Wednesday, December 13, 2017

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA AFANYA ZIARA JIMBO LA NZEGA VIJIJINI

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza jambo na Mbunge wa jimbo la Nzega,Dkt Hamisi Kigwangalla,ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii mapema leo mara baada ya kuwasili kwa ziara fupi ndani ya jimbo la Nzega.kushoto kwake ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tabora Mzee Hassan Wakasuvi pamoja na Katibu wa CCM Wilaya Ndugu Shaibu Ngatiche.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifurahia jambo na Mbunge wa jimbo la Nzega,Dkt Kigwangalla,mapema leo walipokuwa wakishuhudia ngoma ya asili iliyokuwa ikitumbuiza nje ya Ofisi kuu ya chama  ya wilaya ya Nzega mara baada ya kuwasili kwa ziara fupi kufuatia mwaliko wa Mbunge wa jimbo hilo Dk Hamisi Kigwangalla.kushoto kwake ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tabora Mzee Hassan Wakasuvi
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tabora Mzee Hassan Wakasuvi akimkaribisha  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ndani ya Ofisi kuu ya chama  ya wilaya ya Nzega na kuitambulisha kamati kuu ya siasa ya Wilaya mapema leo kabla ya kwenda kwenye mkutano wa ndani wa jimbo hilo.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza mbele ya Kamati kuu ya Siasa Wilaya ya Nzega,mkoani Tabora mapema leo,mara baada ya kupokea taarifa fupi za chama ndani ya Ofisi kuu ya chama  ya wilaya hiyo 
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa ameongozana na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nzega Ndugu Amos Kanuda na viongozi wengine wa chama wakielekea kuweka jiwa la msingi la ujenzi wa Ukumbi utakaotumika kwa shughuli mbalimbali zikiwemo za kijamii,liliojengwa kando kando ya Ofisi kuu ya chama  ya wilaya
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuashiria uwekaji rasmi wa jiwe la msingi la ujenzi wa Ukumbi mkubwa na wa kisasa utakaotumika kwa shughuli mbalimbali zikiwemo za kijamii,uliojengwa kando kando ya Ofisi kuu ya chama  ya wilaya hiyo,kulia kwake ni  Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nzega Ndugu Amos Kanuda pamoja na Mbunge wa Jimbo hilo Dkt Hamisi Kigwangalla (aliyevaa mawani katikati).
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nzega Ndugu Amos Kanuda pamoja na Mbunge wa Jimbo hilo Dkt Hamisi Kigwangalla  wakipiga makofi mara baada ya kuwekwa jiwe la msingi la ujenzi wa ukumbi . 
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana, Mbunge wa Jimbo hilo Dkt Hamisi Kigwangalla,Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nzega Ndugu Amos Kanuda pamoja na  Katibu wa CCM Wilaya Ndugu Shaibu Ngatiche wakikagua ujenzi wa ukumbi huo . PICHA NA MICHUZI JR -NZEGA
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza mapema leo mbele ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM wilaya ya Nzega mkoani Tabora.Ndugu Kinana amefanya ziara wilayani humo mapema leo kwa Mwaliko wa Mbunge wa jimbo la Nzega Vijijini ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Hamisi Kigwangalla,aidha katika ziara hiyo Ndugu kinana amewapongeza viongozi mbalimbali waliochaguliwa katika ngazi ya chama ya wilaya na pia kuweka jiwe la Msingi la ujenzi wa ukumbi mkubwa wa kisasa ambao utatumika kwa matumizi mbalimbali.PICHA NA MICHUZI JR -NZEGA
 Baadhi ya Wafuasi wa chama cha CCM na Wananchi wakishangilia jambo walipokuwa wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mapema leo  wilayani Nzega mkoani Tabora.Ndugu Kinana amewasili Wilayani humo kwa ziara fupi ya Mwaliko wa Mbunge wa jimbo la Nzega Vijijini ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Hamisi Kigwangalla,aidha katika ziara hiyo Ndugu kinana amewapongeza viongozi mbalimbali waliochaguliwa katika ngazi ya chama ya wilaya na pia kuweka jiwe la Msingi la ujenzi wa ukumbi mkubwa wa kisasa ambao utatumika kwa matumizi mbalimbali.PICHA NA MICHUZI JR -NZEGA
Ndugu Kinana akiagana na baadhi ya Wananchama wa CCM waliofika kumpokea katika Makao Makuu ya Ofisi ya Wilaya hiyo mapema leo mchana.Ndugu Kinana anatarajiwa kuzungumza na wananchi wa jimbo la Nzega katika mkutano wa ndani wa jimbo hilo jioni ya leo.

No comments: