Tuesday, November 29, 2016

ITEL TANZANIA YATOA MSAADA WA VIFAA VYA SHULE KWA WANAFUNZI WA SHULE YENYE MAHITAJI MAALUM

Wawakilishi kutoka katika kampuni ya simu ya ITEL Tanzania wakiongozwa na Afisa masoko wa kampuni hiyo Charles charle  wa katikati na Asha Mzambili ambaye ni afisa masoko msaidizi wa ITEL wakiwasili katika viwanja vya shule ya msingi ya Airwing iliyopo Jijini Dar es salaam wakati kampuni hiyo ilipotoa misaada ya vifaa mbalimbali kwa wanafunzi wa Kitengo maalum kilichopo.

 Katika shule hiyo vifaa mbalimbali vimetolewa na kampuni hiyo vikiwemo madaftari kwa ajili ya wanafunzi ,mabegi,na vifaa vingine ambavyo vitawasaidia wanafunzi wa shule hiyo ambao wana mahitaji maalum.
Vifaa mbalimbali vya shule Vilivyotolewa na Kampuni ya ITEL Tanzania leo kwa ajili ya wanafunzi wa Kitengo maalum ambao wana ulemavu wa akili wanaosoma katika shule ya msingi Airwing Jijini Dar es salaam 
Mwanafunzi Linus Alphonce wa shule ya Msingi Air wing Jijini Dar es salaam ambaye yupo kitengo maalum akipokea vifaa mbalimbaloi kutoka kwa mwakilishi wa Kampuni ya ITEL Sarphon Asajile wakati kampuni hiyo ilipokuwa ikitoa msaada mbalimbali katika shule hiyo 

Mwanafunzi Yasin Membe ambaye anasoma katika shule ya msingi Airwing kitengo maalum akipokea msaada wa vifaa mbalimbali kutoka kamouni ya ITEL Tanzania leo Jijini Dar es salaam 
Afisa masoko wa kampuni ya Itel Tanzania Charles Charle akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam wakati kampuni hiyo ilipofika katika shule ya msingi Airwing Primary kwa ajili ya kuta msaada wa vifaa mbalimbali vya kimasomo kwa wanafunzi wanaosoma katika kitengo maalum shuleni hapo ambapo afisa Huyo amesema kuwa kampuni ya ITEL imejipanga kuendelea kuwasaidia watoto hao wenye uhitaji maalum na wataendelea kuwasaidia kila wakati huku akiwataka watanzania wengine kuwa na moyo wa kutoa kidogo wanachopata kwa watanzania wanaohitaji msaada wao.

Aidha amesema kuwa Msaada walioleta leo una thamani ya shilingi laki Tano ambapo umenunua vifaa mbalimbali kama Mabegi kwa wanafunzi hao,madaftari,Mathematical set,na vifaa vingine vidogo vidogo kwa ajili ya kuwasaidia watoto hao katika masomo yao.
Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Air wing Mwalimu Fabiola Malisa akitoa shukrani zake kwa kampuni ya Itel kwa kuwakumbuka watoto hao wenye uhitaji katika shule yake,
Katika shukrani zake amesema kuwa Tangu  Sera mpya ya elimu ipitishwe na kuwataka watoto wote kupelekwa shule kumekuwa na ongezeko kubwa la watoto wa aina hiyo katika shule yake ambapo walitoka watoto hamsini na sasa sabini hiyo akawataka watanzania mbalimbali kuendelea kuwakumbuka watoto hao katika misaada ili kuwapa moyo na kuwafariji 












No comments: