Sunday, October 16, 2016

KILIMANJARO WAADHIMISHA MIAKA 17 YA KUMBUKUMBU CHA KIFO CHA BABA WA TAIFA KWA KUOTESHA MITI.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki akiongozana na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru wakati alipowasili katika chanzo cha maji cha Shiri kwa ajili ya zoezi la kuotesha miti ikiwa ni kuadhimisha miaka 17 ya kifo cha Baba wa Taifa ,Hayati Mwl Julius Nyerere.
Wakuu wa wilaya za Hai na Moshi ,Gelasius Byakanwa (wa pili toka kulia) na Kippi Warioba (wa tatu toka kushoto waliungana na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro katika zoezi hilo.kulia ni Katibu tawala wa mkoa wa Kilimanjaro Mhandisi Aisha Amour.
Eneo lilipo jirani na chanzo cha maji cha Shiri ambalo liliandaliwa kwa ajili ya kuoteshwa miti.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadiki akizungumza kabla ya kuanza kwa zoezi la uoteshaji miti.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki akiotesha mti katika eneo la chanzo cha maji la Shiri Njoro lililopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Gelasius Byakanwa akiotesha mti katika eneo hilo.
Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro,Aisha Amour akiotesha mti katika eneo hilo.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kipi Warioba akiotesha mti katika eneo hilo zoezi ambali lilishirikisha watumishi wa idara mbalimbali za serikali na wafanyakazi wa Mamlaka ya Majsafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi(MUWSA).
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru akiotesha mti katika eneo hilo.
Baadhi ya watumishi wa idara za serikali wakishiriki katika zoezi hilo.
Meneja Biashara wa MUWSA,John Ndetiko akiotesha mti katika eneo hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki akiongozana na viongozi wa wilaya pamoja na wananchi wengine kutembelea chanzo cha maji cha Shiri Njoro .
Mkuu wa wilaya ya Hai,Gelasius Byakanwa(kushoto) Mkuu wa wilaya ya Moshi Kippi Warioba (anayefuatia pamoja na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wakitizama eneo ambalo kunafanyika mgawanyo wa maji katika chanzo cha maji cha Shiri Njoro.
Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Kippi Warioba (kulia) akiwa pamoja na Mkuu wa wilaya ya Hai,Gelasius Byakanwa.
Chanzo cha maji cha Shiri.
Baadhi ya watumishi wa serikali wakitizama chanzo cha maji cha Shiri njoro.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Said Meck Sadiki akizungumza katika chanzo hicho.
Meneja Biashara wa MUWSA ,John Ndetiko akizungumza katika chanzo hicho.
Mkuu wa mkoa akijiadaa kuvuka katika eneo lenye maji katika chanzo hicho.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini. 

No comments: