Wednesday, October 26, 2016

WIZARA YA HABARI YAPOKEA VIFAA VYENYE THAMANI ZAIDI YA SH.MILIONI 20 KUTOKA UBALOZI WA CHINA NCHINI.



. Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw. Petro Lyatuu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa makabidhiano ya Vifaa vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20 kutoka Ubalozi wa China nchini kwa ajili ya maendeleo ya Sekta ya Sanaa leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Wizara hiyo ,kushoto ni Mshauri wa masuala ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China Bw.Gao Wei, na Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Sanaa Bibi Leah Kihimbi.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw. Petro Lyatuu akipokea Luninga kutoka kwa Mshauri wa masuala ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China hapa nchini Bw Gao Wei wakati wa makabidhiano ya. Vifaa vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20 kutoka Ubalozi wa China nchini kwa ajili ya maendeleo ya Sekta ya Sanaa leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Wizara hiyo , kulia ni Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Sanaa Bibi Leah Kihimbi.

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw. Petro Lyatuu (Katikati ) akimshukuru Mshauri wa Masuala ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China Bw Gao Wei kutokana na msaada wa Vifaa walivyotoa kwa Wizara kwa ajili maendeleo ya Sekta ya Sanaa leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Wizara hiyo, kulia ni Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Sanaa wa Wizara Bibi Leah Kihimbi.
Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Sanaa wa Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi (Kulia) akitoa neno la Shukrani kwa Ubalozi wa China hapa nchini baada ya kupokea Vifaa vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20 kutoka Ubalozi wa China nchini kwa ajili ya maendeleo ya Sekta ya Sanaa leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Wizara hiyo ,katikati ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara Bw. Petro Lyatuu, na kulia ni Mshauri wa Masuala ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China Bw. Gao Wei.

…………………………………………………………………..

Na Shamimu Nyaki-WHUSM.

Ubalozi wa China nchini umeipatia Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo vifaa vya ofisi vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20 ikiwa ni kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya Serikali hizo mbili.

Hatua hiyo imekuja ikiwa na lengo la kusaidia katika kukuza na kuendeleza sekta ya sanaa ambayo katika mpango wa miaka mitano ya maendeleo ya Serikiali inatakiwa kuongeza ajira pamoja na pato la taifa kupitia kazi mbalimbali za sanaa.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo leo Jijini Dar es Salaam Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw. Petro Lyatuu aliushukuru Ubalozi huo kwa mchango wao wa kuhakikisha sekta ya sanaa inakuwa na kuleta mabadiliko nchini.

“Tunashukuru Ubalozi wa China kwa kutupatia vifaa hivi ambavyo vitasaidia sana utendaji katika Sekta ya Sanaa ambayo inaendelea kukua kwa kasi hapa chini na kusaidia kuimarisha ushirikiano mzuri baina ya Serikali yetu na China”Alisema Bw. Petro Lyatuu.

Naye Mshauri wa masuala ya Utamaduni kutoka Ubalozi huo Bw Gao Wei amesema kwamba China itaendelea kutoa ushirikiano kwa Wizara katika kuendeleza Sanaa kwa kutoa misaada mbalimbali kwa kadri itakavyohitajika.

“Tutaendelea na ushirikiano huu sio tu kwa kutoa msaada wa vifaa bali pia kubadilishana uzoefu na taaluma ya Sanaa ili Sekta hii ikue na kuheshimika na kutambulika rasmi kama ajira ”Alisema Bw Gao.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa Bibi Leah Kihimbi amesema kuwa vifaa hivyo vitaimarisha utendaji kazi wa Sekta ya Sanaa ukizingatia kuwa ni Sekta ambayo imebeba dhamana kubwa ya kutangaza Sanaa ndani na nje ya nchi.

Vifaa vilivyotolewa na Ubalozi wa China ni pamoja na Komputa 4,Komputa Mpakato 1,Kamera ya video moja na Luninga vyote vikiwa na jumla ya dhamani zaidi ya milioni 20.

No comments: