Sunday, March 18, 2018

MPINA ALIA NA WANAODANGANYA CHAPA







Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (mwenye kofia) akimshika mkia ng’ombe kuangalia kama amepigwa chapa alipotembelea mnada wa Kizota nje kidogo ya mji wa Dodoma leo ambapo ametoa tathimini ya upigaji chapa unaoendelea nchini. 
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalah Ulega(aliyenyosha mkono)akimwonyesha Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (mwenye kofia) chapa ya mifugo alipotembelea mnada wa Kizota nje kidogo ya mji wa Dodoma leo ambapo wametoa tathimini ya upigaji chapa unaoendelea nchini.Nyuma yake ni Kaimu Katibu Mkuu wa Mifugo Bi. Selina Lyimo, wakwanza kushoto mwenye shati la kitenge ni Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Ugani wa Wizara Dkt. Angelo Mwilawa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo nchini, Dkt Maria Mashingo akishiriki zoezi la upigaji chapa mifugo mkoani Kigoma hivi karibuni. Tarehe ya mwisho kitaifa ya uhitimishaji wa kupiga chapa mifugo yote nchini iliyotolewa na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kasim Majaliwa Majaliwa ni 31/3/2018. 


Na. John Mapepele, Dodoma

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa, Luhaga Mpina ametoa onyo kali kwa viongozi wa Serikali katika Halmashauri zote nchini wanayoihujumu operesheni maalum ya kitaifa ya kupiga chapa mifugo inayoendelea nchi nzima kwa kutoa taarifa za uongo zinazoonesha kuwa mifugo mingi imepigwa chapa tofauti na hali halisi ambapo amesema Wizara yake itapita kila Wilaya kufanya tathmini ya kina baada ya tarehe ya mwisho ya upigaji chapa kitaifa iliyotolewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu, Marchi 31 mwaka huu ambapo watendaji watakaobainika kudanganya sheria zitachukua mkondo wake.

Aidha ametoa maelekezo kwa Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya kote nchini kuhakikisha kwamba mifugo yote inatakiwa iwe imepigwa chapa hadi tarehe ya mwisho iliyopangwa na kusiwe na visingizio vyaaina yoyote ikiwa ni utekelezazi wa Sheria ya Utambuzi,Usajili na Ufuatiliaji wa Mifugo Namba 12 ya Mwaka 2010 na kanuni zake za mwaka 2011. 

Maelekezo hayo aliyatoa jana akiwa Naibu Waziri wake Mhe. Abdalah Ulega na Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi walipotembelea mnada wa upili wa Kizota pembeni kidogo wa mji wa Dodoma kutoa tathmini ya zoezi la upigaji chapa nchini kabla ya siku ya mwisho ya upigaji chapa mifugo yote nchini ambayo ni tarehe 31/3/2018.

Waziri Mpina alisema, kulingana na takwimu ambazo Wizara imeletewa hadi tarehe 11 Machi, 2018 inaonyesha kwamba, jumla ya ng’ombe 16,744,355 kati ya 17,390,090 sawa na asilimia 96.3 ya ng’ombe wote nchini wamepigwa chapa. Aidha, jumla ya Punda 51,494 wamepigwa chapa nchini. 

“Hivi karibuni nilitembelea mnada wa Pugu nikaangalia idadi ya mifugo iliyopigwa chapa hawafiki hata asilimia tano, lakini leo hapa sote tumeshuhudia idadi ya mifugo wote waliopigwa chapa katika mnada huu wa Kizota ni chini ya asilimia mbili. Minada hii ndiyo mikubwa nchini ukianzia wa Pugu na huu ni wa Kizota ni wa pili kwa hiyo inadhihirisha kwa uhakika kabisa kuwa kuna udanganyifu mkubwa unaofanywa na watendaji wasio waaminifu wanaopotosha taarifa.” Alisistiza Mpina.

Alisema wilaya nyingine zimeleta takwimu ambazo zinaonyesha zimepia chapa mifugo kwa zaidi ya asilimia elfu moja ambapo amezionya kutojiingiza katika matatizo kwa kuendelea kudanganya. 

Aidha alisema tathmini ya jumla kuanzia mwezi Disemba 2017 hadi tarehe 11 Marchi, 2018 inaonyesha kwamba, Halmashauri 85 zimepiga chapa kwa asilimia 100 na zaidi; Halmashauri 86 zimepiga chapa kati ya asilimia 50 na 100, na Halmashauri 4 zimepiga chapa chini ya asilimia 50. 

Alizitaja Halmashauri hizo kuwa ni Kasulu, Madaba, Arusha na Meru, ambapo alisema Halmashauri zilizobaki ni miongoni mwa Halmashauri zenye ng’ombe wengi wa maziwa nchini wanaotarajiwa kuvishwa hereni. Halmashauri hizo ni Manispaa ya Ubungo, Temeke, Moshi, Kinondoni na Ilala. Alisema Halmashauri zingine zenye ng’ombe wengi wa maziwa kuliko wanaochungwa ni Rungwe, Busokelo na Kibaha. 

Alisema tathmini ya zoezi la chapa tangu kuongezwa kwa muda kutoka tarehe 31 Januari, 2018 hadi sasa inaonyesha ongezeko la Halmashauri 14 zilizopiga chapa mifugo zaidi ya asilimia 100 na kupungua kwa Halmashauri 8 zilizopiga chapa kati ya asilimia 50 – 100 na kupungua kwa Halmashauri 25 zilizopiga chapa chini ya asilimia 50.

“Napenda kutoa maelekezo kwa wafugaji kwamba mifugo yote ipigwe chapa popote ilipo ilimradi ni ya Tanzania ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima baada ya tarehe ya mwisho iliyopangwa na Serikali ambayo ni mwisho wa mwezi huu na ninaomba ieleweke kuwa visingizio vyoyote havitakubalika’ Alisisitiza Waziri Mpina. 

Akielezea umuhimu wa zoezi hilo, Mpina alisema kwamba kukamilika kwa zoezi hilo kutasaidia kutambua mifugo yote iliyopo nchini ili kukidhi mahitaji ya biashara katika masoko ya ndani na nje ya nchi,kudhibiti magonjwa ya mifugo na kudhibiti wizi wa mifugo na usafirishaji holela.

Aidha kutasaidia kuepusha migogoro inayoendelea maeneo mbalimbaili nchini baina ya wafugaji,wakulima pamoja na watumiaji wengine wa raslimali ardhi na kutawezesha Serikali kupata idadi sahihi ya mifugo iliyonayo ili kupanga kupanga mipango inayotekelezeka na kuleta mapinduzi katika sekta hiyo.

Alisema Zoezi la upigaji chapa ni endelevu kwa mifugo ambapo alisema ng’ombe na punda wanaotimiza miezi sita wanatakiwa kupiga chapa.

Awamu ya kwanza ya zoezi la upigaji chapa ng’ombe na punda nchini ilianza rasmi tarehe 14 Desemba, 2016 kufuatia Agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu na ilitarajiwa kukamilika tarehe Desemba 31, 2017. Tathmini iliyofanywa baada ya kukamilika awamu hiyo ya Desember, 2017 ilionyesha jumla ya ng’ombe 7,401,661 sawa na asilimia 38.5 ya lengo walikuwa wamepigwa chapa. Kutokana na kiwango kidogo cha ng’ombe waliokuwa wamepigwa chapa wakati huo, Waziri wa Mifugo, Mheshimiwa Luhaga Mpina aliongeza muda wa kukamilisha zoezi hili hadi tarehe 31 Januari, 2018. Hadi kufikia tarehe 31 Januari, 2018 jumla ya ng’ombe 15,192,565 sawa na asilimia 87.4 walikuwa wamepigwa chapa. 

Aidha jumla ya punda 6,944 walikuwa wamepigwa chapa kati ya punda 572,353 wanaotarajiwa kupigwa chapa nchini. Pia, jumla ya ng’ombe wa maziwa 58,214 walikuwa wamevishwa hereni kati ya ng’ombe wa maziwa 782,995 wanaotarajiwa kuvishwa hereni. Pamoja na muda huo kuongezwa, Halmashauri nyingi zilikuwa bado hazijakamilisha zoezi hili kikamilifu. Kutokana na mapungufu mbalimbali yaliyojitokeza Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kasim Majaliwa Majaliwa alilazimika kuongeza muda zaidi mpaka tarehe 28 Machi, 2018 na kuziagiza Mamlaka ya Serikali za Mitaa kusimamia zoezi hili kikamilifu kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi na kumpa taarifa ya Utekelezaji ifikapo Machi 31, mwaka huu.

Wakati huo huo, Waziri Mpina alisema kuwa Wizara itafanya mageuzi makubwa ya kupanua kiwanda cha machinjio ya nyama cha Dodoma(TMC) ili kiweze kukidhi mahitaji ya sasa ya mifugo ambapo kumekuwa na ongezeko kubwa ya mifugo nchini.

Mmoja wa wafanyabiashara wa mifugo Shabani zuberi, alimweleza Waziri kuwa kwa sasa gharama ya uchinjaji wa nyama katika machinjio ya kiwanda hicho ni juu ukilinganisha na machinjio nyingine nchini ambapo ni shilingi elfu ishirini kwa ng’ombe mmoja na kwamba nyama kwa ajili ya soko la ndani inanyimwa sehemu ya kugandishia tofauti na nyama inayosafirishwa kwenda nje ya nchi suala ambalo linawafanya wapate hasara kubwa nyama ikishindwa kuuzika katika siku husika kutokana na kukosa sehemu ya kugandishia.

Akijibu hoja hizo, Mpina aliielekeza menejimenti ya kiwanda hicho kukaa na Wizara na kuangalia namna bora ya kuweka gharama ya uchinjaji itakayoendana na hali halisi ya bei la soko.

Aidha alikiagiza kiwanda kuanza mara moja kutoa huduma ya kugandisha na kuhifadhi nyama ya walaji wa ndani ambapo pia alitoa wiki mbili kuhakikisha huduma ya maji inaletwa na kiwanda hicho katika machinjio ya Kizota.Alisisitiza kuwa Mnada wa Kizota utaboreshwa na Serikali kwa kuwa unaingiza milioni 624 kwa mwaka hivyo ukiboreshwa miundo mbinu yake utaongeza mapato yake.

“Hatuwezi kuwajali watu kutoka nje ya nchi na usiwajali wananchi wako wa ndani ya nchi, naamuru kwamba TMC wapeni huduma ya kugandisha nyama wateja wenu wa soko la ndani” alisistiza Mpina.

Alimpongeza Naibu Waziri, Abdalah Ulega kwa juhudi anazozifanya za kuhakikisha minada yote nchi inakuwa na miundombinu bora ambapo awali Mhe. Ulega alitembelea mnada wa Kizota na kujadiliana na wadau wa mnada huo kuhusiana na mambo mbalimbali.

Naye Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo Selina Lyimo alimshukuru Waziri Mpina kwa maelekezo aliyoyatoa kwa Wizara na kumhakikishia kwamba yatatekelezwa mara moja ili kuleta mageuzi na mapinduzi makubw a katika sekta. 

Aidha Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti Mafunzo na Ugani,Angelo Mwilawa amesema Idara yake itaendelea kuratibu tafiti mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo hususan kwenye eneo la malisho na uzalishaji wa mbegu bora za mifugo ili wafugaji waweze kufuga kisasa
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (mwenye kofia) akimshika mkia ng’ombe kuangalia kama amepigwa chapa alipotembelea mnada wa Kizota nje kidogo ya mji wa Dodoma leo ambapo ametoa tathimini ya upigaji chapa unaoendelea nchini.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalah Ulega(aliyenyosha mkono)akimwonyesha  Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (mwenye kofia) chapa ya mifugo alipotembelea mnada wa Kizota nje kidogo ya mji wa Dodoma leo ambapo wametoa tathimini ya upigaji chapa unaoendelea nchini.Nyuma yake ni Kaimu Katibu Mkuu wa Mifugo Bi. Selina Lyimo, wakwanza kushoto mwenye shati la kitenge ni Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Ugani wa Wizara Dkt. Angelo Mwilawa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia  Sekta ya Mifugo nchini, Dkt Maria Mashingo akishiriki zoezi la upigaji chapa mifugo mkoani Kigoma hivi karibuni. Tarehe ya mwisho kitaifa ya uhitimishaji wa kupiga chapa mifugo yote nchini iliyotolewa na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kasim Majaliwa Majaliwa ni 31/3/2018.

Na. John Mapepele, Dodoma

Waziri wa  Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa, Luhaga Mpina ametoa onyo kali kwa viongozi wa Serikali katika Halmashauri zote nchini wanayoihujumu operesheni maalum ya kitaifa ya kupiga chapa  mifugo inayoendelea nchi nzima kwa kutoa taarifa za uongo zinazoonesha kuwa mifugo mingi imepigwa chapa tofauti na hali halisi ambapo amesema Wizara yake itapita kila Wilaya kufanya tathmini ya kina  baada ya tarehe ya mwisho ya upigaji chapa kitaifa iliyotolewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu, Marchi 31 mwaka  huu ambapo watendaji watakaobainika kudanganya sheria zitachukua mkondo wake.

Aidha ametoa maelekezo kwa Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya kote nchini kuhakikisha kwamba mifugo yote inatakiwa iwe imepigwa chapa hadi tarehe ya mwisho iliyopangwa na kusiwe na visingizio  vyaaina yoyote ikiwa ni utekelezazi wa Sheria ya Utambuzi,Usajili na Ufuatiliaji  wa Mifugo Namba 12 ya Mwaka 2010 na kanuni zake za mwaka 2011.

Maelekezo hayo  aliyatoa jana akiwa Naibu Waziri wake Mhe. Abdalah Ulega na Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi walipotembelea mnada wa upili wa Kizota pembeni kidogo wa mji wa Dodoma kutoa tathmini ya zoezi la upigaji chapa nchini kabla ya siku ya mwisho  ya upigaji chapa mifugo yote nchini ambayo ni tarehe 31/3/2018.

Waziri Mpina alisema, kulingana  na takwimu ambazo Wizara imeletewa  hadi tarehe 11 Machi, 2018 inaonyesha  kwamba,  jumla ya ng’ombe 16,744,355 kati ya 17,390,090 sawa na asilimia 96.3 ya ng’ombe wote nchini wamepigwa chapa. Aidha, jumla ya Punda 51,494 wamepigwa chapa nchini.


“Hivi karibuni nilitembelea mnada wa Pugu nikaangalia idadi ya mifugo iliyopigwa chapa hawafiki hata asilimia tano, lakini leo hapa sote tumeshuhudia idadi ya mifugo wote waliopigwa chapa katika mnada huu wa Kizota ni chini ya asilimia mbili. Minada hii ndiyo mikubwa nchini ukianzia wa Pugu na huu ni wa Kizota ni wa pili kwa hiyo inadhihirisha kwa uhakika kabisa kuwa kuna udanganyifu mkubwa unaofanywa na watendaji wasio waaminifu wanaopotosha taarifa.” Alisistiza  Mpina

Alisema wilaya nyingine zimeleta takwimu ambazo zinaonyesha zimepia chapa mifugo kwa zaidi ya asilimia elfu moja ambapo amezionya kutojiingiza katika matatizo kwa kuendelea kudanganya.

Aidha alisema tathmini ya jumla kuanzia mwezi Disemba 2017 hadi tarehe 11 Marchi, 2018 inaonyesha kwamba, Halmashauri 85 zimepiga chapa kwa asilimia 100 na zaidi; Halmashauri 86 zimepiga chapa kati ya asilimia 50 na 100, na Halmashauri 4 zimepiga chapa chini ya asilimia 50.

Alizitaja Halmashauri hizo kuwa ni Kasulu, Madaba, Arusha na Meru, ambapo alisema  Halmashauri zilizobaki ni miongoni mwa Halmashauri zenye ng’ombe wengi wa maziwa nchini wanaotarajiwa kuvishwa hereni. Halmashauri hizo ni Manispaa ya Ubungo, Temeke, Moshi, Kinondoni na Ilala.

Alisema Halmashauri zingine zenye ng’ombe wengi wa maziwa kuliko wanaochungwa ni Rungwe, Busokelo na Kibaha.

Alisema tathmini ya zoezi la chapa tangu kuongezwa kwa muda kutoka tarehe 31 Januari, 2018 hadi sasa inaonyesha ongezeko la Halmashauri 14 zilizopiga chapa mifugo zaidi ya asilimia 100 na kupungua kwa Halmashauri 8 zilizopiga chapa kati ya asilimia 50 – 100 na kupungua kwa Halmashauri 25 zilizopiga chapa chini ya asilimia 50.

“Napenda kutoa  maelekezo kwa wafugaji kwamba mifugo yote ipigwe chapa  popote ilipo ilimradi ni ya Tanzania  ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima  baada ya tarehe ya mwisho iliyopangwa na Serikali ambayo ni mwisho wa mwezi huu na  ninaomba ieleweke kuwa visingizio vyoyote  havitakubalika’ Alisisitiza Waziri Mpina.

Akielezea umuhimu wa zoezi hilo, Mpina alisema kwamba kukamilika kwa zoezi hilo kutasaidia kutambua mifugo yote iliyopo nchini ili kukidhi mahitaji  ya biashara katika masoko ya ndani na nje  ya nchi,kudhibiti magonjwa ya mifugo na kudhibiti wizi wa mifugo na usafirishaji holela.

Aidha kutasaidia  kuepusha  migogoro inayoendelea maeneo mbalimbaili nchini  baina ya wafugaji,wakulima pamoja na watumiaji wengine wa raslimali ardhi na kutawezesha Serikali kupata idadi sahihi ya mifugo iliyonayo ili kupanga kupanga mipango inayotekelezeka  na kuleta mapinduzi katika sekta hiyo.

Alisema  Zoezi la upigaji chapa ni endelevu kwa mifugo ambapo alisema ng’ombe na punda wanaotimiza  miezi sita wanatakiwa kupiga chapa.


Awamu ya kwanza ya zoezi la upigaji chapa ng’ombe na punda nchini ilianza rasmi tarehe 14 Desemba, 2016 kufuatia Agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu na ilitarajiwa kukamilika tarehe Desemba 31, 2017.  Tathmini iliyofanywa baada ya kukamilika awamu hiyo ya Desember, 2017 ilionyesha jumla ya ng’ombe 7,401,661 sawa na asilimia 38.5 ya lengo walikuwa wamepigwa chapa. Kutokana na kiwango kidogo cha ng’ombe waliokuwa wamepigwa chapa wakati huo, Waziri wa Mifugo, Mheshimiwa Luhaga Mpina aliongeza muda wa kukamilisha zoezi hili hadi tarehe 31 Januari, 2018. Hadi kufikia tarehe 31 Januari, 2018 jumla ya ng’ombe 15,192,565 sawa na asilimia 87.4 walikuwa wamepigwa chapa.


Aidha jumla ya punda 6,944 walikuwa wamepigwa chapa kati ya punda 572,353 wanaotarajiwa kupigwa chapa nchini. Pia, jumla ya ng’ombe wa maziwa 58,214 walikuwa wamevishwa hereni kati ya ng’ombe wa maziwa 782,995 wanaotarajiwa kuvishwa hereni. Pamoja na muda huo kuongezwa, Halmashauri nyingi zilikuwa bado hazijakamilisha zoezi hili kikamilifu. Kutokana na mapungufu mbalimbali yaliyojitokeza Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kasim Majaliwa Majaliwa alilazimika kuongeza muda zaidi mpaka tarehe 28 Machi, 2018 na kuziagiza Mamlaka ya Serikali za Mitaa kusimamia zoezi hili kikamilifu kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi na kumpa  taarifa ya Utekelezaji ifikapo Machi 31, mwaka huu.


Wakati huo huo, Waziri Mpina alisema kuwa  Wizara itafanya mageuzi makubwa ya kupanua kiwanda cha machinjio ya nyama  cha Dodoma(TMC) ili kiweze kukidhi mahitaji ya sasa  ya mifugo ambapo kumekuwa na ongezeko kubwa ya mifugo nchini.


Mmoja wa wafanyabiashara wa mifugo Shabani zuberi, alimweleza  Waziri kuwa  kwa sasa  gharama ya uchinjaji wa nyama katika machinjio ya kiwanda hicho ni juu ukilinganisha na machinjio nyingine nchini ambapo ni shilingi elfu ishirini   kwa ng’ombe mmoja  na kwamba  nyama kwa ajili ya soko la ndani inanyimwa sehemu ya kugandishia tofauti na nyama inayosafirishwa kwenda nje ya nchi suala ambalo linawafanya wapate  hasara kubwa  nyama ikishindwa kuuzika katika siku husika kutokana na kukosa sehemu ya kugandishia.


Akijibu hoja hizo, Mpina aliielekeza menejimenti ya kiwanda hicho kukaa na Wizara na kuangalia namna bora ya kuweka gharama ya uchinjaji itakayoendana na hali halisi ya bei la soko.


Aidha alikiagiza kiwanda kuanza mara moja kutoa huduma ya kugandisha na kuhifadhi nyama  ya walaji wa ndani ambapo pia alitoa wiki mbili kuhakikisha huduma ya maji inaletwa na kiwanda hicho katika machinjio ya Kizota.Alisisitiza kuwa Mnada wa Kizota utaboreshwa na Serikali kwa kuwa unaingiza milioni 624 kwa mwaka   hivyo ukiboreshwa miundo mbinu yake utaongeza mapato yake.


“Hatuwezi kuwajali watu kutoka nje ya nchi na usiwajali wananchi wako wa ndani ya nchi, naamuru kwamba TMC wapeni huduma ya kugandisha  nyama wateja wenu wa soko la ndani” alisistiza Mpina.


Alimpongeza Naibu Waziri, Abdalah Ulega kwa juhudi anazozifanya  za kuhakikisha minada yote nchi inakuwa  na  miundombinu bora ambapo awali Mhe. Ulega alitembelea mnada wa Kizota  na kujadiliana na wadau wa mnada huo kuhusiana na mambo mbalimbali.

Naye Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo Selina  Lyimo alimshukuru Waziri Mpina kwa maelekezo aliyoyatoa kwa Wizara na kumhakikishia kwamba yatatekelezwa mara moja ili kuleta mageuzi  na mapinduzi makubw a katika sekta.

Aidha Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti Mafunzo na Ugani,Angelo Mwilawa amesema  Idara yake itaendelea kuratibu tafiti mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo hususan kwenye eneo la malisho na uzalishaji wa mbegu bora za mifugo ili wafugaji waweze kufuga kisasa

No comments: