Wednesday, August 24, 2016

WANANCHI WAJITOKEZA KUUPOKEA MWENGE WA UHURU JIJINI ARUSHA

Mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru uliopokelewa leo katika Jiji la Arusha eneo la Kisongo kwaajili ya kukimbizwa kwa siku moja katika urefu wa Kilometa 81.19 katika Tarafa tatu.
Mkurugenzi wa Jiji la Arusha,Athumani Kihamia akipokea Mwenge wa Uhuru ambao utakimbizwa ukiwa unaelimisha na kueneza ujumbe wa "Washirikishwe na Kuwezeshwa" ujumbe huo ukiwa umeambatana na kauli mbiu "Vijana ni Nguvukazi ya Taifa Washirikishwe na Kuwezeshwa"

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa,George Mbijima akizindua Kituo cha Afya  katika Kata ya Elerai jijini Arusha kitakachowahudumia wananchi wa Kata hiyo,Sombetini na Ngarenaro.Miradi yenye thamani ya zaidi ya Sh 1.5 ambayo Soko,Afya,Maji,Elimu,Uwezeshaji wa wananchi kiuchumi makundi maalumu,Ujenzi wa daraja na usafi na utunzaji wa mazingira.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa,George Mbijima akiwagawia Vyandarua ukiwa ni mpango wa Jiji kupiga vita ugonjwa wa Malaria baada ya kuzindua Kituo cha Afya  katika Kata ya Elerai jijini Arusha.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa,George Mbijima akizindua Soko la Mazao mchanyiko   katika Kata ya Elerai jijini Arusha .
Sehemu ya wananchi waliojitokeza kuulaki Mwenge wa Uhuru katika viwanja vya Shule ya Sekondari Kimandolu ambako mradi wa maji ulizinduliwa.

No comments: