Tuesday, October 11, 2016

MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA KIKE DUNIANI: BARAZA LA WOTOTO MKOANI MWANZA LATAKA MTOTO WA KIKE KUPEWA FURSA SAWA KATIKA JAMII

Mwenyekiti wa Baraza la Watoto mkoani Mwanza, Paulina Mashauri, akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani ambayo Jijini Mwanza yamefanyika hii leo Oktoba 11, katika Uwanja wa Furahisha na kuwashirikisha watoto kutoka shule na taasisi mbalimbali.
Na BMG
Haleluya Benjamin ambaye ni Katibu wa baraza la Watoto mkoani Mwanza, akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani ambayo Jijini Mwanza yamefanyika hii leo Oktoba 11, katika Uwanja wa Furahisha na kuwashirikisha watoto kutoka shule na taasisi mbalimbali.
Mwanafunzi James John kutoka shule ya msingi Kitangiri A Jijini Mwanza akizumzia Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani ambayo Jijini Mwanza yamefanyika hii leo Oktoba 11, katika Uwanja wa Furahisha ambapo amesema haungi mkono baadhi ya vitendo wanavyofanyiwa watoto wa kike ikiwemo unyanyasaji kama vile ubakaji, mimba na ndoa za utotoni.
Msimamizi wa Watoto Baraza la Watoto mkoani Mwanza, Karus Masinde, akizungumza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani ambayo Jijini Mwanza yamefanyika hii leo Oktoba 11, katika Uwanja wa Furahisha na kuwashirikisha watoto kutoka shule na taasisi mbalimbali.
Mmoja wa vijana walioshiriki kwenye Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani ambayo Jijini Mwanza yamefanyika hii leo Oktoba 11, katika Uwanja wa Furahisha na kuwashirikisha watoto kutoka shule na taasisi mbalimbali.
Wanafunzi wasichana wakiigiza michezo na maigizo mbalimbali
Wanafunzi wasichana wakiigiza michezo na maigizo mbalimbali
Kulikuwa na matukio mbalimbali ikiwemo wanafunzi kuonesha uwezo wao wa kujibu maswali
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi akitoa ufafanuzi wa jambo

Na George Binagi-GB Pazzo
Baraza la Watoto mkoani Mwanza limeitaka jamii kutoa fursa sawa ya malezi bora kwa watoto wa kike kama ilivyo kwa watoto wa kiume katika masuala mbalimbali ikiwemo fursa ya kupata elimu.
Mwenyekiti wa baraza hilo, Paulina Mashauri, ameyasema hayo kwenye Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani ambayo Jijini Mwanza yamefanyika katika Uwanja wa Furahisha na kuwashirikisha watoto kutoka shule na taasisi mbalimbali.
Naye Haleluya Benjamin ambaye ni Katibu wa baraza hilo amesema bado watoto wa kike wanakabiriwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kukosa fursa ya kupata elimu, mimba na ndoa za utotoni hivyo ni vyema jamii ikaungana pamoja katika kutokomeza changamoto hizo.
Msimamizi wa Watoto Baraza la Watoto mkoani Mwanza, Karus Masinde, ameiomba jamii na serikali kwa ujumla kutoa kipaumbele kwa watoto wa kike katika masuala mbalimbali ikiwemo ya kupata elimu pamoja na fursa za kiuongozi.
Kitaifa Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani yamefanyika mkoani Shinyanga yakiambatana na kauli mbiu isemayo, Msichana Kushika hatam, ikiwa na lengo la kuihamasisha jamii kutoa fursa kwa mtoto wa kike katika masuala mbalimbali katika jamii ikiwemo kupata elimu na uongozi.

No comments: