Friday, September 9, 2016

SERIKALI YA UJERUMANI YATOA MSAADA WA FEDHA YURO LAKI NNE KWA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

 Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Injinia Ngosi Mwihava akikaribisha ujumbe toka Serikali ya Ujerumani uliofika Ofisi kwake Mtaa wa Luthuli jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kusaini mkataba wa makubaliano ya  kuisaidia Ofisi ya Makamu wa Rais kiasi cha fedha yuro laki nne kwa ajili ya shughuli za mabadiliko ya tabia Nchi.
  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Injinia Ngosi Mwihava akiongea jambo na Mwakilishi wa Balozi wa Ujerumani Bi. Lena Thiede kabla ya kuanza shighuli ya kusaini mkataba huo.
 Sehemu ya Watumishi ya Ofisi ya Makamu wa Rais Idara ya Mazingira wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mazingira Richard Muyungi(wa kwanza kulia) wakimsikiliza kwa makini Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Injinia Ngosi Mwihava (hayupo pichani) wakati anatoa neno la shukurani kwa Serikali ya Ujerumani  kabala ya kusiani mktaba huo.
 Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Injinia Ngosi Mwihava pamoja na Mkuu wa program ya Maji toka Ubalozi wa Ujerumani Bw. Ernst Doring wakisaini hati za makubaliano ya Serikali ya Ujerumani kuisaidia Ofisi ya Makamu wa Rais kiasi cha fedha yuro laki nne  kwa jaili ya kuendesha program  za mabadiliko ya tabia Nchi.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Injinia Ngosi Mwihava na Mkuu wa program ya Maji toka Ubalozi wa Ujerumani Bw. Ernst Doring  wakibadilishana hati za makubaliano mara baada ya kusaini  mkataba huo.

No comments: