Saturday, August 31, 2013

Filamu Mpya ya Msanii Elizabeth Michael (Lulu) yazinduliwa kwa kishindo jijini Dar

 Elizabeth Michael Aka Lulu akitoa Shukrani kwaWadau wote waliojitokeza katika Usiku wake wa uzinduzi wa Filamu yake Mpya iitwayo Foolish Age uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City Usiku wa Kuamkia Leo
 Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya Proin Promotions Limited Geofrey Lukaza (Kushoto) akiwa na Waifu wake Groly Lukaza (katikakati) pamoja na Pedeshee Mamaa Ng'onzi wakijiachia Mbele ya Kamera ya Lukaza Blog usiku wa kuamkia Leo katika uzinduzi wa Filamu ya Lulu iitwayo Foolish Age katika Ukumbi wa Mlimani City chini ya kampuni ya Proin Promotions Limited
 Lady Jay Dee aka Anaconda akitoa Burudani katika Uzinduzi wa Filamu mpya ya Lulu iitwayo Foolish Age iliyotengenezwa na Kampuni ya Proin Promotions Limited, Lady Jay Dee akiwa pamoja na Machozi Band walitoa Bururdani Safi Sana katika Uzinduzi huo Uliofanywa na Kampuni ya Proin Promotions Limited katika Ukumbi wa Mlimani City usiku wa Kuamkia Leo
Msanii Barnaba akitoa burudani katika uzinduzi wa Filamu mpya ya Lulu uliofanya na Kampuni ya Proin Promotions Limited katika ukumbi wa Mlimani City Usiku wa Kuamkia leo
 Katikati ni Mama Mzazi wa Elizabeth Michael akiongea kwa furaha huku akitoa machozi na Msanii wa Filamu Tanzania Wema Abraham Sepetu(kushoto) na Rafiki yao katika Uzinduzi wa Filamu ya Lulu ulioandaliwa na kufanywa na Kampuni ya Proin Promotions Limited katika Ukumbi wa Mlimani City usiku wa Kuamkia Leo
 Wema Sepetu (aliyepiga magoti) akikumbatiana na Mama yake mzazi Lulu wakati wa Uzinduzi wa Filamu ya Mwanae Elizabeth Michael katika Ukumbi wa Mlimani City, uzinduzi uliokwenda sambamba na burudani kutoka Kwa Wasanii mbalimbali wa Muziki wa Bongo Fleva katika Ukumbi wa Mlimani City usiku wa Kuamkia leo.
Wadau wakisakata Mduara katika uzinduzi huo wa filamu ya Lulu iitwayo Foolish Age uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City Usiku wa kuamkia leo, Uzinduzi huo wa Kufa mtu uliofanywa na Kampuni ya Proin Promotions Limited ulifana kupita Kiasi
 Baadhi ya Wadau Mbalimbali waliojitokeza katika Uzinduzi huo uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City chini ya Kampuni ya Pron Promotions Limited.
Meza ya Viongozi wa Kampuni ya Proin Promotions Limited Kuanzia Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Proin Promotions Limited Bw Geofrey Lukaza, akifuatiwa na Pedeshee Mamaa Ng'onzi, Bwa Johnson Lukaza Mwenyekiti waa Makampuni ya Proin Tanzania, Gadna G Habash na Lady Jay Dee aka Anaconda wakiwa makini Kufuatilia Uzinduzi Mzima wa Filamu Mpya ya Lulu iitwayo Foolish Age uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City chini ya Kampuni ya Proin Promotions Limited.
Paul SekaBoy Mkurugenzi Wa Sekaboyi Production akiwa na rafiki yake katika uzinduzi wa Filamu ya Lulu iitwayo Foolish Age katika Ukumbi wa Mlimani City Usikuwa kuamkia leo
Mmiliki wa Lukaza Blog Josephat Lukaza akiwa katika Picha ya Pamoja na Mmoja wa Watembeleaji wakubwa kabisa wa Lukaza Blog Mamaa Fetty katika Uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Usiku wa Kuamkia leo
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Lady jay Dee akituzwa Mahela katika Uzinduzi wa Filamu Mpya ya LULU iitwayo Foolish Age ndani ya ukumbi wa Mlimani City Usiku wa Kuamkia leo

Friday, August 30, 2013

WAZIRI MKUU ATOA SH. MILIONI 10 KUSAIDIA VIJANA 87 WAJITEGEMEE

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ameahidi kutoa sh. milioni 10 ili kuwasaidia vijana wanaoishi kwenye kijiji cha vijana cha Tulu ambao wameamua kujitegemea kwa uzalishaji kupitia kilimo, matumizi ya misitu na ufugaji.
 
Alitoa ahadi hiyo jana jioni (Alhamisi, Agosti 29, 2013) wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara na vijana wa kijiji hicho pamoja na wakazi wa vijiji jirani vya Tumbili na Lufwisi wilayani Sikonge mkoani Tabora.
 
Kijiji cha Vijana cha Tulu ambacho wenyewe wanakiita Pathfinders Green City (Jiji la Watafuta Njia) kilianzishwa Aprili 2013 kikiwa ni msitu mtupu baada ya kupewa ekari 280 kutoka vijiji jirani vya Tumbili na Lufwisi. Kilianzishwa kikiwa na vijana 68 kutoka katika kata zote 17 za Wilaya ya Sikonge. Hivi sasa kijiji kina vijana 87 wakiwamo wasichana 22 na wavulana 65 wenye umri wa kati ya miaka 18 na 24.
 
Akizungumza na vijana na wananchi wa vijiji hivyo, Waziri Mkuu alisema atawapatia seti moja ya luninga ili waweze kupata taarifa za matukio mbalimbali ya kitaifa na duniani. Alisema wanahitaji pia deck ili wakipata programu za mafunzo za kwenye CD au DVD, iwasadie kuangalia. Aliahidi kuwapatia bajaj moja ili iwasaidie wakati wa dharura waweze kufika makao makuu ya wilaya ambako ni umbali wa kilometa saba kutoka kijijini hapo.
 
“Katika muda wa miezi mitatu ambayo mmekaa hapa kazi mliyofanya ni kubwa. Siku zote mwanzo ni mgumu lakini nimefarijika kwa sababu ninyi mmethubutu. Mmetumia nguvu zenu kubadilisha mazingira ya mahali mlipo. Haya ndiyo maisha plus yenyewe... maisha plus ya uhalisia na siyo yale ya kwenye televisheni,” alisema huku akishangiliwa.
 
“Nimeona bustani, mabanda ya nyuki, mradi wa kufyatua matofali na Mkuu wa Mkoa (Bibi. Fatma Mwassa) amesema anataka mfuge kuku wa nyama na mayai. Mimi nasema, fedha hizi ziwasaidie kufuga kuku lakini wawe wa kienyeji, mfuge kibiashara zaidi mtapata mayai na kuku wa nyama pia mtauza na kupata fedha za kujikimu,” alisema.
 
Waziri Mkuu ambaye yuko mkoani Tabora kwa ajili ya mahafali ya chuo cha nyuki yatakayofanyika leo, alienda kukagua kijiji hicho ambacho vijana wake ameamua kufuata mfumo wa ‘maisha plus’. Alisema anatambua changamoto ya uhaba wa maji inayokikabili kijiji hicho na akaahidi kuwatafutia wataalam wa kuchimba visima ili waje kufanya utafiti wa maji katika maeneo jirani kwa vifaa vya kisasa zaidi.
 
Naye, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki aliahidi kuwachangia vijana hao sh. milioni tano ili ziwasadie kujiletea maendeleo kwani wamekuwa vijana wa mfano kwa wilaya nyingine na mikoa mingine hapa nchini.
 
Waziri Mkuu aliweka jiwe la msingi kwenye jengo la utawala la kijiji hicho ambalo linatarajia kugharimu sh. milioni 50 hadi kukamilika kwake. Jengo hilo litakuwa na ofisi, ukumbi mdogo wa mikutano na stoo. Pia wanapanga kujenga nyumba 12 za kisasa za kuanzia kwa ajili ya vijana waishio kijijini humo. Hivi sasa vijana wanaishi kwenye nyumba za udongo zilizoezekwa kwa nyasi.
 
Mradi wa kijiji hicho unasimamiwa na Kampuni ya KP Media lakini unafadhiliwa na Halmashauri ya Wilayaya Sikonge ambayo mwaka jana iliwapatia sh. milioni 488 na mwaka huu imepanga kuwapatia sh. milioni 300 ili kuwawezesha vijana kutumia fursa zilizopo kujifunza mbinu mbalimbali za uzalishaji mali kwa kutumia teknolojia za kisasa.
 
Mapema, Bwana Shamba wa kijiji hicho, Bw. Aggrey Kitundu alimweleza Waziri Mkuu kuwa wamekwishalima ekari 10 kwa ajili ya mbogamboga, alkini wametumia nusu eka kupanda miche ya nyanya 4,640 na miche ya vitunguu 6,500. Wamekwishafyatua matofali 7,542 ya Hydrafoam na matofali mengine 49,558 aina ya funganishi (yenye matundu) yamekwishafyatuliwa. Pia wamejenga mabanda 12 ya kufugia nyuki yenye uwezo kwa kutunza mizinga 1,000 lakini hadi sasa wamekwishatengeza mizinga 600 ya kisasa.
 
Naye Mratibu wa mradi huo wa kijiji cha vijana, Bw. Masoud Kipanya alisema baada ya kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu, kijiji cha vijana kinatarajia kuwa na miradi ya ufugaji wa nyuki, uchakataji na usindikaji asali, ufugaji wa kuku wa nyama na mayai na ufugaji wa ng’ombe wa maziwa.
 
Miradi mingine ni kilimo cha mbogamboga na matunda kwa kutumia teknolojia ya Green House na umwagiliaji kwa njia ya matone (Drip Irrigation), kilimo cha mazao ya biashara na chakula, mradi wa ujenzi wa nyumba bora na uchongaji wa samani, mradi wa uhifadhi wa mazingira na upandaji miti pamoja na usindikaji nafaka na mazao ya mafuta.

UJUMBE WA ZANZIBAR WAKUTANA NA WAZIRI MKUU NA KAMPUNI YA SAKURA NCHINI UHOLANZI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akiwa katika picha Waziri Mkuu wa Serikali ya Uholanzi Mark Rutte,alipofika katika Ofisi ya Waziri huyo Nchini The Hague Uholanzi akiwa katika ziara na Ujumbe aliofuatana nao.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu wa Serikali ya Uholanzi Mark Rutte,alipofika katika Ofisi ya Waziri huyo Nchini The Hague Uholanzi akiwa katika ziara na Ujumbe aliofuatana nao,(kushoto) Waziri wa Ardhi,Maji,Makaazi na Nishati Ramadhan Abdalla Shaaban.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akifuatana na Mwenyeji wake Waziri Mkuu wa Serikali ya Uholanzi Mark Rutte,baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ya Waziri huyo Nchini The Hague Uholanzi akiwa katika ziara ya Kiserikali na Ujumbe aliofuatana nao.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Bibi Regine Aalders,kutoka Wizara ya Afya nchini Uholanzi,wakati alipotembelea katika Ofisi ya Kampuni ya Sakura Finatek jana,ambayo inatengeneza Vifaa vya maabara vya Uchunguzi wa Binadamu,nje ya Mji wa The Hague Nchini Uholanzi akiwa katika ziara ya Kiserikali.
Bibi Regine Aalders,kutoka Wizara ya Afya nchini Uholanzi,alipokuwa akiwasilisha mada wakati wa mkutano wa kampuni ya Sekura na Makampuni mengine wakati walipokutana na Ujumbe wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar nchini humo kwa ziara ya Kiserikali ambapo ziara hiyo itamalizika kesho.
Baadhi mya Viongozi wa Ujumbe wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na wenyeji wao Viongozi wa kampuni ya Sakura Finetek Europe,inayojishuhulisha na Utengenezaji wa Vifaa vya maabara vya Uchunguzi wa Binadamu,iliyopo nje ya Mji wa The Hague Nchini Uholanzi wakiwa mkutano wa kufikia kuongeza kasi ya kutoa huduma bora za Kiafya katika ziara ya Kiserikali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akitoa hutuba yake wakati wa mkutano na Kampuni ya Sakura Finetek Europe, inatengeneza Vifaa vya maabara vya Uchunguzi wa Binadamu,wakati alipotembelea katika Ofisi ya Kampuni hiyo jana,iliyopo nje ya Mji wa The Hague Nchini Uholanzi,Rais akiwa katika ziara ya Kiserikali.
Baadhi ya Viongozi na Maafisa wa Ujumbe wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakiwa katika mkutano wa Ushirikiano na kampuni ya Sakura Finetek Europe,katika hatua za makusudi katika kuongeza kasi ya utoaji wa Huduma za Kiafya,walipokuwa katika ziaraya Kiserikali nchini Uholanzi.
Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakiwa katika mkutano wa Ushirikiano na kampuni ya Sakura Finetek Europe,katika hatua za makusudi katika kuongeza kasi ya utoaji wa Huduma za Kiafya,walipokuwa katika ziara ya Kiserikali nchini Uholanzi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Mtaaalamu wa matumizi ya Vifaa vya maabara Robert Heijmen,alipotembelea mashine mbali mbali za uchunguzi wakati wa mkutano na Kampuni ya Sakura Finetek Europe, inayotengeneza Vifaa vya maabara vya Uchunguzi wa maradhi ya Binadamu, jana akiwa katika ziara ya kiserikali nchini uholanzi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipokea Cheki kutoka kwa Rais,pia Meneja Mkuu wa kamapuni ya Sakura Finetek Europe, Chris Koeman,kwa ajili ya Uchunguzi wa Maradhi ya binadamu katika Hospitali ya Mnazi Mmoja,wakati wa mkutano wa ushiriano katika kukuza huduma na kampuni hiyo,na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,katika ziara Nchini Uholanzi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Kamapuni ya Sakura Finetek ,baada ya mkutano uliofanyika jana baina ya kampuni na Ujumbe wa Serikali ya Mapinduzi ukiwa katika ziara Nchini Uholanzi. .[ Picha na Ramadhan Othman,Uholanzi.]

BAN KI MOON ALAANI KUUAWA KWA MLINZI WA AMANI WA TANZANIA,DRC

Pichani ni walinzi wa Amani wakiwa katika moja ya doria kwenye mitaa ya mji wa Goma, mwanzoni mwa wiki hii kumetokea mapingano katika eneo la vilima vya Kibati Magharibi ya Kivu ambapo kundi la waasi la M23 lilishambulia walinzi wa amani wa Misheni ya Kutuliza Amani katika DRC ( MONUSCO) waliokuwa katika Operesheni ya kulinda raia wakishirikiana na Majeshi ya Serikali ya DRC. Shambulio hilo limesababisha mwanajeshi Mtanzania kupoteza maisha na wengine 10 wakiwamo wanajeshi wa Afrika ya Kusini wamejeruhiwa. Tukio la kushambuliwa kwa walinzi hao limelaaniwa vikali na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, na Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa. Ban Ki Moon na Baraza Kuu wametuma salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu na familia za wale waliojeruhiwa na kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Afrika ya Kusini. Aidha Baraza Kuu limesisitiza kwamba vitendo vinavyolenga kudhoofisha mamlaka ya MONUSCO havitavumiliwa.

Na Mwandishi Maalum

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon amelaani kuuawa kwa Mlinzi wa Amani kutoka Tanzania ambapo wengine kadhaa wamejeruhiwa baada ya kushambuliwa na kundi la waasi la M23 katika katika eneo la Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaii wa Katibu Mkuu , inaeleza kwamba. “ Katibu Mkuu analaani kwa nguvu zote mauaji ya mlinzi huyo na kujeruhiwa kwa walinzi wengine 10 na anatoa salamu zake za rambirambi kwa familia za walinzi hao na kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Afrika ya kusini”.

Mashambulizi dhidi ya walinzi hao wa Amani yametokea siku ya jumatano katika Vilima vya Kibati Magharibi ya Kivu ambako Misheni ya kutuliza Amani ya Umoja wa Mataifa katika DRC ( MONUSCO) ilikuwa ikisaidiana na majeshi ya serikali ya DRC kuwalinda raia katika eneo la Goma ambalo lina idadi kubwa ya watu.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, MONUSCO ilijibu mashambulizi hayo kwa kutumia zana mbalimbali za kivita yakiwamo makombora, mizinga na helkopta za kivita wakati majeshi ya DRC yalitumia askari wa ardhini, vifaru na helkopta za kivita na kwamba operesheni hiyo bado inaendelea.

Taarifa inaeleza zaidi kwamba Umoja wa Mataifa utaendelea kuwajibika na kuhakikisha inachukua hatua zote muhimu kwa kuzingatia Azimio namba 2094 ( 2013) la Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa ambalo linasisitiza ulinzi wa raia katika eneo hilo la Mashariki ya Kongo.

Wakati huo huo , wakati mapigano yakiendelea, Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, katika kikao chake kilichofanyika siku ya Alhamisi nalo limetoa tamko la kulaani vikali tukio la kuuawa kwa mlinzi wa Amani wa Tanzania, na kutoa salamu zako za pole kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na familia ya marehemu pamja na wale waliojeruhiwa.

Tamko la Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa limetolewa taarifa hiyo baada ya Baraza hilo kupokea taarifa rasmi iliyowasilishwa na Naibu Mkuu wa Idara ya Operesheni za Ulinzi wa Amani, Bw. Edmond Mulet kuhusu kinachoendelea katika DRC.

Baraza pia limelaani kwa nvugu zote dhidi ya kujirudia rudia kwa matukio yanayofanywa na M23 yanayolenga MONUSCO na rais yakuwalenga raia na MONUSCO.

Na kwa sababu hiyo Baraza Kuu la Usalama limetaka mamlaka ya DRC kuchunguza tukio la kuuawa kwa mlinzi huyo wa Amani na kisha kuwafikisha mbele ya sheria watakaobainika kuhusika na tukio hilo.

Aidha Baraza Kuu limerejea tena tamko lake la kuitaka M23 na makundi mengine yenye silaha katika DRC kuacha aina zote za machafuko na kuweka chini silaha zao. Na kwamba, halitasita kupitisha vikwazo vya nyongeza kwa yeyeyote yule ambaye atabainika kujihusisha na fujo na machafuko na kwamba vikwazo hivyo vitahusu pia silaha.

Aidha wajumbe 15 wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa limeipongeza MONUSCO kwa namna ambavyo imekuwa ikitekeleza mamlaka yake na hususani ya kuwalinda raia na limeitaka na kuihimiza MONUSCO kuendelea na wajibu wake huo huku lilikisisitiza kwamba Baraza Kuu la Usalama halitavumilia kitendo chochote kinacholenga kudhoofisha mamlaka ya MONUSCO.

Vilevile Baraza limeitaka Expanded Joint Verification Mechanism ( EJVM) kuchunguza madai ya kuwapo kwa vitendo vya urushwaji wa makombora kuelekea nchi ya jirani ya Rwanda

Katika hatua nyingine , Muwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu katika DRC. Bw. Martin Koble naye ameelezea kusikitishwa kwake na tukio hilo la kuuawa kwa mlinzi wa Amani wa Tanzania.

Akielezea masikitiko yake, Bw. Martin Koble anasema, “ mlinzi huyo wa Amani ameyatoa muhanga maisha yake ili kuwalinda wananchi wa Goma. Ninaungana na familia ya marehemu na walinzi wenzake katika kombania yake katika kipindi hiki cha majonzi na wakati mgumu”.

Katika mwaka mmoja uliopita, kundi la waasi la M23 pamoja na makundi mengine yenye silaha mara kwa mara yamekuwa yakipambana na Jeshi la Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ( FARD). Ambapo Mwezi Novemba mwaka jana kundi hilo la M23 lilichukua kwa muda mji wa Goma.

Machi 28 mwaka huu , Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, lilipitisha azimio la kuanzishwa kwa Brigedi Maalum ( FIB) iliyopewa mamlaka ya kuyadhibiti makundi ya waasi yenye silaha yenyewe kama FIB na au kwa kushirikiana na Majeshi ya serikali ya DRC ( FARD).

Kupitia azimio hilo Baraza Kuu la Usalama lilitoa wito kwa kundi la M23 kusitisha mara moja aina zote za machafuko ikiwa ni pamoja na kuweka chini silaha zao.

Aidha kwa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa kuimarisha mamlaka ya MONUSCO pamoja na kuundwa kwa FIB kumelenga katika kusaidia utekelezaji wa malengo ya Mpango Mpana wa Kisiasa wa Umoja wa Mataifa kuhusu Amani, usalama na maendeleo katika DRC na eneo la Maziwa Makuu.

CALL FOR INTERVIEW OF MEDICAL DOCTORS AND ASSISTANT NURSING OFFICERS AT MUHIMBILI NATIONAL HOSPITAL

The following candidates are invited for oral interview which 
will be conducted at MNH as per the dates shown below:
MEDICAL OFFICERS II
03RD  SEPTEMBER, 2013, AT CPL MUSEUM, FROM 09.00 AM
SNO



1
MUGISHA N. NKORONKO
30
ELIKAANAN IOELIPOKEA URIO
2
NOEL D.SWAI
31
ZAHARA  MEGHJI
3
JOSEPH  EMMANUEL
32
JUDITH KIVUGO
4
MASAWA K. NYAMURYEKUNGE
33
OLIVA FABIAN ISENGWA
5
CHRISONGONE JUSTINE
34
JANET  KAPINGA
6
ROGERS SEMPINDU
35
AMOUR SULEIMAN MOHAMED
7
SAFIEL  META
36
EMMANUEL A. NHONOLI
8
ZENA MALEWA
37
SEBASTIAN  UVETIE
9
AMINA HAMAD HASSAN
38
ELISHA  O.OSATI
10
NAZARIUS  J.J  GECKE
39
NIMWINDAEL STEPHEN MSANGI
11
GERALD HARLES ROBI
40
LUCAS  JAMES  MAIGA
12
ATUGANILE  NALANGO
41
AMULO AMANDA  ANYOTI
13
PARVINA  KAZAHURA
42
ELIZABETH   SAWAKI
14
RACHEL  K .KATARAIA
43
STANLEY   AMOS
15
ADELINA G. RUTASHOBYA
44
PHILIP STEPHEN
16
BRIGHT  AWADH  SANGIWA
45
GETRUDE   FRANK   MWANG’AMBA
17
DAUDI  H. WAPALILA
46
LUGUGA  A.VEDASTUS
18
RAYA MUSA
47
MEZA WILFRED J.
19
SIA C. KIWIA
48
ALLEN ODEN  KITALU
20
JUDE   NICHOLAUS  TARIMO
49
SYLVIA BEDAS NSATO
21
CHANAI WEBESTER
50
CONSOLATHA  MBATINA
22
NKUBA GEORGE
51
VERIDIANA   BYEMELWA
23
FRANK ROBERT MAYAYA
52
FLORENCE   J. MTEI
24
KARUNGI KAROMA
53
JANETH KOMBA
25
BEN-YEDDY A.CHITAMA
54
ANTONY    G.KINGILO
26
JAMILA SHAMWETA
55
DANIEL  MKAMA  CHOCHOLE
27
HELLEN   MACHANGE
56
KATALYEBA  BENEDICT VITALIS
28
JOACHIM KILEMILE
57
ELITRUDA J. BURETA
29
FLORA NDOBHO
58
ONA ISAAC MACHANGU
04THSEPTEMBER,2013  AT CPL MUSEUM FROM 09.00 AM




1
HASSAN  RIZIKI
23
WINNIE  TEMU
2
AIKA  ABIA  SHOO
24
SEBASTIAN HONORAT  PIMA
3
VIVIAN  RUGARABAMU
25
FESTO  KASMIR
4
DANIEL  GEORGE
26
OCTAR  JAVETY
5
ABDULRAHAMAN  YUSUF
27
RASHID  ALLY
6
JOACHIM  ANGELO
28
ABDULHAMAN  AMIN
7
ARISTIDES  RAPHAEL
29
ANNASTAZIA  EMMANUEL KOMBA
8
ANNA FULGENCE  LEMUNGE
30
MARYAM  AMOUR
9
NEEMA  MOSHI
31
FRANCIS METHOD MWIMANZI
10
RAYMOND SAMUEL
32
DAUDI  HASSAN
11
HAMIS KINYERERO
33
MAGDALENA  F.DENNIS
12
JIMMY ERNEST
34
JASMIN  JUMA  K
13
JUMA  MBUGI
35
LUCAS  DAVID NGAMTWA
14
GEORGIA  M.KAMESE
36
CASTO ELINDA  MLAY
15
LUKAN SOLA MAKUBULA
37
BERTHA KOMBA
16
AGNES MOSES WARIOBA
38
MAIJO R BISEKO
17
JOHN  NKINDA
39
OMARI MSUMI
18
PAUL  MASUA
40
THEOFLO NAHUM MMBANDO
19
MASANJA  DOTO
41
WILLY  MAY SHOO
20
RAMADHAN  KABOTTA
42
SERAPHINE JAMARY  MROSSO
21
GOODLUCK  JOHN UROMI
43
LINDA  AUGUST
22
VICTORIA PAUL
44
REBECCA   KALIKAWE

05TH SEPTEMBER,2013 AT CPL MUSEUM, FROM 09.00 AM




1
OMBENI HARIELI  MSUYA
29
KURENJE  J MBURA
2
EVANCE GODFREY
30
GABRIEL WILFRED  MBWETE
3
ULIMBAKISYA KAINI
31
FADHIL KUMBAKUMBA
4
SARAH SHIRAZ
32
MUSTAFA KACHECHELE
5
REBECA Z.MAJIGE
33
BENEDICT  AUGUSTARD
6
DICKSON ATHANASIO
34
NEEMA  NALITOLELA
7
KENEDY DONALD
35
ALIA KARIM JIURAJ
8
KHADIJA JUMA
36
DIANA TUMAINI  FAINI
9
IKUPA MWASUMBI
37
BOSCO MAPUNDA
10
PETER MWANDINGA
38
GODBLESS  EXAUD MASSAWE
11
KOKUHABWA I.MUKURAS
39
FRANK M.SUDAI
12
JANE C. MASSAWE
40
VIVIENNE AIYANA  MLAWI
13
MAXIGAMA  Y  NDOSI
41
NGWILO MWAKYUSA
14
AGNESS F.SHAYO
42
ISAAC  MLAY
15
AARON NDIPO AARON
43
DEOGRATIUS MALLY
16
MOHAMED HARUN ULOTU
44
SHAZMEER RAMZAN
17
SMITHA  BHARIA
45
EMMANUEL MANYONYI
18
WILLYBROAD A. MASSAWE
46
JUSTINE ROBERT MWAIHOJO
19
STEPHEN S. NANDI
47
JUMA RAMADHNI
20
GUIDO I. LIBABA
48
MICHAEL  K KIREMEJI
21
ARAFAT KHALID
49
ATHUMANI MAMBO
22
DANIEL PAUL
50
WILHELLMUSS  MAUKA
23
GODFREY CHUWA
51
JUSTUS ISHENGOMA
24
JORAM MBAGA THEOBALD
52
LUKA MKENI
25
DESDERIUS  NDUNGURU
53
HANCE L. MPUMILWA
26
FROLIAN VEDASTO
54
BEATRICE P KISIMBO
27
SIGRID CYRIL LUCAS
55
ELISIA PHILIP  MPANGO
28
BRIAN ABRAHAM




         ASSISTANT NURSING OFFICER II
S/N
NAMES



DATE: 02/09/2013         VENUE: CPL MUSEUM, TIME: 09.00 AM
1.
NOEL E.  KALLINGA
18.
ATUKUMBUKE ULIMBOKA
2.
FELIX DOMINIC MLAY
19.
ZUHURA MUSSA
3.
SHEMU SAMSON CHUMA
20.
BEATRICE BEDDA
4.
BARBRA AKOTH OMONDI
21.
REGINA WITHBERTH
5.
MARTHA SOMI
22.
DEOGRASIA MWANYIKA
6.
WINFRIDA K. GULAKA
23.
MAGRETH N. MBARUKU
7.
MARIA FELIX MYULA
24.
FRANCIS M. BIGAMBO
8.
DORICA M. ALEX
25.
LUCY KIANDE
9.
ANGELLA  E. BANTEGA
26.
ROSEMARY G. MPELLA
10.
JANE BENITO MWAKITOSI
27.
JACKLINE URIO
11.
NUSURA HAJI MWANGA
28.
NEUSTER FESTOR
12.
MESHACK JOHN
29.
PHYLIS NYAMBURA GATUA
13.
JENIPHA ELIUD
30.
ELIFURA A.MBISE
14.
SECUNDA S. MBOYA
31.
SABITINA M. MZARA
15.
NEEMA J. BURETHA
32.
LUCIA A D. KABEYA
16.
GAUDENSIA J. KISAWE
33.
ZIADA JUMA JORAM
17.
RAJABU M. RAJABU
34
CHRISTOPHER ON’ENG’A


DATE: 03/09/2013         VENUE: CPL HALL TIME: 09.00 AM

35.
EVETH M. SANGAWE
56.
NGASSA J. MASOLWA
36.
METHOD LIBERI LUSAMBO
57.
SCOLASTICA L. CHUNDU
37.
VERONICA VEDASTUS
58.
ANNA  VICTOR NGWADA
38.
MAINDA HAJI HAMIS
59.
HAPPINESS P. MURAGWA
39.
GETUMA T. CHACHA
60.
NEEMA YEREMIA NG’ADI
40.
SARAH MLWILO
61.
MARIAM GEORGE
41.
ZAINA A. MRINGO
62
 ELIZABETH E. NYUNGANI
42.
IKWABE W. MWITA
63.
BEBICHA G. MHAGAMA
43.
DAVID DANIEL MISIWA
64.
AGNESS J. LUGENDO
44.
GRACE GEORGE
65.
HAPPY E. SANGA

45.
JAMIRU JAPHARY
66.
ANNA S. LYIMO
46.
IBRAHIM T. MODAHA
67.
ZUBEDA AMIR
47.
SHAALI  IDD
DATE: 04/09/2013              VENUE: CPL HALL, TIME: 09.00 AM
48.
RACHEL V. MRONDOR
68.
UPENDO S. SUMARI
49.
AYOUB A. MCHAU
69.
STELLA O. MWAPINGA
50.
NOMENCIA THOMAS
70.
NAVONEIWA PRAYGOD
51.
JULIETH KALAO
71.
JOSYLINE OSANO
52.
ROBERT MBULA
72.
EVANGELINA N. MUTAYOMBWA
53.
MALI JOSEPH SABUNI
73.
HARRIET MORAM NABISWA
54.
AISHA AHMED OMARY
74.
MBOYA B. ACHIENG
55.
AGNESS SALMON KAJANGWA
75.
MUGULI KENETH
DATE: 04/09/2013         VENUE: CPL HALL, TIME: 09.00 AM
76.
SIFA S. BAKARI
91.
JANITH BRYSON MDACHI
77.
PHILIPIRIA MKWIZU
92.
AISHA BAKARI PANDE
78.
MAGRETH G. GERAZIUS
93.
IRENE MATHIAS MDEE
    79
JENIPHER M. MOSHI
94.
REBECCA LUCAS KISUSI
80.
RITHA SIMON
95.
LIZZYBETH A. MALEWO
81.
ZAINAB NASSORO MOHAMED
96.
EVA DAMIAN LYOCHI
82.
ELIZABETH S. KABOMA
97.
YUSUFU M. MOHAMED
83.
RESPICIA KATESIGWA
98.
MARY P. MKWAVI
84.
NADHARA HAJI GOLO
99.
ZENNAIS Y. NGOWI
85.
NANCY OLAMBO
100.
MARTHA TALUKA
86.
EDWIN ALOYCE
101.
ANNASTAZIA K. SAMWEL
87
KAWAMBWA MOHAMED
102.
FURAHINI Y. CHANYEGELA
88.
HAPPINESS MILLINGA
103.
JOSEPH JONSON JARRIES
89.
MAGDALENA M. MANDE
104.
SOPHIA MAKUNDI
90.
MWARAMI J. BUMBO



 IMPORTANT NOTE:

  • Interview will be conducted at  Muhimbili National Hospital Dar es Salaam as indicated above
  • Each applicant should observe time
  • All interviewees should bring their original Certificates
  • Employees who are required by their professional Boards to be registered or licensed should bring their registration Certificate or licenses.
  • For more information during arrival, please call mobile phone No. 0717 109 388 & 0753 099 330
 EXECUTIVE DIRECTOR,
MUHIMBILI NATIONAL HOSPITAL,
P.O.BOX 65000,
DAR ES SALAAM.