Saturday, November 19, 2016

WAZIRI SIMBACHAWENE AFUNGA MAFUNZO YA UONGOZI NA MAADILI YA VIJANA WAZALENDO 47 KIVUKONI JIJINI DAR ES ESALAAM

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene, akisalimiana na Katibu Mkuu mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilson Mukama, baada ya kuwasili Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kufunga mafunzo ya uongozi na maadili ya vijana wazalendo 47 yalifungwa chuoni hapo Dar es Salaam leo. Kulia ni Samuel Kasori, aliyekuwa Msaidizi wa Hayati Baba wa Taifa ambaye alipata fursa ya kuzungumza katika hafla hiyo kuhusu suala zima la maadili ya uongozi na uzalendo.
Kikao kifupi kikifanyika ofisini kwa mkuu wa chuo hicho 
kabla ya kwenda ukumbini.
Wanafunzi wa chuo hicho wakiwa ukumbini kwenye hafla hiyo.

 
 
Mgeni rasmi Waziri Simbachawene (wa pili kushoto) na viongozi wengine wakielekea ukumbini. Kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filbert Sanga, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Wilson Mukama na Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Profesa Shadrack Mwakalila.
Wimbo wa Taifa ukiimbwa.
Wimbo wa Taifa ukiimbwa.
Taswira ya ukumbi wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filbert Sanga akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mbunge wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile akizungumza.
Mzee Samuel Kasori, aliyekuwa Msaidizi wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere akizungumza kwenye hafla hiyo.
Wahitimu hao 47 wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Wahitimu hao 47 wakiimba wimbo maalumu.
Waziri Simbachawene akihutubia.
Muhitimu, Ebeneza Emmanuel akipokea cheti kutoka kwa 
mgeni rasmi.
Petro Magoti akikabidhiwa cheti.
Mhitimu Happiness Agathon akipokea cheti.
Mzalendo Theodora Malata akipokea cheti.
Mgeni rasmi katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali.
Picha ya pamoja na wahitimu hao.


Na Dotto Mwaibale
 
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene amesema ili kusimamia mabadiliko na maendeleo ya nchi na maadili inatakiwa kuwa na kiongozi mbabe na mtemi.
 
Simbachawene aliyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya uongozi na maadili kwa wahitimu 47 wazalendo waliyoyapata Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere Kivukoni Kigamboni jijini Dar es Salaam baada ya kumaliza kazi ya ujenzi ya kujitolea ya mwezi mmoja wilayani Mkuranga mkoani Pwani.
 
Alisema ili kusimamia mabadiliko na maendeleo nchi inatakiwa kuwa na mtu mbabe na mtemi na si kutegemea kundi fulani la watu kwani kwa kufanya hivyo kila kundi litahitaji kupendelewa baada ya kujiona bora kuliko jingine.
 
Alisema bila kuwa na viongozi wenye maadili nchi haiwezi kusonga mbele kwani tangu kuachwa kwa vijana kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ambako kulikuwa kukitolewa mafunzo ya maadili athari zake zilijitokeza na ndipo kwa kipindi cha miaka 20 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilijikuta kikivamiwa na matajiri wakitaka nafasi mbalimbali za uongozi katika ngazi za ubunge, urais na kuingia katika ujumbe wa mkutano mkuu wa chama kwa njia ya fedha.
 
“Napenda kusema kuwa tunahitaji mabadiliko makubwa ya kukifumua chama chetu hasa katika mfumo mzima wa kupata viongozi kwani uliopo umetufanya tupoteze baadhi ya nafasi katika majimbo na hata katika uchaguzi ndogo kutokana na mfumo mbaya tulishindwa vibaya baada ya wanachama wetu kumpigia kura mtu mwingine kwa hasira huko vikao vyote vikiendeshwa kwa misingi ya fedha” alisema Simbachawene.
 
Alisema ilifika kila jambo lilikuwa haliwezi kufanyika bila ya kuomba ufadhili kutoka kwa matajiri ambao wengi wao ndio hao walikuwa wakwepa kodi.
 
Aliongeza kuwa watumishi wa umma wamekuwa wakilalamika kuwa hali ya maisha imekuwa ngumu huku wengine wakisema hazina hakuna fedha wakati hakuna hata mwezi mmoja ambao mtumishi amekosa kupewa mshahara wake.
 
Alisema pengine hali hiyo inatokea kwa kuwa watumishi hao walikuwa wakitegemea kitu kingine mbali ya mshahara baada ya mianya hiyo kufungwa ndio maana wameanza kulalamika.
 
Simbachawene alisema awali bandarini kulikuwa na pilika pilika nyingi mlundikano wa mankotenta na magari lakini makusanyo yalikuwa hayafiki hata bilioni moja kwa mwezi lakini hivi sasa pilika pilika hizo hazipo tena makusanyo yanafikia trioni  moja hii inaonesha pamoja na kuwepo kwa pilika pilika hizo kodi ilikuwa hailipwi ipasavyo.
 
Alisema nchi ilifikia pabaya kwani kila sehemu kulikuwa na madalali iwe hospitali, ofisi za serikali, mahakamani na hata kupata cheo lakini hivi sasa mambo hayo yamebanwa.
 
 Alisema anachokifanya Rais John Magufuli ni mabadiliko ili watu waache kuishi kwa mazoea badala yake wafanye kazi ili nchi ipige hatua katika masuala yote.
 
Simbachawene alisema changamoto kubwa iliyopo ni kuchanganya sera za siasa na za uongozi jambo linalosabisha mambo mengine kushindindwa kusonga mbele.


Waziri Simbachawene aliwapongeza wahitimu hao kwa kuwa na uzalendo kwa nchi yao ambapo aliahidi majina yao kuyapeleka kwa Rais Dk. John Magufuli kuona jinsi ya kuwasaidia ukizingatia kuwa wote ni wasomi wa shahada ya kwanza katika ngazi ya taaluma mbalimbali na akawaomba vijana wengine kuiaga mfano wa vijana hao.

Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Profesa Shadrack Mwakalila alisema baada ya kuona mmomonyoko wa maadili miongoni mwa jamii ya watanzania hasa kwa baadhi ya viongozi chuo hicho kimeona ni vyema kurejesha tena mafunzo ya uongozi na maadili ili kupitia mafunzo hayo waweze kupunguza kama si kumaliza kabisa kasi ya mmomonyoko wa maadili iliyopo kwa sasa.

No comments: