Wednesday, October 12, 2016

WAZIRI LUKUVI. HAKUNA MAKAZI HOLELA YATAKAYOBOMOLEWA JIJINI MWANZA.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Willium Lukuvi, akizungumza na wakazi wa Kata ya Buhongwa Jijini Mwanza, alipofanya ziara Jijini Mwanza hii leo.

Waziri ameziagiza halmashauri za Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza, kuhakikisha zinakamilisha zoezi la upimaji na urasimishaji makazi yaliyojengwa kiholela hadi ifikapo june 30 mwakani.
Na BMG
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Willium Lukuvi, akizungumza na wakazi wa Kata ya Buhongwa Jijini Mwanza, alipofanya ziara Jijini Mwanza hii leo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Willium Lukuvi, akimkabidhi hati ya umiliki wa ardhi na makazi mmoja wa wakazi wa Kata ya Buhongwa Jijini Mwanza ambaye makazi yake yamerasimishwa kutoka makazi holela baada ya zoezi la upimaji kufanyika.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Willium Lukuvi, akimkabidhi hati ya umiliki wa ardhi na makazi mmoja wa wakazi wa Kata ya Buhongwa Jijini Mwanza ambaye makazi yake yamerasimishwa kutoka makazi holela baada ya zoezi la upimaji kufanyika.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Willium Lukuvi, akizungumza na watendaji mbalimbali Jijini Mwanza (Ilemela na Nyamagana).
Baadhi ya Watendaji na Madiwani wa Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza
Baadhi ya Watendaji na Madiwani Jijini Mwanza
Pia Waziri Lukuzi amempandisha cheo aliyekuwa Afisa Mipango na Maendeleo ya Jiji la Mwanza, Deogratius Kalimerize, kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mipango Miji na Vijijini Kanda ya Ziwa. 

Ni baada ya kuridhishwa na kazi yake ya usimamiaji na uandaaji wa Mpango Kabambe wa Jiji la Mwanza wa mwaka 2015-3015 ambao umelenga kulifanya Jiji la Mwanza kuwa kitovu cha kiuchumi na biashara katika nchi za maziwa makuu.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, akizungumza kwenye mkutano huo baina ya waziri Lukuvi na watendaji mbalimbali wa Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela.
Watendaji na wananchi wa Kata ya Buhongwa wakimsikiliza waziri Lukuvi (hayupo pichani).
**********************
Na George Binagi-GB Pazzo
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Willium Lukuvi, ameziagiza halmashauri za Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza, kuhakikisha zinakamilisha zoezi la upimaji na urasimishaji makazi yaliyojengwa kiholela hadi ifikapo june 30 mwakani.

Waziri Lukuvi ametoa agizo hilo hii leo Jijini Mwanza alikofanya ziara ya kujionea utekelezaji wa urasimishaji makazi yaliyoendelezwa kiholela Jijini Mwanza ambapo amebainisha kwamba Serikali haina mpango wa kuwavunjia wananchi makazi yaliyojengwa kiholela na badala yake imeandaa mpango huo ili kutambua makazi hayo na kuwapatia wananchi hati miliki ya makazi yao.

Aidha amewatahadharisha wananchi kwamba, mpango wa kurasimisha makazi yaliyojengwa kiholela hautayahusisha makazi yaliyojengwa kwenye maeneo hatarishi ikiwemo kwenye mabonde, miinuko, mafuriko pamoja na hifadhi za barabara.

Baadhi ya wananchi Jijini Mwanza ambao makazi yao yamerasimishwa na kupewa hati ya umiliki, wameipongeza serikali kwa hatua hiyo ambapo wameomba kasi ya zoezi hilo kuongezeka ili wananchi zaidi ya elfu 35 ambao makazi yao hayajapimwa, yaweze kupimwa na kupatia hati za umiliki kwa wakati kama Waziri Lukuvi alivyoagiza.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, amemuhakikishia Waziri Lukuvi kwamba hadi kufikia mwezi Januari mwaka ujao, zoezi la kupima makazi yaliyojengwa kiholela na kuyarasimisha katika Jiji la Mwanza na Maspaa ya Ilemela, litakuwa limekamilika.

No comments: