Sunday, December 30, 2012

Balozi Sefue ahimiza ushiriki wa Smart Partnership Dialogue


Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (kulia) akijadiliana jambo kuhusiana na mkutano mkubwa wa kimataifa wa ushirikiano kwa manufaa ya wote, Smart Partnership Dialogue ‘Global 2013’, unaotarajiwa kufanyika hapa nchini mwezi Mei mwaka 2013 alipokua akiongea na wanahabari jijini la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, (katikati) ni Kaimu katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC), Bw. Samson Chemponda na kushoto ni Meneja Mradi wa Smart Partnership Dialogue ‘Global 2013,’ Rosemary Jairo.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (kulia) akijadiliana jambo kuhusiana na mkutano mkubwa wa kimataifa wa ushirikiano kwa manufaa ya wote, Smart Partnership Dialogue ‘Global 2013’, unaotarajiwa kufanyika hapa nchini mwezi Mei mwaka 2013 alipokua akiongea na wanahabari jijini la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, (katikati) ni Kaimu katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC), Bw. Samson Chemponda na kushoto ni Meneja Mradi wa Smart Partnership Dialogue ‘Global 2013,’ Rosemary Jairo.

Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam

Viongozi katika ngazi mbalimbali Tanzania wamepewa changamoto kutoa umuhimu mkubwa na kushiriki kikamilifu katika majadiliano ya ushirikiano kwa manufaa ya wote (Smart Partnership Dialogue) ili kuchochea haraka maendeleo katika nchi.

Wito huu umetolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alipokua akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na matayarisho ya mikutano ya kitaifa na ule wa kimataifa kuhusiana na majadiliano hayo hapa nchini.

“Ningewataka viongozi nao watoe umuhimu mkubwa kwenye jambo hili kwa sababu watanufaika sana kupata mawazo mbalimbali ya wananchi,” alisema Balozi Sefue mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa viongozi washiriki katika majadiliano katika ngazi zote kitaifa na pia wajiandae na majadiliano ya kimataifa.

Haya ni majadiliano yanayolenga kutoa fursa kwa jamii kukaa pamoja na kuzungumzia maswala mbalimbali ya maendeleo.

Kwa hapa Tanzania, chombo kitakachosimamia na kuratibu majadiliano haya kitaifa ni Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) wakati Wizara ya Mambo ya Nje ina jukumu la kuratibu mkutano wa kimataifa kuhusu majadiliano hayo hapa nchini mwezi Mei, 2013.

Mchakato wa majadiliano haya ulishazinduliwa na Rais Jakaya Kikwete tangu Mei, 2012.

Balozi Sefue ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya TNBC alisema kwamba kila mtanzania ajitahidi kuelewa dhana hii kwa kusoma na kusikiliza vyombo vya habari kwa sababu ni fursa nzuri kwa kila mwananchi kushiriki katika maendeleo ya nchi na namna tunavyoweza kufikia maendeleo ya haraka.

“Hakuna mwenye ukiritimba wa mawazo kwa hiyo tunahitaji mawazo ya kila mwananchi na hivyo kila mtu ajione kuwa ana wajibu wa kuchangia maana faida itakua kwa kila mmoja na nchi kwa ujumla,” alisema.

Alisema dhana hii ya majadiliano kwa manufaa ya wote ni muhimu sana hasa kwa viongozi kwa kuwa kadiri kiongozi anavyopata maoni ya watu wengi zaidi, ndio maamuzi yake yatakavyokua sahihi zaidi na yatazingatia mahitaji ya makundi mbalimbali katika jamii.

“Kwa mfano, maamuzi ya serikali yatakubalika kwa urahisi zaidi na wananchi kwa sababu watakua wameshiriki katika kuyaandaa,” alisema.

Akielezea zaidi alisema kujenga nchi kunahitaji makundi yote kwa hiyo ni vyema watu wakipata fursa nyingine kukakaa pamoja na kujadili mambo ya msingi ya maendeleo.

Alisema majadiliano kama haya ni fursa nyingine ya kushirikisha wananchi na wadau wengine katika kuhakikisha kuwa mipango katika kutekeleza Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 inazingatia maoni na inakua na faida kwa kila kundi katika jamii.

Mkutano wa mwezi Mei, 2013 ni mwendelezo wa mikutano kama hii ambayo imeanza kiasi cha miaka kumi na tano iliyopita na ikianzishwa na Jumuia ya Madola kupitia taasisi yake inayoitwa Commonwealth Partnership for Technology Management na kwa ushiriki mkubwa wa aliyekuwa waziri Mkuu wa Malaysia, Dkt. Mahathir Mohammed.

Tayari TNBC imeshaanza kuendesha semina za uhamasishaji zenye lengo la kutoa ufahamu kuhusu majadliliano ya kitaifa kabla ya yale ya kimataifa.

Kitaifa, majadiliano haya yatahusisha makundi mbalimbali yakihusisha serikali, wanasiasa, wafanyabiashara, wasomi,wafanyakazi, vijana, wasanii na wakulima ambao watakaa pamoja na kujadili maswala mbalimbali yanayohusu biashara na maendeleo.

Makundi haya yatapata fursa hiyo kupitia mabaraza ya mikoa na yale ya wilaya ya TNBC ambako madajiliano hayo yatafanyika kuanzia huko hadi ngazi za kitaifa kabla ya majadiliano ya kimataifa mwezi Mei.

Makundi yote yatapata fursa ya kujadili na kutoa mapendekezo yao.

Thursday, December 27, 2012

TAARIFA KWA UMMA JUU YA MAAMUZI YA BARAZA LA MADAKTARI KUHUSU MADAKTARI WALIOGOMA



UTANGULIZI
Kutokana na mgomo wa madaktari uliotokea kati ya tarehe 23 na 29 mwezi juni 2012.Wizara iliwasilisha malalamiko kwenye Baraza la madaktari Tanganyika ili lifanye uchunguzi kuhusu madaktari hao .Idadi ya madaktari wote waliogoma walikuwa 394, kati yao madaktari 376 walikuwa ni madaktari walio katika mafunzo kwa vitendo (Interns) kutoka hospitali za Muhimbili, K.C.M.C. Bugando, Mbeya Rufaa, St.Francis - Ifakara, Dodoma, Temeke, Mwananyamala, Amana, Haydom na Sekou Toure. Aidha, Madaktari waajiriwa(Registrar) 18 walishiriki katika mgomo huo kutoka hospitali ya Rufaa ya Mbeya.
Baraza lilipitia malalamiko yote na limetoa adhabu stahiki kwa kila daktari aliyethibitishwa kushiriki katika mgomo huo.  Adhabu hizo zilikuwa katika makundi yafuatayo; onyo, onyo kali na kusimamishwa udaktari kwa muda wa kati ya mwezi mmoja na miezi sita.Vile vile kuna Madaktari ambao hawakuwa na hatia ya kushiriki katika mgomo na hivyo walifutiwa mashtaka.
MCHANGANUO WA ADHABU
  • Waliofutiwa mashitaka madaktari 49
  • Waliopewa onyo  madaktari 223
  • Waliopewa onyo kali madaktari 66
  • Kusimamishwa kwa muda madaktari 30
  • Mashitaka yaliyoahirishwa kutokana na wahusika kuhitaji ushauri wa kisheria madaktari 4
  • Mashitaka yasiyosikilizwa kutokana na wahusika kutofika walipoitwa na Baraza madaktari 22
Wizara inakamilisha taratibu za kinidhamu kwa mujibu wa Kanuni za Utumishi wa Umma kwa Madaktari wote waajiriwa ambao walipatikana na hatia mbele ya Baraza la Madaktari.   Wizara pia imeridhia kuwapa Madaktari waliokuwa katika mafunzo kwa vitendo fursa nyingine ya kuendelea na mafunzo hayo katika hospitali za Umma walizokuwepo kabla ya kuondolewa.  Hata hivyo fursa hii haitawahusu Madaktari wote waliopewa adhabu za kusimamishwa na Baraza la Madaktari, hadi hapo watakapomaliza kutumikia adhabu zao.
HITIMISHO
Kwa taarifa hii madaktari wote waliofutiwa mashtaka na wale waliopewa onyo na onyo kali wanatakiwa kuwasilisha kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii barua kutoka kwa msajili wa Baraza la Madaktari ikithibitisha kurejeshewa usajili  na kuruhusiwa kuendelea na mafunzo kwa vitendo. Vile vile madaktari waajiriwa(Registrar) wanatakiwa pia kuripoti kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya ili kupewa barua zao kulingana na Adhabu walizopewa.  Barua hizi zitatolewa  kuanzia tarehe 2 Januari, 2013.Madaktari wote walio katika mafunzo kwa vitendo wanatakiwa kuanza kazi katika vituo vyao vya awali  ifikapo tarehe 14 Januari, 2013.Hakuna muda utakaoongezwa kwa kipindi kilichobakia cha mafunzo kwa vitendo. Kwa wale wote waliopewa adhabu wataanza kutumikia adhabu hizo kuanzia tarehe ya adhabu hiyo ilivyotolewa.

Nsachris Mwamwaja
Msemaji
WIZARA YA AFYA NA USTAWI  WA JAMII
27/12/2012

Vodacom yaupa nguvu Mradi wa Mbwa Mwitu

Rais Jakaya Kikwete akionesha mbwa mwitu(hawapo pichani) wanavyorejea katika hifadhi ya Serengeti mara baada ya kuachiwa kutoka katika banda maalum walilokuwa wamehifadhiwa ikiwa ni awamu ya pili ya kundi la mbwa hao chini ya Mradi wa Uhifadhi na Ulinzi wa wanyama hao walio katika hatari ya kutoweka. Vodacom Foundation hadi sasa imeshatumia zaidi ya Sh 450 Milioni kufadhili mradi huo kama sehemu ya kuchangia maendeleo ya sekta ya Utalii nchini. Kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Tifa - TANAPA Allan Kijazi, Meneja wa Mahusiano ya Nje wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim na Meneja wa Vodacom Foundation Grace Lyon. 
Rais Jakaya Kiwete Kikwete akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani)katika eneo la Nyamuma ndani ya hifadhi ya taifa ya Serengeti mara baada ya kuongoza zoezi la kuwaruhusu mbwa mwitu kumi na watano kurejea hifadhini baada ya kuwa chini ya uangalizi maalum kupitia mradi wa Uhifadhi na Ulinzi wa Wanyama hao walio katika hatari ya kutoweka. Vodacom Foundation hadi sasa imeshatumia zaidi ya Sh 450 Milioni kufadhili mradi huo kama sehemu ya kuchangia maendeleo ya sekta ya Utalii nchini.

Kampuni ya Vodacom imesema itaendelea kutoa ushirikiano katika juhudi mbalimbali zinazochukuliwa na serikali katika miradi inayolenga kuchochea kasi ya maendeleo ya nchi na wananchi wake.

Hayo yamesemwa na Meneja Mahusiano ya Nje wa Kampuni hiyo Salum Mwalim wakati wa zoezi la kuwaachia kundi la pili la Mbwa Mwitu kumi na tano katika eneo la Nyamuma ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mwishoni mwa wiki.

Mbwa hao walikuwa chini ya uangalizi maalum wa mradi wa Uhifadhi na Ulinzi wa Wanyama hao ambao wapo katika hatari ya kutoweka katika hifadhi hiyo tangu mwanzoni mwa miaka ya tisini kutokana na sababu mbalimbali.

“Kampuni ya Vodacom imekuwa ikiunga mkono juhudi mbalimbali za kimaendeleo kupitia uwajibikaji kwa Jamii – CSR chini ya mfuko wake wa kusaidia Jamii - Vodacom Foundation na kwamba inaunga mkono juhudi zote zinazochukuliwa katika kuchochea maendeleo ya nchi na wananchi.”Alisema Mwalim.

Akizungumzia mradi huo wa Mbwa Mwitu Mwalim amesema Vodacom imeshatumia zaidi ya Sh. 450 Milioni kufadhili mradi huo tangu mwaka 2010 kwa kutambua umuhimu na mchango wa sekta ya Utalii hapa nchini.

“Vodacom imekuwa mfadhili mkuu wa meradi huu tangu ulipoanzishwa na inafanya hivyo kutokana na umuhimu wa Hifadhi ya Serengeti katika sekta ya Utalii na mchango wake katika maendeleo ya nchi hii.”Alisema Mwalim.

“Tunapoowaangalia wanyama hawa tunaweza tusione jambo muhimu ndani yake lakini kwa kuangalia umuhimu wa sekta ya Utalii na mchango wake katika pato la taifa kwa wakati huu ni wazi kwamba kila jambo linaloongeza thamani ya hifadhi zetu ni la msingi kwa mustakabali wa uchumi wa nchi yetu.”Aliongeza Mwalim wakati akizungumza katika hafla hiyo iliyoongozwa na Rais Jakaya Kikwete.

Mbali na ufadhili wa fedha, teknolojia ya mtandao wa Vodacom ndio inayotumika kufuatilia maisha ya wanyama hao mara baada ya kuachiwa huru kupitia vifaa maalum wanavyofungwa mbwa hao kuwezesha kazi ya ufuatailiaji kwa njia ya Satelite.

“Tumewezesha teknolojia ya simu ya mtandao wa Vodacom pia kutumika kuwezesha ufuatiliaji wa maisha ya mbwa hawa mara baada ya kuachiwa huru ili kutopoteza rekodi za maedneleo yao hifadhini.”Alisema Mwalim.

Lengo la mradi wa uhifadhi Mbwa Mwitu ni kurejesha viumbe hao katika hali yake ya kawaida katika hifadhi ya Serengeti baada ya kutoweka mwanzoni mwa miaka ya tisini.

Chini ya mradi huo viumbe hao hushikwa na kutunzwa ndani ya boma maalum ili kuwawezesha kuzaliana na hatimae huachiwa huru kuendeleza maisha asilia katika hifadhi ya Serengeti. Lengo ni kufikisha idadi ya Mbwa Mwitu sitini ambao kuanzia hapo watakuwa na uwezo wa kuendeleza vizazi ndani ya hifadhi hiyo.

Kwa mujibu wa mratibu wa mradi huo Emmanuel Massenga Hifadhi ya taifa ya Serengeti inakadiriwa iliwahi kuwa na zaidi ya mbwa mwitu mia tano kabla ya kuanza kutoweka hadi kufikia hatari ya kutoweka kabisa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo magonjwa na kuuawa na wananchi.

Jumla ya Mbwa Mwitu Kumi na mmoja waliachiwa Agosti mwaka huu chini ya mradi huo na hivyo kufanya idadi ya mbwa mwitu hao ndani ya hifadhi ya Serengeti kwa sasa kufikia ishirini na sita.

Zoezi la kuachiwa huru kwa kundi la pili la mbwa mwitu hao liliongozwa na Rais Jakaya Kikiwete ambapo ametaka kujitokeza kwa wadau zaidi kusaidia mradi huo.

Mambo yanavyotabiriwa kuwa wakati wa usajili wa dirisha dogo ligi kuu ya Uingereza


Arsenal

TARGETS: Wilfried Zaha (C Palace), Demba Ba (Newcastle), Nani (Man Utd).
BUDGET: £30million CHANCES: High. Arsenal are desperate for a striker and all are possible signings — if Arsene Wenger is prepared to fork out the asking price.

Aston Villa

TARGETS: Luke Murphy (Crewe), John Guidetti (Man City), Glenn Murray (Palace), James Henry (Millwall).
BUDGET: £5million CHANCES: Slim to none, though Paul Lambert’s budget could change if Darren Bent is sold.

Chelsea

TARGETS: Andre Schurrle (B Leverkusen), Radamel Falcao (Atletico Madrid), Paulinho (Corinthians), Joao Moutinho (Porto).
BUDGET: £75million CHANCES: Falcao will cost £50m and a central midfielder is needed if Frank Lampard leaves.

Everton

TARGETS: Jack Butland (Birmingham), Vegard Forren (Molde).
BUDGET: £6million CHANCES: David Moyes has such a tight budget he is likely to end up with just loan players. Old boys Tim Cahill and Landon Donovan are possible.

Fulham

TARGETS: Vegard Forren (Molde), Darren Bent (Aston Villa), BUDGET: £10million CHANCES: It’s 50-50. Martin Jol could be tempted to strengthen. Might go for Bent if he becomes available at a decent price.

Liverpool

TARGETS: Daniel Sturridge (Chelsea), Thomas Ince (Blackpool), Burak Yilmaz (Galatasaray). BUDGET: £28million CHANCES: Good. Sturridge is effectively a done deal, while late competition for Ince is unlikely to sway him away from an Anfield return.

Man City

TARGETS: Alen Halilovic (Dynamo Kiev), Paulinho (Corinthians) Daniele de Rossi (Roma), Fernando Llorente (A Bilbao).
BUDGET: Unlimited CHANCES: City have no plans to spend big in January, unless they have an injury crisis or a huge offer for Mario Balotelli.

Man Utd

TARGETS: Theo Walcott (Arsenal), Victor Wanyama (Celtic), Alen Halilovic (D Kiev), Robert Lewandowski (B Dortmund) Ezequiel Garay (Benfica).
BUDGET: £20million CHANCES: Very slim. Alex Ferguson has said he will ‘definitely not’ be signing anyone in January.

Newcastle

TARGETS: Tom Ince (Blackpool), Loic Remy (Marseille), Mathieu Debuchy (Lille) Douglas (Twente).
BUDGET: £15million CHANCES: Fairly low. Remy is in demand along with Ince and Debuchy. Brazilian defender Douglas could be a goer.

Norwich

TARGETS: Danny Graham (Swansea), Cameron Jerome (Stoke), Matt Phillips (Blackpool).
BUDGET: £5million CHANCES: Good. Norwich are having a storming season and have identified some sensible targets. Boss Chris Hughton insists no one will be leaving.

QPR

TARGETS: Michael Dawson, Scott Parker (both Spurs), Nicolas Anelka (Shanghai Shenhua), Joe Cole (Liverpool).
BUDGET: £13million CHANCES: Have every chance of getting Cole on loan but Spurs have told them to forget about Dawson and Parker.

Reading

TARGETS: Lee Camp (N Forest), Paul Robinson (Blackburn). Roman Pavlyuchenko (Lokomotiv Moscow).
BUDGET: £5-£10million CHANCES: Unknown. The Royals are in desperate need of some new recruits if they are serious about beating relegation.

Southampton

TARGETS: Abdul Kader Keita (free), Scott Dann (Blackburn), Matt Besler (Kansas City).
BUDGET: £5million CHANCES: Good. There should be some money available to boss Nigel Adkins, who needs to boost his defensive options.

Stoke

TARGETS: Danny Simpson (Newcastle), Chung-Yong Lee (Bolton), Marko Marin (Chelsea), Atiba Hutchinson (PSV), Martin Olsson (Blackburn).
BUDGET: £2-£3million CHANCES: Low. Tony Pulis needs to move players out if he wants to raise transfer funds.

Sunderland

TARGETS: Danny Rose (Spurs), Gary Hooper (Celtic), Danny Graham (Swansea) BUDGET: £8million CHANCES: Fair. Sunderland have a good chance of signing Rose on a permanent deal from Spurs. Boss Martin O’Neill could be tempted to add another striker.

Swansea

TARGETS: Christophe Berra (Wolves), Ryan Fraser (Aberdeen), BUDGET: £4million CHANCES: Excellent. If Swans keep targets realistic, then boss Michael Laudrup has every chances of signing them. Has already proved a good operator in the transfer window with Michu capture.

Spurs

TARGETS: Joao Moutinho (Porto), Christian Eriksen (Ajax).
BUDGET: £25million CHANCES: Spurs almost signed Portuguese playmaker Moutinho in the last window and chairman Daniel Levy could be tempted to resurrect that deal to boost the North Londoners’ top-four hopes.

West Brom

TARGETS: No names on the radar until next summer.
BUDGET: £0 unless there is an emergency.
CHANCES: No chance. Boss Steve Clarke has made it clear Albion are unlikely to buy next month, although loan signings are a possibility if needed. That is despite Baggies’ recent loss of form.

West Ham

TARGETS: Darren Bent (Aston Villa), Faouzi Ghoulam (St Etienne), Joe Cole (Liverpool) Andreas Cornelius (FC Copenhagen), BUDGET: £10million CHANCES: Good. Boss Sam Allardyce has been linked with several players but his priority will be keeping hold of Mohamed Diame.

Wigan

TARGETS: Roger Espinoza (Sporting Kansas City), Ryan Fraser (Aberdeen), Christophe Berra (Wolves).
BUDGET: £4million CHANCES: Excellent. A deal for Espinoza looks nailed on after he was granted a work permit while Fraser and Berra are realistic targets. Defenders are a priority for Latics.

SIKU YA WACHAGA YAFANA SANA MJINI MOSHI

Tamasha kubwa la kihistoria lililopewa jina la Chagga Day Cultural Festival 2012 - Moshi lilifanyika kwenye ukumbi wa ZUMBA LAND katika manispaa ya Moshi siku ya Jumamosi tarehe 22/12/2012 kuanzia saa sita mchana mpaka saa sita usiku na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa mji huo huku baadhi wakioongozana na familia zao.

Tamasha hilo lililotawaliwa na shangwe za mara kwa mara kutoka kwa wakazi wa mji wa Moshi waliofurika kwenye viwanja hivyo maarufu kwa michezo ya watoto, liliandaliwa na kampuni ya Myway Entertainment ya jijini Dar chini ya Mkurugenzi wake Paul Mganga na kudhaminiwa na kampuni ya bia (TBL) kupitia bia ya Safari Lager na kampuni ya vinywaji baridi (SBC) kupitia kinywaji chake murua cha Pepsi.

Katika shoo hiyo iliyoacha gumzo lisilokwisha kwa wakazi mjini Moshi na vitongoji vyake, kulikuwa na mambo mengi yahusuyo kabila hili maarufu ambapo historia halisi ya kabila na asili yake ilisomwa jukwaani na Mkurugenzi wa kituo binafsi cha makumbusho cha Uhuru Museum.

Tukio hilo lilikwenda sambamba na maonesho ya zana na nyenzo mbalimbali zilizokuwa zikitumiwa na wazee wa zamani wa kichagga katika kilimo, uvunaji, uandaaji vyakula, utunzaji, upishi, uhunzi, ulinzi nk huku mamia ya watu waliohudhuria walionesha kuvutiwa sana nazo na wengine wakipiga picha kwa ajili ya kumbukumbu zao.

Burudani katika shoo hiyo zilikuwa bendi ya muziki wa dansi ya Serengeti yenye maskani yake jijini Arusha, kundi la wanenguaji (dancers) wanaojiita Boda 2 Boda pia toka Arusha. Sambamba nao aliyefunga pazia la burudani alikuwa mwanamuziki wa Bongo Flava Ommy Dimpoz ambaye ali[pagawisha sana kwa nyimbo zake za Naynay, Baadae na Me & You.

Mratibu wa shoo hiyo, Paul Mganga akiongozana na Meneja wake Kaka Mwinyi, walisema kuwa, wameshukuru Mungu kwa kufanikisha onesho hilo ambalo awali lilifanyika kwa mafanikio jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Leaders, Kinondoni miezi miwili iliyopita ambapo kama ilivyokuw Moshi, tamasha la Leaders liliburudishwa na bendi za African Stars 'Twanga Pepeta' na Msondo Ngoma.

"Hatuna cha kuongeza kwa maelezo, karibu kila kitu kimejionesha wazi... shoo imefana, watu wengi wamejitokeza, wamefurahia na familia zao kuanzia vyakula, mambo ya asili na utamaduni, muziki wa dansi, shoo za madansa, muziki wa Bongo Flava nk. Kwa ujumla timu nzima ya Myway Entertainment inawashukuru wakazi wa Moshi kwa kulipokea vizuri tamasha letu," akasema Kaka Mwinyi.

Akizungumzia mipango ya baadaye ya kampuni yake, Paul Mganga alisema kuwa, kutakuwa na mfululizo wa matamasha ya makabila mbalimbali ya Tanzania ambapo yatakayofuata ni ya kihaya, kisukuma, kinyakyusa, kingoni, kigogo, kihehe, kimakonde nk kwa lengo la kuyafikia makabila yote na kuwakutanisha wenye asili yao waburudike, waelimike na kubadilishana mawazo na mipango ya maendeleo.

mtoto akichorwa katika mashamsham ya chagga day ukumbini Zumba Land.
mkurugenzi uhuru museum akitoa historia ya kabila la wachagga.
chagga day ilivyopambwa ndani ya zumbaland mjini moshi.
boda 2 boda wakiwajibika jukwani shoo ya chagga day moshi ndani ya zumbaland.
ommy dimpoz akiimba na washabiki chagga day moshi.
ommy dimpoz akimuimbisha mtoto shoo ya chagga day ndani ya zumbaland.
thecla mgaya 'aisha' wa mambo hayo alikuwemo ndani ay nyumba akifurahia chagga day pale zumbaland moshi.
palipendezaje hapo zumbaland shoo ya chagga day.
washabiki wakiburudika na vinywaji huku wakifuatilia shoo za chagga day jukwaani pale zumbaland moshi.
akinadada hawa walikuwepo chagga day moshi.
binti huyu akikwea puto katika ukumbi wa zumbaland katika shoo ya chagga day mjini moshi.
watoto wakiinjoi kwa treni za umeme shoo ya chagga day moshi.
mfano wa santa claus akiwafurahisha watoto katika ukumbi wa zumbaland siku ya chagga day ikiwa ni maandalizi ya sikukuu ya kris
santa claus huyu alikuwepo chagga day.
zana na vifaa vya kihistoria vya wachagga vilioneshwa na uhuru museum ya moshi ndani ya chagga day moshi.

Wednesday, December 26, 2012

DIAMOND, DIMPOZ WAFANYA KUFURU USIKU WA X-MAS DAR LIVE

...Chezea Diamond wewe!
Watu weweee: Kila mmoja akiwa na shauku ya kumpa mkono Diamond.
...Leka dutigite: Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na Diamond wakiwapagawisha mashabiki kwa wimbo wa Leka dutigite.
Ommy Dimpoz 'on da stage'!
Dimpoz na wasanii wake wakiwasha moto kuwakumbuka wapendwa wao waliotangulia mbele ya haki.
...Dimpooo...zzz: Umati ukipiga yowe wakati Ommy Dimpoz akifanya kufuru stejini.
...Platnumz hewani: Diamond akiwa amebebwa juu na madansa wake.
...Nataka kulewa, zikinipanda nimwage radhi.
...Nataka kulewa, lewa...: Diamond akiimba wimbo wake wa Nataka Kulewa.
...Nature ua... Nature ua... Nature ua..: Ndivyo Juma Nature alivyokuwa akienda sambamba kwa staili hiyo na mashabiki.
...Wanaume Halisi wakiendeleza libeneke ndani ya Dar Live.
Mtangazaji wa MTV Base na Choice FM, Vanessa Mdee akichombezana na Ommy Dimpoz wakati wakiimba wimbo wao wa Me & You stejini.
KR Muller akigonga mvinyo ndani ya mask.
...Zitto kazini: Siyo siasa tu, hata mistari mi mkali.
Kikosi cha Diamond Platnumz kazini.
Dimpoz na Vanessa wakipagawisha katika jukwaa la kupanda na kushuka ndani ya Dar Live.
Manjonjo ya madansa wa Dimpoz.
Diamond akiwachizisha mashabiki.
Madansa wa Dimpoz wakionyesha umahiri wao.
...Wakizidi kukonga nyoyo za mashabiki.
Zitto Kabwe akicheza kwenye kiti baada ya kunogeshwa na swagga za Dar Live.
Platnumz na dansa wake kama 'The Wacko Jacko'.
Shughuli pevu ya Diamond na madansa wake.
...Waacheni watoto waje kwangu: Ndivyo allivyokuwa akichombeza Diamond wakati akitaka kumchukua mtoto huyu.
Platnumz akiipagawisha meza ya wageni waalikwa.
Waalikwa wakionyesha nyuso za tabasamu wakiongozwa na Mwasiti (wa pili kulia) na Prodyuza aliyetengeneza wimbo wa Leka dutigite, Tudi (wa tatu kushoto).
Prodyuza na Mwanamuziki mkongwe, Ally Mohammed 'Baucha' akikamua stejini.
...Nimpende naniii... Nimpende...: Wapambe "Wemaaaaaaaaaaaaa!"
Madansa wa Extra Bongo wakinogesha zaidi burudani za X-Mas ndani ya Dar Live.
Mpiga gitaa la besi wa Extra Bongo, Hosea Mgoachi akijiachia na shabiki jukwaani.
Pozi la Platnumz.
---
Wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya nchini Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' na Omary Nyembo 'Ommy Dimpoz' usiku wa kuamkia leo wameweka historia kwa kufanya shoo ya aina yake ndani ya ukumbi wa kisasa wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam. 

Wasanii hao walisindikizwa na mkali Juma Nature na kundi lake la Wanaume Halisi, Msanii mkongwe Ally Baucha pamoja na Bendi ya Extra Bongo. Shoo hii imeletwa kwenu kwa hisani kubwa ya Serengeti Premium Lager na Vodacom - Wajanja wa Kujirusha.

(PICHA ZOTE : RICHARD BUKOS NA ISSA MNALLY / GPL)