Saturday, January 31, 2015

SIMBA YAITUNGUA JKT RUVU BAO 2 - 1 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR LEO

 Beki wa timu ya Simba,Hassan Isihaka (26) akiangalia namna ya kumzuia Mshambuliaji wa Timu ya JKT Ruvu,Jabir Aziz katika mtanange wa Ligi Kuu Tanzania Bara,uliomalizika hivi pinde kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.Simba imeshinda Bao 2-1.
 Nyanda wa Timu ya Simba,Ivo Mapunda akiwania mpira wa juu na Mshambuliaji wa timu ya JKT Ruvu,Samuel Kamuntu katika mtanange wa Ligi Kuu Tanzania Bara,uliomalizika hivi pinde kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.Simba imeshinda Bao 2-1.
 Weeee.........
 Wachezaji wa Timu ya JKT Ruvu wakishangilia goli lao la kusawazisha dhidi ya Simba,katika mtanange wa Ligi Kuu Tanzania Bara,uliomalizika hivi pinde kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.Simba imeshinda Bao 2-1.
Kiungo wa JKT Ruvu akiruka daruga .
 Kocha wa Timu ya Simba akiwapa mawaidha wachezaji wake.

CHIPUKIZI WA UVCCM WAJIFUA VIKALI TAYARI KWA KILELE CHA MIAKA 38 YA CCM KESHO

 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na Mratibu wa Maadhimisho ya Miaka 38 ya CCM, Emmanuel Nchimbi, walipokuwa wakikagua mazoezi ya vijana wa Chipukizi wa CCM ya paredi na halaiki kwa ajili ya Maadhimisho ya Kilele cha Miaka 38 ya CCM, yatakayofanyika Kitaifa kesho kwenye Uwanja wa majiMaji mjini Songea.
 Vijana wa Chipukizi wa CCM waliopo katika mazoezi ya halaiki na paredi kwa ajili ya Maadhimisho ya Miaka 38 ya CCM mjini Songea, wakikipiga saluti wakati wa mazoezi ya mwisho leo kwenye uwanja wa Majimaji
 Kijana wa Chipukizi wa CCM Mbaraka Ngonyani akionyesha umakini wake wakati akipiga saluti wakati wa mazoezi hayo ya mwisho leo
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Katibu Mkuu wa  UVCCM Sixtus Mapunda wakitazama mazoezi ya mwisho ya Chipukizi hao
 Mshika bendera ya CCM kwenye kikosi cha Bendera cha Gwaride la Umoja wa Vijana wa CCM, Sharif Mohammed na wenzake wakipita kwa ukakamavu mbele ya jukwaa kuu wakati wa mazoezi ya mwisho ya gwaride na halaiki kwa ajili ya Kilala cha Maadhimisho ya miaka 38 ya CCM yanayofanyika kesho Kitaifa kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea mkoani Ruvuma 
 Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha mazoezi ya ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Vijana wa Chipukizi wakionyesha ohodari wao wa mazoezi ya 'kikomandoo' wakati wa mazoezi yao ya mwisho ya paredi na halaiki kwa ajili ya kilele cha maadhimisho ya miaka 38 ya CCM kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
 Chipukizu hao wakiwa kwenye mazoezi ya halaiki
Mmoja wa Chipukizi wa CCM waliokuwa katika mazoezi hayo akisaidiwa baada ya kuanguka kutokana na mazoezi hayo ya mwisho kupamba moto. Alipata ahueni baada ya kupatiwa huduma ya kwanza. (Picha zote na Bashir Nkoromo)

BENKI MPYA YA MAENDELEO YA KILIMO(TADB) YAAHIDI KUTOA HUDUMA BORA ZA KIBENKI KWA WATEJA WAKE

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Thomas Samkyi akizungumza katika warsha juu ya kujadili mpango wa maendeleo wa taasisi hiyo kwa miaka 25 ijayo. Warsha hiyo ilifanyika hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency, Dar es Salaam.
Mkuu wa Mipango, Sera na Ushirikiano wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, Francis Assenga akizungumza na wadau katika mkutano huo.
Wadau wa sekta ya kilimo, uvuvi na ufugaji wakifuatilia warsha ya mpango wa maendeleo wa miaka 25 wa benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) uliofanyika kwenye hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency, Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Sophia Kaduma akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi, wakurugenzi wa benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania pamoja na wadau walioshiriki warsha ya Maendeleo ya miaka 25.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Sophia Kaduma (katikati) waliokaa akiwa na Viongozi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) mara baada ya kufungua mkutano wa Mpango wa Maendeleo wa miaka 25 ya benki hiyo.

Na Bakari Issa,Globu ya Jamii - Dar

Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TADB) imeahidi kutoa huduma bora za kibenki kwa wateja wake ili kuwa na mwanzo mzuri wa kutoa huduma bora za kifedha kwa wananchi.

Benki hiyo ya Maendeleo ya Kilimo imeanza na mtaji wa Sh 100 Billion kwa mwaka 2015-2016 na kuahidi kutenga kiasi hicho hicho cha Sh 100 Billion kila mwaka kwa ajili ya maendeleo ya kibenki.

Akizungumza katika warsha fupi iliyofanyika leo katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam,Mjumbe wa Bodi ya TADP,Adrew Temu amesema  wanataka kuanza na mwanzo mzuri wa kutoa huduma bora za kibenki kwa wananchi na kusema kuwa benki hiyo sio tu ya watu wa tabaka la juu bali itawahusu hata watu wa tabaka la kati,chini,wazalishaji,wasindikaji katika sekta ya kilimo.

Aidha,Bw.Temu amesema wataendelea kuwaelimisha wananchi juu ya huduma za kibenki ya kilimo na kuahidi watakayoyatasmini watatekeleza na kutoa msimamo katika tija kwa pamoja na kutoa huduma nafuu za kifedha.

Kwa upande wake,Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Chakula,Sophia Kaduma amesisitiza juu ya umuhimu wa kupanga mikakati na kuweka vipao mbele kwa kuhakikisha mikakati pamoja na vipao mbele hivyo vinasimamiwa na kuleta matokeo ya haraka.


Pia amesisitiza TADB kutafuta fedha na mitaji ili kukuza mtaji wa benki pamoja na kuiga mfano kutoka katika nchi kama za India na China.

Kenya National Assembly Committee on regional integration visits EACJ

The Judge President East African Court of Justice, Hon. Justice Dr. Emmanuel Ugirashebuja welcomed Members of the committee on regional integration from the National Assembly of the Republic of Kenya.

 His Lordship informed the Committee on the composition of the Court, achievements and challenges of the Court - that the EACJ is composed of ten (10) Judges, two (2) from each Partner State and that each of the two divisions of the Court has a bench of five (5) Judges.

The Judge President also informed the Committee the two Judges representing the Republic of Kenya,  Hon. Mr. Justice Aaron Ringera of the Appellate Division and Hon. Mr. Justice Isaac Lenaola Deputy Principal Judge of the First Instance Division.

The Judge President further informed the group that the EACJ has established Sub-registries in all Partner States’ capitals and that in Kenya it is located at the Milimani Law Courts. The Sub-registries were established to bring justice closer to the East Africans by giving the citizens access to the Court for any dispute that might arise.
Judge President Hon. Justice Dr. Emmanuel Ugirashebuja addressing the team 

His Lordship again informed the team that the sub-registries have led to an increase in the cases before the Court as litigants no longer have to travel to Arusha to file their cases which is costly and time consuming.  
The Committee was informed that in an effort to enhance its publicity and to reach the Citizens in East Africa, the Court has been going to the Partner States to sensitize Civil Society Organisations and Judges of the National Courts on the role and operations of the Court.

In 2014 the Court held workshops in Kampala, Uganda and Kigali, Rwanda to educate Civil Society organizations the role of the Court in settling disputes that are in violation of the Treaty for the Establishment of the East African Community.

The Court targets the Civil Society with the aim to educate on the procedures of lodging a case in the EACJ while the Judges of the National Courts are made well informed and aware on how to refer matters on preliminary rulings to the EACJ for interpretation in accordance to Articles 30 (1) and 34 of the Treaty. The Court is still in the process of educating the target groups in the other Partner States.
Ag. Registrar Ms. Geraldine Umugwaneza talking to the Committee Members in the Court Room

The Judge President also informed the Committee that Judges of the Court serving on ad hoc basis is one of the major challenges faced by the Court. That due to increase of cases especially in the First Instance Division, the Court experiences some delay in determining these cases hence leading to justice delayed. 

He also added that some Judges serve in the National Courts making it very difficult to have all of them free from their National judicial services at the same time.

Justice Ugirashebuja noted that the limited Jurisdiction of the Court is another challenge. Due to limited jurisdiction on human rights issues, some cases are dismissed on grounds of lack of jurisdiction. However, he said that the Protocol on the extension of the Court’s jurisdiction is under discussion and it is expected that the Council of Ministers will make a decision at a suitable time in pursuant to Article 27 (2) of the Treaty.
Group photo opportunity Judge President and Ag. Registrar with the Team.

His Lordship thanked the team for having considered the Court and encouraged them to be Its Ambassadors and that the Court will continue pursuing justice and to achieve its mandate.

Hon. Christopher Doye, Nakuleu, MP, Turkana North Constituency Head of the Committee, thanked the Judge President and Ag. Registrar Ms. Geraldine Umugwaneza for allowing them to visit the Court and sharing its experience on the achievements, challenges and developments of the Court and urged that the Judges be allowed to be permanent residents especially in the First Instance Division and that the Protocol on extension of the jurisdiction of the Court be concluded as issues on human rights are critical as the Partner States are implementing of the Customs and Common Market Protocols. 

PAC yaishauri Serikali namna ya kuinusuru kampuni ya TTCL

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Kabwe Zitto (kulia) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Deo Filikunjombe wakiwa katika majukumu yao. Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Kabwe Zitto (kulia) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Deo Filikunjombe wakiwa katika majukumu yao.Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) akiwa katika majukumu. Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) akiwa katika majukumu.

  KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imetoa mapendekezo ya kuinusuru Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kutokana na hali mbaya ya kampuni hiyo kifedha kwa sasa ambapo inaendeshwa kwa hasara huku ikiwa na madeni makubwa. 

PAC imetoa mapendekezo hayo katika taarifa yao kwa bunge ya mwaka juu ya ukaguzi wa hesabu za Serikali kwa mashirika ya umma iliyotolewa Januari 28 mwaka 2015. Kwa mujibu wa taarifa ya PAC hali ya mapato na matumizi ya TTCL kwa mwaka 2012 ilipata hasara ya bilioni 20.883 huku kwa mwaka 2013 ikipata hasara ya bilioni 16.258. 

PAC ilisema majumuisho ya hasara ya TTCL kupata hasara kwa takribani kwa miaka 10, Kampuni sasa imekuwa na hasara ambayo kwa mwaka 2013 ilifikia bilioni 334.48, jambo ambalo limeiondolea mvuto wa kukopeshwa na taasisi za fedha hata zile zenye nia ya kuikopesha. 

 "...Ukosefu wa fedha za kutosha kutekeleza miradi ya Kampuni umekuwa kikwazo kwa TTCL kukabiliana na ushindani wa kibiashara. Kwa kipindi kirefu ufanisi wa TTCL kiuwekezaji na kifedha umeendelea kudorora. Tangu TTCL ibinafsishwe mwaka 2001, hakuna uwekezaji mkubwa uliofanyika na mpango wa kutafuta mkopo kutoka mabenki ya ndani na nje ya nchi unakwamishwa na masharti ya kupata udhamini wa Serikali," ilieleza taarifa hiyo ya PAC. 

 PAC iliongeza kuwa ukiacha madeni yaliopo pia TTCL inadaiwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) jumla ya bilioni 25 hivyo kufanya jumla ya deni kufikia bilioni 101.6. Kamati hiyo ya bunge imesema kuna umuhimu wa Serikali kufanya maamuzi ya haraka ya kuikwamua TTCL ili iweze kuendelea kutoa huduma kwenye Sekta ya Mawasiliano ikizingatiwa kuwa ndiyo inayoendesha Mkongo wa Taifa wa mawasiliano.

 Katika mapendekezo ya PAC ili kuikwamua TTCL imeishauri Serikali kununua hisa asilimia 35 zinazomilikiwa na Bharti Airtel katika TTCL kwa gharama ndogo kwani Bharti Airtel haikutimiza kikamilifu masharti ya mkataba wa mauziano ya hisa hizo hapo awali kwani tangu inunue hisa hizo haijafanya uwekezaji katika Kampuni ya TTCL. 

 "...TTCL isamehewe deni la Serikali Sh. 76.6 bilioni na deni la TCRA Sh. 25 bilioni ambayo jumla yake ni Sh. 101.6 bilioni na fedha hizo zipelekwe kuongeza mtaji ili Kampuni itoke kwenye kuwa na mtaji hasi wa Sh. 87.896 bilioni na kuwa na mtaji chanya wa sh. 13.704 bilioni. Likifanyika hili basi Kampuni hiyo itaweza kukopesheka. 

Serikali ikamilishe taratibu zake za kuimilikisha TTCL Mkongo wa Taifa ili izidi kuuendeleza kwa ufanisi na kuongeza mapato ya TTCL," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo. Hata hivyo PAC imeshauri kuwa kuna umuhimu wa kufanya marekebisho ya muundo wa Kampuni ya TTCL kwani kwa sasa ina idadi kubwa ya wafanyakazi (1549) isiyoweza kuwalipa. 

Aidha, ilibainisha kuwa kwa sasa zinahitajika bilioni 32 kwa ajili ya kugharamia urekebishaji wa muundo wa Kampuni ili uendane na mahitaji ya utoaji wa huduma mbalimbali. 

 Mashirika mengine yenye hali mbaya kifedha na uendeshaji ni pamoja na Shirika la Ndege Tanzania, ATCL ambayo kwa sasa ina madeni makubwa huku ikiwa na ndege moja aina ya Dash 8–Q 300, Wafanyakazi 142 na Jengo la ATC House lililoko mtaa wa Ohio, Dar es Salaam.

Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela washauriwa kutumia ujuzi kujiajiri

 Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa wa pili kulia akizungumza na Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Kyela Dr. Festo Dugange jana wakati wa ziara ya kuhamasisha vijana wa Kyela. Wa kwanza kulia ni Afisa Maendeleo ya Vijana Bi. Amina Sanga, wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele na wa pili kushoto ni Afisa Vijana Mkoa wa Mbeya Bw. George Mbijima.
 Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga akiwaelimisha vijana wa Wilaya ya Kyela kuhusu mwongozo unaosimamia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana wakati wa semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyofanyika jana katika Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya.
 Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya walioudhuria semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana wakifuatilia mambo mbalimbali yaliyokua yakiendelea wakati wa semina hiyo.
 Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela wakiwa katika kikundi kujadiliana namna ya kuandika andiko la mradi baada ya kupata mafunzo ya jinsi ya kuandika andiko la mradi wakati wa semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyofanyika jana katika Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya.
Mwenyekiti wa Wadau Self Supporting Group Bw. Godbless Konga wanne kulia akizungumza na maafisa kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo walipotembelea kikundi hicho kuangalia mradi unaoendeshwa na vijana wa kikundi hicho jana wakati wa ziara ya kukagua miradi ya vijana wa Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya.

LICHA YA CHANGAMOTO NYINGI BARA LA AFRIKA LINAPIGA HATUA - ZUMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisoma makabrasha ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa AU unaofanyika kwa siku mbili jijini Addis Ababa kuanzia leo. Nyuma ya Mhe. Rais ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb). Waziri wa Jinsia na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Sophia Simba (Mb) na Balozi wa Tanznia nchini Ethiopia, Mhe. Naimi Aziz (mwenye ushungi).

Na Ally Kondo, Addis Ababa
Wakuu wa Nchi za Afrika wamekumbushwa kuwa, Mwaka 2015 umeingia lakini Bara la Afrika bado linakabiliwa na changamoto nyingi ambazo kama hazitapatiwa ufumbuzi ustawi wa bara hilo utaendelea kudumaa. Kauli hiyo ilikuwa inarudiwa mara kwa mara na viongozi waliopata fursa ya kuhutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika jijini Addis Ababa siku ya Ijumaa tarehe 30 Januari 2015.

Changamoto hizo ni pamoja na mabadiliko ya tabianchi, ugaidi, migogoro ya kutumia silaha, ukatili wa kutisha, biashara haramu ya binadamu, umasikini na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola. Walishauri katika mwaka wa 2015 lazima matatizo hayo yajadiliwe kwa kina kwa madhumuni ya kuyatafutia ufumbuzi wa kudumu.

Alipokuwa anahutubia mkutano huo, Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mhe. Nkosazana Zuma alisema kuwa, licha ya changamoto hizo, Bara la Afrika linapiga hatua kimaendeleo na kwamba Agenda 2063 inayowasilishwa katika Mkutano huo inatoa wito kwa Serikali na sekta nyingine kushirikiana kwa pamoja ili kukuza uchumi kwa kuweka mkazo kwenye ubunifu katika sekta ya kilimo, usindikaji wa mazao na ujenzi wa miundombinu.

Mhe. Zuma alisisitiza umuhimu wa kutumia fedha za ndani kwa ajili ya kugharamia miradi ya kipaumbele ambayo imezingatiwa katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka 10 ambao nao utawasilishwa katika mkutano huo. Alieleza kuwa Sekretarieti imefanyia kazi pendekezo la kutafuta vyanzo mbdala vya fedha ambapo Mawaziri wa Fedha walijadili na ripoti yao itawasilishwa wakati wa mkutano huo. Umoja wa Afrika pia umeanzisha Mfuko Maalum utakaozinduliwa wakati wa mkutano huo kwa ajili ya kuhifadhi fedha hizo.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. Ban Ki-moon alieleza kuwa mwaka 2014, AU na UN zilishirikiana kutafuta amani katika nchi zenye migogoro. Alisema mafanikio makubwa yalipatikana na hivyo kusisitiza kuwa pande zilizosaini mikataba ya amani lazima zitekeleze vipengele vya mikataba hiyo. Alitoa mfano wa Mkataba wa Arusha na kusema kuwa pande zinazohusika zitekeleze makubaliano ya kugawana madaraka. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kukitokomeza kikundi cha waasi cha FDLR kinachoendesha uasi wake Mashariki mwa DRC.

Mhe. Ban Ki-moon pia aliwakemea viongozi wa Afrika wanaong’ang’ania madaraka. Aliwashauri viongozi hao waache tabia hiyo na kuruhusu demokrasia ichukue mkondo wake.
Rais wa Kikao cha 69 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda, Mhe. Sam Kutesa pamoja na mambo mengine, alizungumzia mabadiliko ya mfumo katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Alisema katika uongozi wake atafanya jitihada kuhakikisha kuwa mfumo wa Baraza hilo, chombo ambacho alikitaja kama kisichokuwa na demokrasia kuliko vyombo vyote duniani unafanyiwa mabadiliko.

Viongozi hao pia walihimiza juhudi za kutafuta tiba na chanjo ya ugonjwa wa Ebola na kusisitiza kuwa kampeni ifanywe ili nchi zilizoathirika na ugonjwa huo zisamehewe madeni.

Mkurugenzi Mkuu wa NHC atembelea miradi Geita na Mwanza

Msimamizi wa mradi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Bombambili Geita Bw, Julius Ntoga (kulia) akitoa maelezo ya mradi huo kwa ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu alipotembelea mradi huo jana. Mradi huo wenye nyumba 48 ni wa nyumba za kuuza na unakamilika Februari mwaka huu.
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC ukitembelea nyumba za gharama nafuu zilizojengwa eneo la Bombambili, Geita kwa ajili ya kuuzia wananchi.
Sehemu ya nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC eneo la Bombambili Mkoani Geita
Sehemu ya nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC eneo la Bombambili Mkoani Geita
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akitoa ufafanuzi kwa jopo la wasimamizi wa miradi ya Shirika na watendaji wengine ya namna wanavyoweza kupunguza gharama za ujenzi wa nyumba ili wananchi wengi wa kipato cha kati na chini waweze kumudu kuzinunua.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akiwapa mawaidha ya namna ya kupanua uwezo wa kikundi cha Vijana Kazi Wilayani Misungwi alipokitembelea jana. Kikundi hiki ni mojawapo ya vikundi vilivyopewa na NHC msaada wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana ili kujiajiri. Bw. Mchechu ameziasa Halmashauri zote nchini kusaidia makundi ya vijana kwa kuwapa maeneo ya kufanyia kazi zao za kufyatua matofali na kuwapa tenda za ujenzi zinazokuwepo katika Halmashauri  hizo.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akionyeshwa na Afisa Ardhi wa Halmashauri ya Misungwi eneo lililotengwa na Halmashauri hiyo kwa ajili ya NHC kujenga nyumba za gharama nafuu
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC ukionyeshwa ramani yenye eneo lililotengwa na Halmashauri ya Wilaya ya Nyamagana na Afisa Mipango Miji Bw. Maduhuna Bw. Ardhi Bw. Salvatory ili NHC iweze kujenga mji unaojitegemea(satellite town) na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Jiji la Mwanza linalopakana na nchi za maziwa makuu.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akiwashauri viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyamagana kuona uwezekano wa kupunguza gharama ya NHC kulipa fidia ya eneo lililotengwa kujenga mji wa kisasa. Bw. Mchechu aliwataka viongozi hao kuitizama NHC kama chombo cha Serikali kinachowaletea maendeleo yao na si kama mwekezaji ili kufanya upangaji wa eneo hilo muhimu kufanyika.
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC ukipokelewa katika mradi wa ujenzi wa nyumba eneo la Buswelu na Mkandarasi wa mradi huo Bw. Said Kiure(kulia)’
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu ukipewa maelezo ya mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu na Mkandarasi wa mradi huo Injinia Saidi Kiure walipotembelea mradi huo Jijini Mwanza jana. Suala la kupunguza gharama za ujenzi wa nyumba hizo ili ziwe nafuu lilisisitizwa na Mkurugenzi Mkuu.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akiendelea kutembezwa na Meneja wa NHC Mkoa wa Mwanza Bw. Benedict Kilimba katika mradi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC eneo la Buswelu.

Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu na ujumbe wake wakitembelea nyumba za NHC zilizoko barabara ya Kenyatta Jijini Mwanza ambazo zitaendelezwa ili kuongeza mapato ya Shirika na taswira ya Jiji hilo.