Sunday, October 30, 2016

DTB YAZINDUA TAWI LA 26 BARABARA YA MWAI KIBAKI, MBEZI CHINI, JIJINI DAR ES SALAAM

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Benjamin Sitta, akikata utepe katika uzinduzi wa tawi jipya la Benki ya Diamond Trust lililopo barabara ya Mwai Kibaki, Mbezi Chini Jijini Dar es salaam, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Viju Cherian na kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Fedha Joseph Mabusi na Meneja wa Tawi hilo Msingo Kimune wakishuhudia. Tawi hilo ni tawi la 12 jijini Dar es Salaam na ni tawi la 26 nchini Tanzania.(picha na Mpiga picha wetu)
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Benjamin Sitta akiongea na wageni waalikwa kwenye uzinduzi wa tawi jipya la Benki ya Diamond Trust lililopo barabara ya Mwai Kibaki, Mbezi Chini jijini Dar es salaam, Tawi hilo ni tawi la 12 jijini Dar es Salaam na ni tawi la 26 nchini Tanzania. (picha na Mpiga picha wetu)

Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Diamond Trust pamoja na wageni waalikwa wakisikiliza hotuba ya Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Benjamin Sitta (Hayupo pichani) aliyekuwa mgeni rasmi kwenye hafla ya uzinduzi wa tawi jipya la benki hiyo lililopo barabara ya Mwai Kibaki, Mbezi chini jiji Dar es Salaam. Tawi hilo ni la 12 jijini la Dar es Salaam na ni tawi la 26 nchini Tanzania. 

No comments: