Thursday, November 17, 2016

ASASI ZA KIDINI PAMOJA NA ASASI ZA KIRAIA ZATAKIWA KUWEKEZA KATIKA HUDUMA ZA KIJAMII.


   Na,Abel Daud,Globu ya Jamii- Kgoma.

Katika kuepuka vifo vya mama wajawazito na watoto,wazazi wameshauriwa kutotumia dawa za asili sambamba na kuwahi kufika katika vituo vya afya ili kuokoa maisha ya mama wajawazito na watoto.

Rai hiyo imetolewa na Daktari mfawidhi wa kituo cha afya Nguruka Dkt.Stanford Chamgeni ,wakati akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Bi,Mwanamvua Mlindoko katika kukabidhiwa jengo la maternity ward lililopo katika kijiji cha Mganza kata ya Mganza Wilayani Uvinza lenye dhamani ya tsh.30 million,lililotolewa na Kanisa la POOL OF SLOAM.

Naye Kuhani ISRAEL EXTRA POWER,ambaye alimwakilisha kiongozi mkuu wa kanisa hilo hapa nchini,alisema kuwa kupitia hatua hiyo ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za serikali katika kukamilisha huduma za kijamii.

Akinukuu maneno ya kitabu cha Isaya 58 aya ya 7 na Yakobo 2-14,Kuhani ISRAEL POWER alieleza kuwa,sehemu ya kusaidia maisha ya wenye uhitaji lazima kuwepo na umoja kwa viongozi na jamii kwa ujumla,sambamba na kuongeza kuwa,kwa kuwa MUNGU hana upendeleo,kama kanisa ni lazima kuendelea kuona uchungu wa kuhudumia jamii.

Kwa upande wake Afisa mtendaji wa kata ya Mganza Bw,BONIFACE BAHINGAI,ametoa shukurani kwa kanisa hilo ambapo alisema kuwa kuwepo sasa kwa ward hiyo,itasaidia kutatua changamoto zilizokuwepo kijijni humo,sambamba na kutoa wito kwa taasisi zingine za kidini kuona umuhimu kusaidia huduma za kijamii.

Nao baadhi ya wananchi kijijini humo akiwemo DAFROZA GWIMO,alitanabaisha kuwa uwepo sasa wa ward hiyo itawarahisishia kuondoa changamoto iliyokuwepo ya kwenda kujifungulia mbali,na kupelekea kuhatarisha maisha ya mama mjamzito na mtoto.
Waumini wa kanisa hilo pamoja na wanakijiji wakiwa wamelizunguka jengo hilo
 Kuhani Israel Extra Power akiongea na wana kijiji pamoja na waumini waliohudhuria sherehe hiyo
Mwakilishi wa Mkuu wa wilaya pamoja na Kuhani Israel Power wakielekea kwenye jengo tyr kwa uzinduzi
 Kuhani Israel Power akimkabidhi ufunguo wa jengo hilo Mwakilishi wa mkuu wa Wilaya Dr.Chamgeni
Kuhani Israel  pomoja na Dr.Chamgeni wakifunua kitambaa kilichofunika jiwe la msingi kuashiria ufunguzi wa jengo hilo

No comments: