Tuesday, October 25, 2016

TANZANIA YAPATA MKOPO WENYE MASHARTI NAFUU WA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 300 KUTOKA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA (afdb) NA SERIKALI YA KOREA

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (wa nne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri wenzake wa Fedha kutoka nchi 54 za Kiafrika, wanaohudhuria Mkutano wa 5 wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na nchi za Afrika (KOAFEC), unaofanyika Jijini Seoul, Korea Kusini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo Afrika anayeiwakilisha Tanzania (AfDB) Dkt. Nyamajeje Weggoro (katikati) wakimsikiliza kwa makini Raisi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kabla ya kuanza kwa mkutano unaojadili namna kilimo na mapinduzi ya viwanda vinavyoweza kuibadili Afrika Kiuchumi na Kijamii wakati wa Mkutano wa 5 wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na nchi za Afrika (KOAFEC) unaofanyika Jijini Seoul, Korea Kusini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (kulia) akitia saini makubaliano ya uteuzi wa mradi utakao fadhiliwa kwa pamoja kati ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Serikali ya Korea, wenye thamani ya dola Milioni 50 za Marekani sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 100.18 zitakazotumika kujenga njia ya usafirishaji umeme kwanjia ya gridi ya Taifa, yenye msongo wa kV 400 katika ukanda wa kaskazini Magharibi itakayoanzia mkoani Mbeya, Nyakanazi hadi Mkoani Kigoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (katikati) akiwa na Mawaziri wenzake kutoka nchi za Kenya, Uganda na Ethiopia (wengine hawako Pichani) wakionesha kwa waandishi wa habari (hawako pichani pia) nyaraka za makubaliano ya uteuzi wa mradi utakao fadhiliwa kwa pamoja kati ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Serikali ya Korea, wenye thamani ya dola Milioni 50 za Marekani sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 100.18 zitakazotumika kujenga njia ya usafirishaji umeme kwa njia ya gridi ya Taifa, yenye msongo wa kV 400 katika ukanda wa kaskazini Magharibi kwa upande wa Tanzania itakayoanzia mkoani Mbeya, Nyakanazi hadi Mkoani Kigoma. wakati wa Mkutano wa 5 wa ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na nchi za Kiafrika, unaoendelea Jijini Seoul Korea Kusini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), kushoto, na Mwenyekiti ambaye pia ni Rais wa Benki ya EXIM ya Korea Kusini, Lee Duk-Hoon, wakitia saini Mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za marekani milioni 90.092 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 194 za Tanzania, kwa ajili ya mradi wa Upanuzi wa Miundombinu ya mfumo wa maji taka Jijini Dar es salaam, wakati wa Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na nchi za Afrika, unaoendelea Jijini Seoul, Korea Kusini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), kushoto, na Mwenyekiti ambaye pia ni Rais wa Benki ya EXIM ya Korea Kusini, Lee Duk-Hoon, wakipeana mikono baada ya kusaini Mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za marekani milioni 90.092 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 194 za Tanzania, kwa ajili ya mradi wa Upanuzi wa Miundombinu ya mfumo wa maji taka Jijini Dar es salaam, wakati wa Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na nchi za Afrika, unaoendelea Jijini Seoul, Korea Kusini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), kushoto, na Mwenyekiti ambaye pia ni Rais wa Benki ya EXIM ya Korea Kusini, Lee Duk-Hoon, wakionesha mkataba waliousaini wa mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za marekani milioni 90.092 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 194 za Tanzania, kwa ajili ya mradi wa Upanuzi wa Miundombinu ya mfumo wa maji taka Jijini Dar es salaam, wakati wa Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na nchi za Afrika, unaoendelea Jijini Seoul, Korea Kusini.
Baadhi ya wajumbe kutoka Tanzania na Korea walioshuhudia utiawaji saini wa mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za marekani milioni 90.092 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 194 za Tanzania, kwa ajili ya mradi wa Upanuzi wa Miundombinu ya mfumo wa maji taka Jijini Dar es salaam, wakati wa Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na nchi za Afrika (KOAFEC), unaoendelea Jijini Seoul, Korea Kusini. (Picha zote na Benny Mwaipaja-Wizara ya Fedha na Mipango)​

No comments: