Tuesday, August 2, 2016

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII PROFESA MAGHEMBE AWAASA BODI YA UTALII KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII.

  Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe akizungumza na wajumbe wa bodi ya utalii Tanzania(TTB) jijini Dar es Salaam leo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa bodi ya utalii. Amesema kuwa  bodi ya utalii wanawajibu wa kutangaza vivutio vilivyopo hapa nchini ili kila mtu na aweze kutembelea vivutio hivyo kwaajili ya kuongeza pato la Nchi.

Pia amesema kuwa Bodi ya Utalii inapaswa kulipa deni la bodi hiyo kwani linaleta doa katika bodi ya utalii hiyo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii(TTB), Jaji Mstaafu Thomas Mihayo akizungumza na wajumbe wa bodi ya utalii Tanzania jijini Dar es Salaam leo. Amesema kuwa Bodi ya Utalii inakabiliwa na deni la shilingi bilioni 3.7 ambalo limetokana na matangazo yaliyokuwa yakitangazwa nje ya nchi kwenye viwanja vya mpira kwaajili ya kutangaza utalii.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Angeline Madete (Kulia ) na Mkurugenzi wa Wizara ya Maliasili na utalii, Zahoro Kimwaga wakiwa kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Bodi ya Utalii Tanzania jijini Dar es Salaam leo.

Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Utalii wakimsikiliza  Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe jijini Dar es Saalaam.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe(Katikati) Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii(TTB), Jaji Mstaafu Thomas Mihayo kushoto na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Angeline Madete wakiwa katika picha ya Pamoja na wajumbe wa bodi ya Utalii (TTB)jijini Dar es Salaam leo.

No comments: