea katika kituo chao Msimbazi.
Hawa ni baadhi ya wafanyakazi wanaojitolea kufanya kazi katika mfuko huo wakiwa katika hafla hiyo.
Baadhi ya wageni walioalikwa kuhudhuria hafla hiyo.

Baadhi ya wageni waalikwa.


Baadhi ya wageni waalikwa.

Monday, May 23, 2011

SUSAN MASHIBE FLOATING LIKE A BUTTERFLY IN USA

 Here posing with the Google Team that participated in the flight.
 Susan Mashibe.
 Before Zero G with my mentor.
 Mimi na mentor wangu tuna elea tu.
 Once we reached a safe altitude, we sat down on the floation area and weight for gravity.
 Raha sana ilikuwa aisee.
I went to do a Zero Gravity flight with my mentor Marissa.
The flight is called a Parabolic flight. It is what is used by NASA astronauts to practice before going to space. We actually floated and levitated with objects as if we were in Mars or the moon.

Friday, May 20, 2011

DKT. BILAL MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SHEREHE ZA WAUGUZI MNAZI MMOJA DAR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akisoma hotuba yake wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 40 ya kuzaliwa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA), zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salam leo Mei 20.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akimkabidhi zawadi, Paul King’ara Muuguzi kutoka mkoani Mwanza wakati wa maadhimisho ya Sherehe za ya miaka 40 ya kuzaliwa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA), zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salam leo Mei 20.
Catherine Magole, akikabidhiwa zawadi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo ya jinsi wauguzi wanavyofanya kazi kuhusu mishipa ya fahamu na Ubongo, kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama cha Wauguzi Tanzania Tawi la Moi, Prisca Tarimo, wakati alipotembelea banda la Moi Dharura, kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 40 ya kuzaliwa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA), zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salam leo Mei 20.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na Muuguzi mstaafu Jito Ramu, aliyekuwa mmoja kati ya wauguzi waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 40 ya kuzaliwa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA), zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salam leo Mei 20. Dkt Bilal alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo.
Wauguzi waliohudhuria sherehe hizo wakila kiapo mbele ya mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati wa sherehe hizo.
Wauguzi wakipita na mabango yenye ujumbe mbalimbali mbele ya mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya miaka 40 ya kuzaliwa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA), zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salam leo Mei 20.
Baadhi ya wauguzi wakiserebuka kushangilia sherehehe hiyo wakati msanii wa muziki Mrisho Mpto, walipokuwa akitoa burudani kwenye sherehe hizo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Bodi ya Udhamini baada ya sherehe hizo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Wenyeviti wa Mkoa na Wauguzi wakuu wa Hospitali za Mikoa.Picha na Muhidin Sufiani-OMR