Friday, March 24, 2017

BALOZI WA KOREA AKABIDHI MAKTABA YA KISASA KWA SERIKALI YA TANZANIA

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Serikali ya Korea kupitia mradi wa ''Thank you Small Ribray program'' leo imekabidhi Vifaa na kuzindua maktaba ndogo ya kisasa katika ofisi za makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo balozi wa Korea nchini Song Geum Young amesema kuwa serikali yake licha ya kusaidia serikali katika miradi mingi lakini kwa sasa wameamua kusaidia katika kuwawezesha watoto kupata elimu inayoendana na wakati.

"sisi kama korea tunaamini kuwa ukimpa mtoto elimu umeweza kumpa maisha ya kesho, hivyo vifaa hivi vitaweza kuwasaidia katika kukuza taaluma yao " amesema Balozi.Balozi ametoa wito kwa wazazi kuwaleta watoto waweze kutumia maktaba hiyo kwa kutumia sehemu hiyo kwa ajili kukuza taaluma yao .
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo akiwa na Balozi wa Korea nchini , Song Geum Young na Mama Anna Abdalah Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Makumbusho ya Taifa wakikata utepekuashiria uzinduzihuo.

Balozi wa Korea nchini , Song Geum Young akizungumza kabla ya uzinduzi wa wa Maktaba ya kisasa ambayo imetolewa na Serikali ya korea.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo, akikabidhi vitabu kwa Mwenyekiti wa bodi ya Makumbusho ya Taifa , Mama Anna Abdalah
Mkurugenzi Mtendaji wa Makumbusho ya Taifa , Audax Mabula akizungumza kabla ya uzinduzi wa Maktaba ya Kisasa katika Makumbusho ya Taifa.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo akizungumza kabla ya uzinduzi wa Maktaba ya Kisasa katika ukumbi wa Makumbusho ya taiafa kwa msaada wa Serikali ya watu wa Korea.
Baadhi ya wadau walioshiriki tukio hilo
Viongozi mbalimbali akiwemo na balozi mteule wa korea wakifatia hotuba ya balozi
Wanafunzi wa shule ya Msingi Bunge wakishuhudia tukio hilo
Mwenyekiti wa bodi ya Makumbusho ya Taifa , Mama Anna Abdalah akizungumza na waandishi wa habari 

Wanafunzi wa shule ya Msingi Bunge wakitumia baadhi ya vifaa vilivyopo katika Maktaba ya Kisasa ndani ya ukumbi huo wa makumbusho ya Taifa

Wanafunzi wa shule ya Msingi Bunge wakitumia baadhi ya vifaa vilivyopo katika Maktaba ya Kisasa ndani ya ukumbi huo wa makumbusho ya Taifa

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo akiwa na Balozi wa Korea nchini , Song Geum Young wakipata maelekezo jinsi ya namna vifaa vya kielektronic vinavyofanya kazi katikakutoa elimu kwa watoto ndani ya maktaba hiyo ambayo imefadhiliwa na serikali ya Korea

Picha ya pamoja ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo akiwa na Balozi wa Korea nchini , Song Geum Young na Mama Anna Abdalah wageni waalikwa wengine waliohudhuria katika hafla hiyo

No comments: