Tuesday, January 31, 2012

TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA

(TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES – TCU)

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UENDESHWAJI WA UDAHILI - ELIMU YA JUU KWA MWAKA WA MASOMO 2012/2013

UTANGULIZI

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (‘Tanzania Commission for Universities’-TCU) ikishirikiana na Baraza laTaifa la Elimu ya Ufundi (‘National Council for Technical Education’ - NACTE) pamoja na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi Elimu ya Juu (Higher Education Students Loans Board) inapenda kuutarifu umma kuhusu utaratibu wa kujiunga na vyuo vya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2012/2013 kupitia mifumo ya “Pre-entry”, “Mature Age Entry”, “Equivalent Qualifications” na mfumo wa pamoja wa udahili (‘Central Admission System’) na utaratibu wa mikopo kama ifuatavyo:

MFUMO WA UDAHILI KUANZIA MWAKA 2012/13
1.1 Utaratibu wa Kuendesha Program za “Pre-entry” na “Mature Age Entry”

Kuanzia mwaka huu 2012, vyuo vyote vitakavyotaka kuendesha mafunzo ya awali kabla ya mwombaji kustahili kudahiliwa ili kuweza kujiunga na programu za elimu ya juu (pre-entry programmes) pamoja na kuendesha mitihani ya kupitia mfumo wa “Mature Age Entry” vinatakiwa kuwasilisha programu hizo Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) au Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) kwa uhakiki na kupata kibali. Programu hizo ni lazima ziendeshwe kwa muda wa mwaka mmoja. Hali kadhalika kwa upande wa mitihani kupitia mfumo wa mature entry, Tume kwa ushirikiano na Baraza, kwa pamoja wataandaa na kuratibu utaratibu wa mitihani katika vituo maalum kikanda ili vyeti vitakavyotolewa viwe na ulinganifu unaostahili na hatimaye kuweza kutumika katika udahili wa sifa linganishi katika vyuo mbalimbali.

Vyuo vinatakiwa kuandaa programu za mifumo ya “Pre-entry” na “Mature Age Entry” na kuziwasilisha Tume na Baraza ili zihakikiwe kwani mwaka wa masomo kwa kusudi hili utaanza mwezi Agosti 2012/2013. Kwa utaratibu huu, watakaofanya mafunzo hayo watatakiwa kufanya mitihani yao na kujiunga na masomo ya elimu ya juu katika mwaka wa masomo 2013/2014.

Kwa taarifa hii, mwaka 2012/13 hakutakuwapo na udahili wa wanafunzi kwa mfumo wa “Pre-Entry” na “Mature Age Entry”.

1.2 Utaratibu wa Udahili Kupitia Mfumo wa Pamoja (Central Admission System)

Waombaji watakaopitia mfumo wa pamoja wa udahili (CAS) wamegawanyika katika makundi manne, ambapo waombaji wa kundi (i), (ii) na (iii) watatambuliwa kama “Direct Applicants” na kundi (iv) watatambuliwa kama “Indirect Applicants”

Waliohitimu elimu ya sekondari kidato cha sita katika kipindi cha miaka miwili iliyopita pamoja na wale watakaohitimu mwaka huu.
Waliohitimu mafunzo ya diploma ya elimu ya ufundi (NTA level 6) kutoka vyuo vinavyotambulika na NACTE miaka miwili iliyopita pamoja na wale watakaohitimu mwaka huu;
Waliohitimu mafunzo ya Diploma ya Ualimu (kutoka vyuo vinavyotambulika) katika kipindi cha miaka miwili iliyopita pamoja na wale watakaohitimu mwaka huu.
Waombaji ambao sio wa moja kwa moja (Indirect Applicants) ni wote waliohitimu kidato cha sita, Diploma ya Elimu ya Ufundi (NTA level 6) na Diploma ya Ualimu katika kipindi cha zaidi ya miaka miwili iliyopita (kuanzia 2009 kurudi nyuma).
1.2 Waombaji Watakaowasilisha Maombi yao Moja kwa Moja Vyuoni

Waombaji watakaowasilisha maombi kupitia vyuo husika ni wenye sifa linganishi (Equivalent Qualifications) yaani wenye vyeti vya Astashahada na Diploma ambazo hazitambuliwi moja kwa moja na NACTE. Ili kukamilisha udahili, wanashauriwa kuwasiliana na NACTE ili vyeti vyao vitambuliwe na kusajiliwa kabla udahili haujaanza.

Vyuo vinavyofundisha programu mbalimbali katika ngazi ya Astashahada na Diploma ambavyo havina usajili wa NACTE/NECTA vinatakiwa kuwasilisha matokeo ya wanafunzi wao NACTE haraka iwezekanavyo ili matokeo hayo yaweze kutumika katika utambuzi wa vyeti vya wanafunzi husika.

MUDA WA UDAHILI KWA MAKUNDI MBALIMBALI
Muda wa maombi wa kuwasilisha maombi ya udahili kwenye CAS umegawanyika katika makundi matatu kama ifuatavyo:

Kundi la Kwanza – (1 Aprili mpaka 30 Aprili 2012)
Waombaji wote waliomaliza kidato cha sita, Diploma ya Elimu ya Ufundi (NTA level 6), na Diploma ya Ualimu kuanzia mwaka 2011 kurudi nyuma wataanza kuomba udahili kuanzia Aprili 1, 2012 hadi 30 Aprili 2012.

Kundi la Pili
Waombaji wote watakaomaliza kidato cha sita, Diploma ya Elimu ya Ufundi na Diploma ya Ualimu mwaka 2012 wataanza kuomba udahili baada ya matokeo yao ya mitihani kutangazwa na vyombo husika. Hakuna mwanafunzi atakayesajiliwa kwa kutumia matokeo ya muda (provisional or expected results).


Kundi la Tatu
Waombaji wote ambao ni raia wa Tanzania waliosoma nje ya nchi au wenye vyeti ambavyo si vya mfumo wa elimu ya Tanzania (mfano: Cambridge, Bacclaureate, n.k). Waombaji wa kundi hili wanashauriwa kuomba udahili mara matokeo yao yatakapotangazwa na watatakiwa kupeleka vyeti vyao Baraza la Taifa la Mitihani (“National Examinations Council of Tanzania – NECTA”) au Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (National Council for Technical Education - NACTE) kwa ajili ya kulinganisha alama zao za matokeo au kupata ithibati kabla ya kuanza kuomba udahili. Hakuna wanafunzi watakaodahiliwa kwa matokeo ya muda.

UTARATIBU WA MIKOPO
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mamlaka iliyopewa kisheria itatoa mwongozo na utaratibu wa utoaji wa mikopo mwezi Februari 2012. Miongozo hii itachapishwa katika vyombo vya habari na kusambazwa kwenye vyuo vyote vya elimu ya juu nchini na Ofisi za Posta na kwa Wakuu wa Elimu kila wilaya. Maombi ya mikopo kwa mwaka wa masomo 2011/2012 yataanza kupokelewa ifikapo mwezi Machi 2012 na mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 30 Juni 2012. Utaratibu huu utahusu waombaji wote wapya na wale walioko masomoni katika vyuo vya elimu ya juu.

HITIMISHO
Tunapenda kuwajulisha waombaji wote kuzingatia muda wao wa udahili kama ulivyoainishwa katika tangazo hili. Muda ukiisha hawataweza kuomba hadi mwaka wa masomo 2013/2014. Pia waombaji wote wanashauriwa kufuata taratibu za mikopo kam zitakazotolewa na Bodi ya Mikopo ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza katika swala hili

Maelezo zaidi na ufafanuzi kuhusu udahili na mikopo wa 2012/13 yanapatikana katika tovuti zifuatazo:

Tume ya Vyuo Vikuu; www.tcu.go.tz

Baraza la taifa la elimu ya ufundi; www.nacte.go.tz

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Elimu ya Juu; www.heslb.go.tz


IMETOLEWA NA: Katibu Mtendaji, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, S.L.B 6562, Dar es Salaam. Barua pepe (e-mail) es@tcu.go.tz

Vifaa na Mazingira Bora ya Kazi Huzaa Huduma Bora za Afya


Ni Jumatatu asubuhi. Hali ya hewa ya joto la kadiri ilikuwa ni kitu cha kawaida kwa maeneo haya ya Dar es Salaam kipindi cha miezi hii ya mwisho wa mwaka. Tupo darasani kwenye presentation ya somo linalohusu magonjwa ya figo. Mada ilihusu kushindwa kufanya kazi ghafla kwa figo au Acute Renal Failure kwa lugha ya wenzetu. Lilikuwa somo refu lililozungumzia kwa undani tatizo hilo. Baada ya mwenzetu mwasilishaji kumaliza kuwasilisha somo lake kikafuata kipindi cha maswali na majibu na masomo zaidi kutoka kwa Profesa aliyekuwa anasimamia ile mada.

Mada ilikuwa moto. Maswali yetu pamoja na uzoefu wa yule profesa ulitosha kuibua somo na majibu yaliyotosheleza kiu zetu za kujifunza zaidi. Kisha baada ya somo akauliza swali kwa hali ya utani kidogo, nani kati yenu anapenda kuwa Nephrologist (daktari bingwa wa magonjwa ya figo). Wote tulibaki kimya tukitazamana kisha mwanafunzi muwasilisha mada huku akitabasamu alininyoshea kidole akasema Fabby huyo. Profesa aliniangalia kisha akainamisha kichwa chini kwa masikitiko akasema “I feel sorry for you my friend (nakuonea huruma rafiki yangu)”. Sikuelewa kwanini alisema vile nikashtukia tu namuuliza “why Professor?” Huku bado akiendelea kunitazama akanijibu “because you will be seeing your patients dying everyday”. Jibu lake ghafla likanirudisha nyuma kama mwaka mmoja hivi nikiwa nafanya kazi hospitali moja ya Mission iliyopo mkoa fulani kusini mwa nchi. 

Ilikuwa siku ya Jumatano asubuhi. Hali ya kaubaridi baridi iliyokuwepo siku hiyo iliashiria kuanza kwa siku njema. Ninaingia wodini na kusalimiana na wauguzi wa wodi yangu kabla ya kuingia ofisini kujiandaa na round. Nilikuwa na kawaida ya kuanza siku kwa kufanya round kwa wagonjwa waliolazwa kabla ya kuingia ofisini kuwaona wagonjwa wengine wapya na wale wanaokuja kwa ajili ya follow up. 

Baada ya kuwaona wagonjwa kadhaa, nikakifikia kitanda cha mgonjwa mpya aliyekuwa amelazwa usiku wa kuamkia siku hiyo na kuonwa na Clinical officer aliyekuwa zamu. Ni binti wa miaka takribani 20 (kwa sababu za kimaadili sitataja jina, umri wake halisi, mahali anapoishi wala details zake nyingine). 

Hali yake ilikuwa mbaya maana alikuwa amenyong’onyea na alikuwa akipumua kwa shida sana. Mpira wa mkojo ulikuwa ukining’inia pembeni ya kitanda lakini hakukuwa na kitu ndani yake. Uso wake ulionekana kuvimba kwa mbali na alikuwa akizungumza kwa shida. Midomo ilikuwa mikavu na hata ngozi yake ilionekana iliyosinyaa na kavu kuliko kawaida. Nilimuita mwangalizi wake na kuanza kuchukua upya historia ya mgonjwa maana yeye mwenyewe alikuwa akizungumza kwa shida sana. 
Mwangalizi aliniambia kuwa mgonjwa wake, alianza kupata tatizo la kukosa mkojo kwa ghafla kama siku saba zilizopita. Hawakujua sababu hivyo wakadhani ni mambo ya ushirikina wakaamua kumpeleka kwa mganga wa kienyeji ambaye alikaa naye siku tatu huku akimnywesha kila aina ya miti shamba lakini bila mafanikio.

Akasema, “tulipoona hali yake bado ipo vile vile tukaamua kumkimbiza hapa ili tujaribu huduma za kizungu. Kwahiyo kwa ujumla ana siku kama kumi tangu tatizo lilipojitokeza. Wakati tupo kwa mganga angalau hali yake ilikuwa siyo mbaya sana lakini jana usiku ndiyo hali ikabadilika tukaamua kumkimbiza huku. Sasa hivi hali chochote maana analalamika kichefuchefu muda wote, na akijaribu kula tu anatapika chote. Wakati mwingine anaongea vitu havieleweki basi baba ndiyo hivyo hivyo tu”.

Baada ya kuuliza maswali zaidi kulingana na taratibu zetu, kwa muonekano wa mgonjwa na historia yake harakaharaka niliweza kuhisi ni kitu gani kitakuwa kinamsumbua huyu mgonjwa. Niliamua kumfanyia uchunguzi wa mwili (physical examination) ili kuona vishiria vingine vya ugonjwa. Alikuwa na dalili zote za mtu mwenye matatizo ya figo, na mbaya zaidi alikuwa katika hali ya hatari zaidi ya ugonjwa.

Uchunguzi ulionesha, pamoja na dalili nyingine, kuwa alikuwa amevimba miguu (pedal edema) kwa kiasi fulani, tumbo lake lilishaanza kuvimba (ascites) na alikuwa akipumua kwa shida  sana (dysponea), alikuwa na dalili za upungufu wa damu (anemia) na ngozi kavu kuliko kawaida kuonesha kuwa alikuwa amepungukiwa maji mwilini (dehydrated). 

Nikaagiza tufanye vipimo kadhaa kama vile vya kuchunguza utendaji kazi figo, vya kuchunguza uwiano wa madini/chumvi mwilini (electrolytes analysis), ultrasound ya tumbo, vipimo vya moyo na vipimo vingine kadiri nilivyoona inafaa.
Ingawa vingi ya vipimo nilivyoagiza vilishindikana kufanyika ama kwa vile hakukuwa na vifaa vya kufanyia vipimo hivyo au hatukuwa na wataalamu wa maabara wenye ujuzi wa kufanya vipimo hivyo pamoja na kuwepo kwa mashine, bado niliweza kupata jawabu la tatizo lililokuwa linamsumbua mgonjwa wangu ingawa nakiri sikuweza kufahamu chanzo hasa cha ugonjwa wake ni nini kwa vile hatukuwa na vipimo vya kufanya hivyo. Alikuwa akisumbuliwa na kushindwa kufanya kazi ghafla kwa figo yaani Acute Renal Failure (ARF) na kwa dalili zake tayari alishafikia hatua ya kuwa na kiasi kikubwa cha madini ya potassium katika damu (hyperkalemia) na kwamba mrundikano wa uchafu mwilini ulikuwa katika kiwango cha hali ya juu kwa sababu figo zilishaacha kufanya kazi zake inavyotakiwa.

Pamoja na kumuanzishia matibabu, katika hali aliyokuwa nayo matibabu sahihi ilikuwa kwanza kufahamu chanzo cha tatizo ili kukitibu, kumfanyia dialysis ili kutoa uchafu mwilini na hatimaye kama ikionekana figo zimekufa kabisa basi afanyiwe upandikizaji wa figo mpya.

Nilipowaeleza yeye na mwangalizi wake kuhusu matokeo ya vipimo, hatua ya ugonjwa iliyofikiwa na nini cha kufanya ghafla niliona machozi yanamlengalenga mwangalizi. Kwa kweli alistahili kuwa vile. Kwa unyonge akaniuliza, “sasa baba hayo matibabu mnaweza kuyafanya hapa.” Nilimtazama tena na kwa kujitutumua ilibidi nimueleze tu ukweli kuwa hatuna uwezo wa kufanya dialysis pale kwetu, na wala hospitali ya karibu ya mkoa haina uwezo wa kufanya hivyo mjipigepige mumsafirishe mgonjwa Dar es Salaam kwa matibabu zaidi. 

Kama aliyekuwa anasubiri bomu zaidi nikamtajia na gharama za kufanya hayo matibabu na muda anaotakiwa kufanyiwa. Mama mwangalizi alinyamaza kwa sekunde kadhaa kama mtu anayefikiria kitu kisha kwa unyonge akasema , “baba kwa umaskini wetu huu hali yenyewe hii unaiona nilivyo. 
Naomba chonde chonde ujitahidi kufanya lolote lile hapa kama Mungu akipenda kumchukua basi mapenzi yake yafanyike maana hatuna uwezo wa kumsafirisha siyo tu kwenda huko Dar es Salaam bali hata hapo mkoani hatuwezi kufika”. Sikuwa na jinsi zaidi ya kuendelea na matibabu na kufanya kwa kadiri ya uwezo wangu kuokoa maisha ya mgonjwa wangu. 
Nasikitika kuwa baada ya masaa kadhaa mgonjwa yule alifariki kwa mshtuko wa moyo kama complication ya hypekalemia. Nilihuzunika sana lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kuendelea kuchapa kazi kuhudumia wagonjwa wengine.
Kwanini nimekikumbuka hiki kisa?
Hiki ni kisa kimoja tu kati ya visa vingi vingi ambavyo madaktari wanakutana navyo kila siku katika utendaji wao wa kazi. Kushuhudia uhai ukipotea wakati ungeweza kuokoa maisha lakini huna vifaa au wataalamu wa kusaidiana nawe ni jambo linaloumiza sana kwa daktari na watoa huduma ya afya kwa ujumla wake. 
Nawafahamu wenzangu waliowahi kufanya operesheni kwa kutumia mwanga wa tochi za simu baada ya umeme kukatika hospitalini kukiwa hakuna jenereta wala taa hata ya kandili, wapo waliolazimika kubuni mbinu mbadala baada ya kukosekana maji ya drip (iv fluids) kwa ajili ya matibabu. 
Hapa majuzi tumesikia kuhusu watumishi wa hospitali moja ya misheni huko mkoani Manyara wanaolazimika kutumia vipande vya nguo na mashuka kama gloves wakati wa kuhudumia wagonjwa, ipo mifano mingi mingi inayoonesha uzembe wa watendaji wanaotakiwa kuboresha mazingira ya kazi ili watoa huduma ya afya waweze kutoa huduma katika mazingira salama kwao wenyewe na kwa wagonjwa wao na hivyo kuokoa maisha yao.

Kifo cha mgonjwa yule kingeweza kuzuilika au hata kucheleweshwa kwa mfano kama hospitali ya mkoa ingewezeshwa kutoa huduma ya dialysis kiasi cha kuweza kumkimbiza mgonjwa hospitalini hapo haraka. Lakini pia ingewezekana kuwa katika wakati mzuri wa kutambua chanzo cha ugonjwa wake kama hospitali ile ingekuwa na vifaa vya uhakika vya vipimo na pengine kulipatia ufumbuzi bila hata kuhitaji kumpa referral. Ipo mifano mingi yenye kufanana na hiyo. 

Mgogoro unaondelea hivi sasa nchini kati ya madaktari kwa upande mmoja na serikali kwa upande mwingine ni jambo linalosikitisha kutokana na jinsi suala hili lilivyoshughulikiwa na watendaji wakuu wa wizara pamoja na kuwa madai ya madaktari hawa ni ya msingi sana. Moja ya madai ya madaktari ni kutaka uboreshaji wa hospitali na vituo vyetu vya afya kwa maana ya vitendea kazi na mazingira ya kufanyia kazi. Dai hili siyo tu lina nia njema ya kuwahakikishia madaktari wanafanya kazi katika mazingira bora yenye vitendea kazi vya uhakika bali pia linahusu afya njema kwa ajili ya wananchi wenyewe. Kwa maneno mengine madai ya madaktari yanahusu pia ustawi wa afya za wananchi wengine na siyo maslahi yao tu binafsi.
Ni aibu sana kwa hospitali ya Taifa, kwa mfano, kukatikiwa umeme bila kuwa na chanzo kingine mbadala cha umeme huku ukitegemea watoa huduma hawa kuacha kunung’unika. Haiingii akilini hospitali ya Wilaya kukosa hata strips za kupimia sukari mwilini na kisha ukategemea wafanyakazi wawe na furaha na kazi yao. Haingii akilini wauguzi wafurahie kufanya kazi kwenye wodi ambayo wagonjwa wamelala watatu watatu kwenye kitanda kimoja. Ni aibu, ni aibu, ni aibu. 

Pamoja na nia njema ya madai hayo, bado inasikitisha kuona jinsi ambavyo serikali kupitia kwa Waziri Mkuu walivyoona kuwa hakuna njia ya kuweza kushughulika na madai hayo zaidi ya KUAMURU madaktari kurudi kazini kana kwamba AMRI inaweza kuboresha mazingira ya kazi. Kumlazimisha tabibu pamoja na watoa huduma wengine wa afya kurudi katika mazingira yale yale wanayoyapigia kelele siyo tu hakutatui tatizo bali kunaongeza ukubwa wa tatizo. 

Hakuna tabibu na muuguzi atakayefanya kazi kwa moyo mmoja huku akiwa na hasira na kinyongo kwanza kwa kuamrishwa bila kusikilizwa anachodai lakini pili kwa kulazimishwa kurudi katika mazingira yaleyale anayodai yarekebishwe. Hatari ninayoina ni kwa wagonjwa kuzidi kupoteza maisha na wengine kuishia kupata vilema kutokana na matibabu butu watakayopewa na wahudumu wasioridhika. Na haya yakitokea wahudumu wa afya kamwe wasilaumiwe!

Amri, vitisho, ubabe wala kamata kamata ya madaktari siyo suluhisho la matatizo. Ni matumaini yangu, wale wenye mamlaka wataona uzito wa madai ya madaktari na kuyapatia ufumbuzi wa kweli badala ya kuyapatia majibu ya kisiasa yenye vitisho na nia ya kufunika kombe ili mwanaharamu apite. 
Kinyume na hapo ni kuahirisha matatizo na kuendelea kuhatarisha afya za wananchi wengi masikini na wengine kufa kama yule binti. Lakini pia ni matumaini yetu, wananchi watatambua nia njema ya madaktari ya kutaka kuboreshewa mazingira yao ya kazi ili wananchi nao waweze kupatiwa huduma bora zaidi na uhakika tofauti na sasa.


MAKALA HII IMEANDIKWA NA FABIAN P. MGHANGA

Sunday, January 29, 2012

sbl yazindua muonekano mpya wa dhahabu wa kinywaji cha serengeti premium lager.

Chupa mpya ya Serengeti  Premium Lager yenye muonekano wa Dhahabu, ikiibuka kutoka kwenye maji mara baada ya kuzinduliwa rasmi usiku wa kuamkia leo,huku wageni waalikwa mbalimbali wakilishuhudia tukio hilo.

Mgeni rasmi,Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda Biashara na Masoko B. Joyce Mapunjo akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari,mara baada ya uzinduzi huo uliofanyika usiku wa kuamkia leo,jijini Dar na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali.
 Cheeersss....!
 Mdau akicheers na meza kuu..!

Mgeni rasmi,Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda Biashara na Masoko B. Joyce Mapunjo akiwa na viongozi wa kuu wa SBL pamoja na wadau wa kinywjai hicho wakiwa katika picha ya pamoja.

Mgeni rasmi,Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda Biashara na Masoko B. Joyce Mapunjo akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo ya mabadiliko ya muonekano mpya wa kinywaji cha Serengeti Premium Lager.iliyofanyika Golden Tulip,jijini Dar usiku wa kuamkia leo.
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Richard Wells akizungumza katika uzinduzi huo wakati alipomkaribisha mgeni rasmi,Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda Biashara na Masoko B. Joyce Mapunjo.
Mkurugenzi wa Masoko kampuni ya bia ya Serengeti,Bw.Ephraima Mafuru akizungumzia mafanikio mbalimbali yaliyopatikana katika taifa kupitia kinywaji murua kabisa cha Serengeti premium Lager.
Meneja wa Kinywaji cha Serengeti Premium Lager,Allan Chonjo akiwakaribisha wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo usiku wa kuamkia leo ndani ya Hotel ya Golden Tulip,jijini Dar.
 Muonekano mpya wa dhahabu unaosisimua.
 Muonekano mpya wa dhahabu unaowasisimua wengi kama hivi pichani.
Moja ya kikundi cha ngoma za asili kikitumbuiza usiku huu kabla ya uzinduzi rasmi kufanyika.
Mkurugenzi wa Masoko kampuni ya bia ya Serengeti,Ephraim Mafuru akiongea na Mkurugenzi wa Extra Bongo Mzee wa farasi Ali Choki , kulia ni Meneja Masoko wa (SBL) Emilian Rwejuna.
 Meneja Masoko wa (SBL) Emilian Rwejuna (kati) akiwa na wadau.
Meneja wa kinywaji cha Tusker,Rita Mchaki akiwa na mdau kwenye uzinduzi huo.
Wadau ndani ya uzinduzi wa muonekano mpya wa dhahabu wa kinywaji cha Seregengeti Premium Lager
 Serengeti bia yetu,kinywaji chetu kwa rahaaa zetuuuu...!
Pichani wanne kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Richard Wells,akiwa na wageni waalikwa mbalimbali usiku huo.

Bendi ya muziki wa dansi ya Extra Bongo ikitumbuiza kwenye uzinduzi huo.
Shoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Richard Wells,  Mkurugenzi wa Masoko kampuni ya bia ya Serengeti,Ephraima Mafuru na Meneja wa Mahusiano kampuni ya bia ya Serengeti Nandi Mwiyombela wakijadiliana jambo kabla ya uzinduzi rasmi kufanyika.
Wadau,wageni waalikwa mbalimbali wakiserebuka kwanza huku wakisubiri kwa hamu uzinduzi huo mpya wa dhahabu wa kinywaji cha Serengeti Premium Lager,usiku wa kuamkia leo kwenye hotel ya  Golden Tulip,jijini Dar.

Friday, January 27, 2012

Mechi ya hisani kati ya Twiga Stars vs Bunge SC kwenye uwanja wa karume jijini dar

Kikosi cha timu ya Bunge SC kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo wao na timu ya Taifa ya Wanawake ‘Twiga Stars’, ambao ulikuwa ni maalumu kuichangia timu hiyo uliofanyika kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam. Twiga Stars imeshinda 2-1.
Kikosi cha Twiga Stars kikiwa katika picha ya pamoja.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi, akipeana mkono na mshambuliaji wa Twiga Stars, Mwanahamis Omari.
Wachezaji wa Bunge SC, Halima Mdee na William Ngeleja, wakibadilishana mawazo kabla ya kuanza kwa mchezo.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu, akizungumza kabla ya kukabidhi kitita cha sh. milioni 7 kwa wachezaji wa Twiga Stars.
Nahodha wa timu ya Twiga Stars, Sophia Mwasikili, akionesha kitita cha sh. milioni 7 baada ya kukabidhiwa na Naibu Waziri, Ummy Mwalimu (kulia).
Mlinzi wa timu ta Twiga Stars, Siajabu Hassan akimtoka mshambuliaji wa Bunge SC, Adam Malima.
Mshambuliaji wa Bunge SC, Sadifa Juma Khamis akimtoka beki wa Twiga, Fatuma Khatib.
Mshambuliaji wa timu ya Bunge SC, Adam Malima akimtoka beki wa timu ya Twiga Stars, Siajabu Hassan wakati wa mchezo wa hisani  ambao ulikuwa ni ni maalumu kwa kuichangia timu ya Twiga Stars uliofanyika kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam. Twiga Stars imeshinda 2-1.
Nahodha wa timu ya Twiga Stars, Sophia Mwasikili.Picha na Francis Dande.

Thursday, January 26, 2012

ARUSHA TECHNICAL COLLEGE EMPLOYMENT OPPORTUNITIES

Arusha Technical College (ATC) is an autonomous Institution established by the Government Establishment Order No. 78 as enabled by the NACTE Act No. 9 of 1997. ATC replaced the then Technical College Arusha (TCA) that existed since 1978. 

The vision of ATC is to be a centre of excellence in training, research and consultancy in science and technology in Africa by 2020. In order to fulfill its functions properly, the College is seeking to recruit qualified and experienced Tanzanians to fill in the following vacancies:

LECTURER (3 Posts: Civil Engineering/Structural Engineering, Irrigation Engineering, Chemistry, Electrical Engineering) Qualification: Holder of Doctorate (PhD) Degree in relevant field.

Duties and Responsibilities:

Teaches up to undergraduate (NTA level 8);
Prepares learning resources and design training exercises for students;
Conducts consultancy and community services;
Develops and reviews existing curriculum;
Undertakes individual research and participates in scientific/academic congregations ;
Coaches junior teaching staff; and
Performs any other duties as assigned by supervisors.
Salary Scale: PHTS 10 - 12

Terms of Engagement: Permanent and Pensionable

ASSISTANT LECTURER (7 Posts: Computer Engineering/Science/IT, Electrical Engineering, Electronics and Telecommunication Engineering, Land Surveying/Geomatics, Irrigation Engineering/Water Resources/Integrated Water Resources, Transportation Engineering, Automobile Engineering/Mechanical Engineering with a bias in hydraulics and Pneumatics)
Qualification: Holder of Masters’ Degree in relevant field.

Duties and Responsibilities:

Teaches up to undergraduate (NTA level 8);
Prepares learning resources for tutorial exercises;
Conducts research, seminars and case studies;
Carries out consultancy and community services;
Prepares teaching manual; and
Performs any other duties as assigned by supervisor.
Salary Scale: PHTS 8 - 9

Terms of Engagement: Permanent and Pensionable

TUTORIAL ASSISTANT (10 Posts: Entrepreneurship, Physics, Biology, Mechanical Engineering with specialization in Energy Technology and Industrial Experience, Electrical Engineering, Electronics and Telecommunication Engineering, Civil Engineering with specialization in Geotechnical Engineering/Pavement Engineering /Highway Engineering/Structural Engineering, Automobile/Autoeletric and electronics Engineering)
Qualification: Holder of Bachelor’s Degree in relevant field.

Duties and Responsibilities

Teaches up to NTA level 7 (Higher Diploma) ;
Assists in conducting tutorial and practical exercises for students;
Prepares learning resources for tutorial exercises;
Assists in conducting research under close supervision;
Carries out consultancy and community services;
Performs any other duties as assigned by supervisors.
Salary Scale: PHTS 4 - 7

Terms of Engagement: Permanent and Pensionable

SENIOR INSTRUCTOR II (4 Posts: Electrical engineering, Electronics and Telecommunication Engineering, Mechanical Engineering with specialization in Welding/Foundry/ fitter Mechanics, Automobile Eng. and Communication Skills )
Qualification: Holder of Bachelor’s Degree or equivalent in relevant field.
Duties and Responsibilities

Teaches up to NTA level 7 (Higher Diploma) ;
Conducts research and consultancy projects;
Develops and reviews curricula;
Supervises students projects;
Supervises and assists junior teaching staff;
Assumes leadership roles; and
Performs any other duties as assigned by supervisors.
Salary Scale: PTSS 13 - 14

Terms of Engagement: Permanent and Pensionable

ACCOUNTS TECHNICIAN II (2 Posts)
Qualification: Holder of Ordinary Diploma in Accountancy from a recognized institution, ATEC II or

equivalent qualifications with at least two years working experience.

Duties and Responsibilities

Ensuring that all invoices are properly recorded and filed after payments;
Posting of all primary data in the respective journals;
Cashiering;
Maintaining Petty cash journals;
Performs any other duties assigned by his/her seniors.
Salary Scale: PGSS 8 - 9

Terms of Engagement: Permanent and Pensionable

SENIOR TECHNICIAN I (2 Posts: Laboratory Science – Chemistry , Electrical Engineering)
Qualification: Holders of Ordinary Diploma (NTA-6) or FTC in the relevant field with at least three (3) years working experience

Duties and Responsibilities

Assists the Principal Technician in administrative work;
Ensures availability of materials and equipment and their safe custody;
Supervises junior technicians;
Supports lecturers and Instructors in their teaching, research and consultancy services;
Trains or conducts orientations for newly recruited technicians;
Conducts routine repairs and regular maintenance of equipment in the respective ;
Laboratory workshop.
Performs any other duties assigned by his/her seniors.
Salary Scale: PGSS 12-14

Terms of Engagement: Permanent and Pensionable

TECHNICIAN I (7 Posts: Civil Engineering, Transportation/Highway Engineering, Electrical Engineering, Mechanical Engineering, Automotive Engineering, Computer Engineering/Science/IT)
Qualification: Holders of Ordinary Diploma (NTA-6) or FTC in the relevant field with at least three (3) years working experience

Duties and Responsibilities

Assist in students’ practical training and projects;
Maintains laboratory/ workshop facilities and equipment;
Trains and supervises newly recruited and junior technicians / artisans;
Supports lecturers and Instructors in teaching, research and consultancy projects;
Provides specialized technical services to the public;
Performs any other duties assigned by the Head of Department or relevant senior staff.
Salary Scale: PGSS 8-9

Terms of Engagement: Permanent and Pensionable


HUMAN RESOURCES OFFICER II (1 Post)
Qualification: Holders of a Bachelor Degree with a bias in either Human Resources Management, Personnel Management, Business Administration or equivalent qualifications from a recognised Institution.

Duties and Responsibilities

Collects, analyses, tabulates and maintains personnel records and statistics;
Assists in the administration of recruitment and staff allocation;
Assists in office management, personnel management, and staff welfare;
Performs any other duties assigned by his/her seniors.
Salary Scale: PGSS 8-9

Terms of Engagement: Permanent and Pensionable

SENIOR PLANNING OFFICER II (2 Posts)
Qualification: Holders of a Bachelor degree in Economics, Educational Planning, Engineering/General Management/Human Resources Management, System analysis/, Statistics or its equivalent with at least two (2) years of working experience in that position.

Duties and Responsibilities

Heads the activities of the information sub-section of the Planning unit;
Formulates and co-ordinates corporate plans and strategies based upon priorities for resource allocation to various functional programmes;
Prepares plans or projects document for submission through Governing Board to Government and other Donors for funding;
Prepares basic statistical and management reports;
Stores and retrieves inventory information;
Interprets and analyses data for plan formulation ;
Performs any other duties as delegated by principal.
Salary Scale: PGSS 12-13

Terms of Engagement: Permanent and Pensionable

SENIOR ESTATES OFFICER GRADE II (1 Post)
Qualification: Holders of a Bachelor Degree in Civil Engineering,, Architectural Studies or equivalent from a recognised Institution and must have at least two years of working experience.

Duties and responsibilities

Supervises maintenance and cleaning of College properties and grounds;
Examines bills of quantities;
Follows-up of title deeds and acquisition of land;
Prepares budgets for maintenance works
Ensures that ATC office buildings, staff houses, furniture and equipment are properly maintained;
Ensures that all staff houses and office buildings have Title Deeds;
Performs any other duties assigned by his/her seniors.
Salary Scale: PGSS 12-13

Terms of Engagement: Permanent and Pensionable

PRINCIPAL INTERNAL AUDITOR II (2 Posts)
Qualification: Holder of a Bachelor Degree in Commerce majoring in Accountancy or ADA from a recognized institute, CPA (T) and must be registered by NBAA as authorized Auditor/Accountant, with at least three years working experience.

Duties and Responsibilities:

Plans, coordinates and directs all internal audit operations;
Advises the College on the soundness, adequacy and application of Internal controls, accounting and financial regulations;
Conducts checks and investigates all books of accounts;
Keeps all offices informed of College policies, regulations and Governing Board resolutions related to internal auditing matters;
Examines financial documents and controls over assets of the College and reports to the Principal quarterly on the findings;
Advises on measures to reduce expenses and increase revenue;
Reviews and audits the financial activities;
Performs any other duties as may be assigned by his/her senior.
Salary Scale: PGSS 17

Terms of Engagement: Permanent and pensionable

SENIOR LEGAL OFFICER GRADE III (1 Post)
Qualification: Holder of a Bachelor Degree in Laws or Equivalent Qualification from a recognized institution with at least three years of working experience.

Duties and Responsibilities

Represents the college in courts of law;
Drafts contracts as may be required by the College;
Prepares draft amendments to the College’s Act;
Recommends improvements in Governing Board regulations in line with the College’s Act;
Assists in the interpretation of laws and other Legal documents;
Performs any other duties as may be assigned by Principal.
Salary Scale: PGSS 12-13

Terms of Engagement: Permanent and pensionable

WARDEN GRADE I (1 Post)
Qualification: Holder of a Bachelor Degree with a bias in Education/Social Science or Advanced Diploma in Social Science or Community Development with at least one year working experience.

Duties and Responsibilities

Assists the Dean of Students in planning, directing and managing the operations of the student’s welfare;
Undertakes the administration of student’s welfare services in the areas of accommodation, catering, health and recreation;
Acts as advisor of the students organisation;
Assists the general election of the students Government;
Ensures that the Colleges by laws and regulations guiding the students’ life in Halls of residence are being observed;
Performs any other duties assigned by his/her seniors.
Salary Scale: PGSS 10-11

Terms of Engagement: Permanent and pensionable

ARTISAN I (5 Posts: Fitter and tuner, Carpentry and Joinery, Masonry and Brick laying, Electrical Engineering Automotive Parts Machinist/Automechanics, )
Qualification: Holder of Certificate of Secondary School Education (CSSE) and Trade Test I or equivalent in the relevant fields.

Duties and Responsibilities

Performs routine specified tasks that demand higher technical skills under supervision;
Keeps the work place tidy;
Collects and takes care of working tools;
Carries out minor repairs and maintenance;
Reports maintenance problems to senior staff;
Performs any other duties as assigned by the relevant senior staff.
Salary Scale: PGSS 6-7

Terms of Engagement: Permanent and pensionable

SENIOR LIBRARY ASSISTANT II (1 Post)
Qualification: Holder of Diploma in Librarianship from SLADS with at least one year working experience.

Duties and Responsibilities

Performs library clerical duties;
Registration of readers ;
Issuing of books to readers;
Receiving books from readers;
Assists in cataloguing and classification of books, journals reprints;
Performs any other duties assigned by his/her seniors.
Salary Scale: PGSS 9-10

Terms of Engagement: Permanent and pensionable

SUPPLIES OFFICER II (2 Posts)
Qualification: Holder of Diploma in Materials Management , Supplies, Procurement and have passed Part II examinations conducted by the Procurement and Supplies Professionals and Technicians Board and who has completed at least three (3) years of satisfactory service in that position.

Duties and Responsibilities

Ensures full responsibilities for the entire procurement of supplies functions;
Co-ordinates and forecast stores requirements;
Ensures maintenance and amendment of stock level figures;
Performs any other duties assigned by his/her seniors.
Salary Scale: PGSS 9-10

Terms of Engagement: Permanent and pensionable

OFFICE MANAGEMENT SECRETARY I (1 Post)
Qualification: Holders of a Diploma in Secretarial Studies from government recognized institutions and who has advanced training in modern office technology including computer application with office administration and working experience of at least three years.

Duties and Responsibilities

Provides assistance to top executives of the College;
Undertakes routine correspondence with prior approval of his/her senior;
Arranges meetings and appointment schedules for the Senior Executives;
Assists in drafting and proof – reading speeches and write-ups for the executives;
Deals with confidential matters in the office of the Executives;
Performs any other duties as may be assigned by his/her senior.
Salary Scale: PGSS 13-15

Terms of Engagement: Permanent and pensionable

SECRETARY I (2 Posts)
Qualification: Holders of a Diploma in Secretarial Studies from government recognized institutions also serving in that position for at least three years and has training in Office Management, Computer applications, Word Processors and other modern Office Machines like scanner, Telefax etc.

Duties and Responsibilities

Types all general correspondence and non-confidential matters;
Types letters, minutes, notes, bulletins, circulars, certificates, charts and stencils;
Duplicates reports, letter etc. ;
Takes proper care of all machines under his/her charge and make sure that are used for official work only;
Files copies of typed letter in relevant files;
Receives and directs visitors;
Makes sure there are all necessary facilities for proper job performance e.g. typewriters, different typing papers, carbon papers, erasing ink, ribbons etc;
Uses modern machines in discharging his/her duties;
Takes care of all facilities under his/her charge ;
Performs any other duties assigned by his/her seniors.
Salary Scale: PGSS 8-9

Terms of Engagement: Permanent and pensionable

OFFICE ATTENDANT (W) (1 Post: Automotive Stores Attendant)
Qualification: Holders of Certificate of Secondary School Education (CSSE) and Trade Test II or equivalent qualification with at least three years working experience.

Duties and Responsibilities

Keeps the work place tidy;
Collects and takes care of working tools;
Carries out minor repairs and maintenance;
Reports maintenance problems to senior staff.
Salary Scale: POSS 8-9

Terms of Engagement: Permanent and pensionable

SENIOR DRIVER II (2 Posts)
Qualification: Holder of Certificate of Secondary School Education (CSSE) and Class “C” driving license with at least three years of clean driving experience and have passed Trade Test II or equivalent qualification in a motor vehicle mechanics or other relevant field.

Duties and Responsibilities

Drives motor vehicles, cars, pick-ups and lorries as may be assigned;
Ensures motor vehicles and their accessories are in good condition;
Makes some minor repairs;
Maintains and records log sheets (books) for all journeys made;
Reports promptly any defects or problems detected in the vehicles;
Performs any other duties assigned by his/her seniors.
Salary Scale: POSS 8-9

Terms of Engagement: Permanent and pensionable

GENERAL REQUIREMENTS FOR APPLICANTS

Applicants must submit signed application letters accompanied with the following:
Copies of relevant certificates and transcripts;
Current Curriculum Vitae.
Names and complete addresses of two referees;
Age limit: Not above 45 years.
Application should reach the College by using the address below not later than 24th February, 2012.
Only short- listed applicants will be contacted.

The Principal,
Arusha Technical College,
P. O. Box 296,
Arusha.