Na Teresia Mhagama
Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani ameeleza kuwa ukomo wa
kuunganishia umeme wateja walioomba kuunganishiwa huduma hiyo kwa muda
mrefu ni Agosti 30, 2017 na Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania
(TANESCO) atakayeshindwa kutimiza agizo hilo atashushwa cheo.
Dkt.
Kalemani aliyasema hayo kwa nyakati tofauti akiwa katika ziara ya
kuzindua mradi wa Usambazaji Umeme Vijijini wa Awamu ya Tatu katika
mikoa ya Rukwa, Ruvuma na Mtwara.
"Unakuta
kuna wateja wameomba kuunganishiwa umeme miezi kadhaa iliyopita lakini
mpaka sasa hawajaunganishwa wakati vifaa vipo, kwa hili lazima tuchukue
hatua kwa Meneja kama ni wa wilaya, mkoa, Kanda au Mkurugenzi
atayechelewa kuunganishia wateja Umeme," alisema Dkt. Kalemani.
Dkt. Kalemani alisema kuwa muda wa kumuunganishia mteja Umeme mara anapolipia huduma hiyo ni Siku Saba na si vinginevyo."Natambua kuna maeneo ambayo TANESCO mnafanya kazi vizuri lakini katika hili tutawajibishana," alisisitiza Dkt. Kalemani.
Wakati
huohuo. Dkt. Kalemani aliwaagiza watendaji wa TANESCO kuhakikisha kuwa
watu wote wanaofanya kazi ya kutandaza nyaya za umeme ndani ya nyumba
wawe wanatambulika na Shirika hilo ili kuondoa tatizo la vishoka kufanya
kazi hiyo pasipo ufanisi na baadaye kuleta madhafa kama ya moto.
Vilevile
aliwataka watendaji hao kutokukaa maofisini na badala yake wawafuate
wananchi sehemu walipo, suala ambalo litafanya Shirika hilo kuongeza
idadi ya wateja na kuwaondolea wananchi kero ya kutembea kwa umbali
mrefu kufuata huduma TANESCO.
Kuhusu
usimamizi wa mradi wa usambazaji Umeme Vijijini Awamu ya Tatu ambao
umeshaanza kutekelezwa nchini, Dkt Kalemani aliwataka watendaji wa
TANESCO kuhakikisha kuwa wanawasimamia wakandarasi wanaofanya kazi hiyo
usiku na mchana ili mradi ukamilike ndani muda uliopangwa.
Aidha
Dkt. Kalemani alitoa maagizo mbalimbali ambayo yanapaswa kutekelezwa na
wakandarasi wote waliopewa kazi ya kusambaza umeme vijijini katika
Mradi wa Awamu ya Tatu.
Naibu
Waziri aliwaagiza Wakandarasi hao kutoajiri wakandarasi wasaidizi
wanaotoka nje ya eneo lao la kazi ili wananchi wanaotoka katika maeneo
hayo wapate ajira na kutoa huduma mbalimbali kwa wakandarasi hao na
hivyo kujiongezea kipato.
Pia
aliwataka wakandarasi hao kutokuruka kijiji, kitongoji, sehemu
zinazotoa huduma muhimu kama mitambo ya maji, Shule, vituo vya afya na
sehemu za biashara, na nyumba ambazo tayari zimeshafanyiwa malipo ya
kuunganishwa na huduma ya umeme.
"
nisingependa kusikia Kituo cha Afya, Shule au Mitambo ya Maji imerukwa
na haijawekewa Umeme hivyo nichukue nafasi hii kuwashauri watendaji wa
Halmashauri nchini kutenga fedha kwenye Bajeti zao kwa ajili ya
kutandaza nyaya za Umeme kwenye sehemu hizo ili wakandarasi waweze
kuingiza Umeme," alisema Dkt. Kalemani.
Vilevile,
Dkt. Kalemani aliwataka wakandarasi hao kutoa malipo kwa wakandarasi
wadogo ndani ya wakati ili kuepusha mradi huo kusuasua na
kuwacheleweshea huduma wananchi.
Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani akizungumza na
wananchi (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa mradi wa kusambaza Umeme
Vijijini Awamu ya Tatu katika mkoa wa Ruvuma.
No comments:
Post a Comment