Thursday, August 18, 2016

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KATIBU MKUU MSAIDIZI WA UMOJA WA MATAIFA DKT. NATALIA KANEM PIA AKUTANA NA KATIBU MKUU WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI BALOZI LIBERAT MFUMUKEKO IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Katibu Mkuu Msaidizi wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya Watu (UNFPA), Dkt. Natalia Kanem alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya nae mazungumzo.
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo wakati akizungumza na Katibu Mkuu Msaidizi wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni  Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya Watu (UNFPA), Dkt. Natalia Kanem wapili kutoka (kushoto) Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akitazama vitabu alivyopewa na mgeni wake Katibu Mkuu Msaidizi wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni  Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya Watu (UNFPA), Dkt. Natalia Kanem wapili kutoka (kushoto) Ikulu jijini Dar es Salaam. Wakwanza (kulia) ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiangalia vitabu hivyo.
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Katibu Mkuu Msaidizi wa Umoja wa Mataifa na Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya Watu (UNFPA), Dkt. Natalia Kanem mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Katibu Mkuu Msaidizi wa Umoja wa Mataifa na Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya Watu (UNFPA), Dkt. Natalia Kanem watatu kutoka kulia mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.wengine katika picha ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga watatu kutoka (kushoto). 
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Balozi Liberat Mfumukeko Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya  mazungumzo. 
PICHA NA IKULU.

No comments: