Monday, October 10, 2016

WAZIRI MHAGAMA ATOA MAAGIZO KWA HALMASHAURI NCHINI.


Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama, akizungumza na Vijana na Wananchi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.
 Baadhi ya Vijana wa Mkoa wa Simiyu wakionesha mabango yenye jumbe mbalimbali kwa Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Wiki ya Vijana Mjini Bariadi.
Kikundi cha Brass Band cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mgulani Dar es Salaam wakiwaongoza vijana katika maandamano ya amani kuelekea uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi ambapo wiki ya vijana imezinduliwa rasmi leo.
  Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama (wa tano kushoto) viongozi mbalimbali ngazi ya taifa na Mkoa wakipokea maandamano ya vijana katika Uzinduzi wa Wiki ya Vijana,  Uwanja wa Sabasaba Mjni Bariadi.
 Baadhi ya Vijana wa Mkoa wa Simiyu wakiwa wamebeba  bango wakielekea uwanja wa Sabasaba,Mjini Bariadi mahali ulipofanyika Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitifa mwaka 2016.
 Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama, akivishwa skafu na vijana wa skauti wa Mkoa wa Simiyu kabla ya kupokea maandamano ya amani ya vijana katika Uzinduzi wa Wiki ya Vijana,  Uwanja wa Sabasaba Mjni Bariadi.
Picha four:Kikundi cha Brass Band cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mgulani Dar es Salaam wakiwaongoza vijana katika maandamano ya amani kuelekea uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi ambapo wiki ya vijana imezinduliwa rasmi leo.
Vijana wa Halaiki wakiwa katika katika maandamano ya amani kuelekea uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi ambapo wiki ya vijana imezinduliwa rasmi leo.

Na Stella Kalinga Simiyu.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama ameziagiza halmashauri zote nchini ambazo hazijatenga maeneo kwa ajili ya vijana kufanya hivyo mara moja.
Mbali na hilo Mhagama ameziagiza halmashauri nchi nzima kuhakikisha zinafungua na kuanzisha SACCOS za Vijana na kuzisimamia ili vijana wapate mikopo yenye masharti nafuu, ikiwa pamoja na kuhakikisha zinatenga asilimia 5 ya mapato ya ndani kama inavyotakiwa.
Waziri Mhagama alitoa maagizo hayo Mkoani Simiyu wakati akiongea na mamia ya wananchi na vijana wa Mkoa huo mjini Bariadi katika ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya vijana Kitaifa yanayofanyika mkoani hapa.

Mhagama amesema kuwa mpaka sasa ni halmashauri 72 zimeshatenga hekari 84037 kati 185 kwa ajili ya vijana katika shughuli za kilimo, ufugaji na kibiashara, ili kuweza kujiletea maendeleo ya kiuchumi.

“ ..kupitia maadhimisho haya ninaagiza halmashauri zote nchini ambazo zinafahamu bado hazijatenga maeneo haya kuhakikisha wanatenga mara moja…na kuwapatia vijana kwa ajili ya kufanya shughuli hizo” Alisema Waziri
Aidha Waziri huyo aliongeza kuwa bado kuna halmashauri nchini zimeshindwa kutekeleza maagizo ya serikali ya kuanzisha SACCOS za Vijana, ambapo mpaka sasa ni halmashauri 113 tu ambazo zimeanzisha SACCOS hizo kati ya 185, huku zikiwa zimetenga jumla ya shilingi Bilioni.3.9 kwa mwaka wa fedha 2016/17 na akazitaka halmashauri zingine kuanzisha SACCOS hizo na kutenga fedha za Vijana mara moja.
Awali akimkaribisha Waziri huyo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwa mkoa huo umeanza kutekeleza kwa vitendo agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli la kuifanya Tanzania kuwa ya viwanda kwa kuanzisha viwanda viwili vidogo; kiwanda cha kutengeneza chaki kilichopo wilaya ya Maswa na  cha kusindika Maziwa kilichopo Meatu.
Mtaka amesema Serikali mkoani humo imedhamiria kuufanya mkoa huo kuwa wa mfano na kuwa miongoni mwa mikoa mitano ya kutumainiwa kibiashara ambao viongozi mbalimbali wataenda kujifunza namna unavyotekeleza.
Hata hivyo Waziri Mhagama alimpongeza Mkuu wa mkoa huyo na kusema kuwa amekuwa kiongozi wa kwanza kutekeleza agizo la Rais, na kumuahidi kuwa ofisi ya Waziri Mkuu iko tayari kusaidia juhudi hizo hata kwa kutoa fedha za kuwawezesha vijana.
Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia wenye ulemavu amewataka Wakuu wa mikoa , wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa Halmashauri kote nchini  kuwa chachu  na kiungo muhimu katika  kuandaa na kutekeleza mikakati ya kutokomeza unyanyapaa na vitendo vya ukatili,  wanavyofanyiwa watu wenye ualbino ili nao waweze kufanya shughuli za maendeleo bila uoga kama ilivyo kwa baadhi yao.
Wiki ya vijana itahitimishwa pamoja na Mbio za Mwenge wa Uhuru na Kumbukumbu ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere, tarehe 14 Oktoba, 2016 Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.

No comments: