Wednesday, August 24, 2016

Naibu Waziri wa Afya Dk.Kigwangalla aagiza Hospitali zote nchini kufanya ukarabati wa vifaa vya Mahospitali

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla ameagiza Hospitali zote nchini kuweza kufanya ukarabati wa vifaa vyote vya Mahospitali yao ambavyo wamerundika stoo, ili kusaidia kupunguza gharama za manunuzi ya vifaa vipya ambavyo ni gharama kubwa.


Dk. Kigwangalla ameyasema hayo Wilayani Meatu, Mkoani Simiyu wakati wa ziara yake ya kikazi ambapo amepongeza juhudi za Hospitali ya Meatu kwa hatua yao ya kuamua kufanya ukarabati wa vifaa vyote vya Hospitali hiyo huku wakiokoa mamilioni ya fedha.

“Napongeza Hospitali ya Meatu kwa ubunifu huu waliofanya. Kwani wameweza kuokoa mamilioni na hii napenda kutoa maagizo kwa Hospitali zote hapa nchini kuhakikisha wanakarabati vifaa hivyo ambavyo vingi wamekuwa wakirundika tu stoo kwa kufanya hivyo watasaidia kupunguza gharama.” Amesema Dk. Kigwangalla wakati wa kutoa maagizo hayo.

Hospitali hiyo ya Meatu imeweza kufungua kalakana ya kufanyia matengenezo na ukarabati wa vifaa mbalimbali ikiwemo vitanda vya wagonjwa pamoja na vifaa vingine vingi ambavyo kwa manunuzi yake ni gharama kubwa sana.

Naibu Waziri huyo pia amepata kutembelea maeneo mbalimbali ya Hospitali hiyo ikiwemo sehemu za Mahabara, Chumba cha upasuaji, wodi ya Wakinamama, kitengo cha meno, mapokezi na bohari ya chanjo ya Wilaya pamoja na duka la dawa la wilaya hiyo ndani ya Hospitali huku akikuta mapungufu kadhaa ambayo amwaagiza wawe wameyashughulikia ndani ya miezi mitatu kabla ya kuchukuliwa hatua thabiti pindi watakapokiuka.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akionyeshwa baadhi ya vitanda vya Hospitali vilivyofanyiwa ukarabati
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akishuhudia baadhi ya vitanda vya Hospitali vilivyofanyiwa ukarabati.
Baadhi ya vitanda vilivyofanyiwa ukarabati
Vitanda vya kujifungulia wodi ya wazazi.. ambavyo inaelezwa kuwa kitanda kimoja kina gharimu zaidi ya milioni moja na nusu
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akionyeshwa baadhi ya vitanda vya Hospitali vilivyofanyiwa ukarabati.
Baadhi ya vitu vya Hospitali hiyo ya Meatu.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua Chumba cha Upasuaji ambapo hata hivyo alikuta mapungufu mbalimbali na kuwapa miezi mitatu wawe wamerekebisha.
chumba cha upasuaji cha Hospitali ya Wilaya ya Meatu.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akiingia kwenye Kituo cha Afya Mwandoya ambacho licha ya udogo wake, kimeanzisha huduma za upasuaji miezi 6 iliyopita na hadi sasa tayari wamefanya Operesheni 40, zote zimefanikiwa.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akitoa maelezo kwa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Meatu namna ya kituo hicho licha ya udogo wake lakini kipo na viwango kamili namna ya Chumba cha upasuaji kinavyotakiwa kiwe. Ambapo pia ametoa wito kwa vituo vyote vya Afya kuhakikisha wanajenga ama kukarabati chumba cha upasuaji.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akimjulia hali mmoja wa watoto ambaye alifanyiwa operesheni kwenye kituo cha Afya Mwandoya,Wilayani Meatu ambacho licha ya udogo wake, kimeanzisha huduma za upasuaji miezi 6 iliyopita na hadi sasa tayari wamefanya Operesheni 40, zote zimefanikiwa.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akipata picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa kituo hicho cha Mwandoya, kilichopo Wilayani Meatu, Mkoani Sumiyu.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akiwa amembeba mmoja wa watoto aliyejifungua siku hiyo wakati ametembelea kituo hicho cha Mwandoya ambacho licha ya udogo wake, tayari wameweza kuwa na chumba cha upasuaji na kinatoa huduma bora safi licha ya kuwa pia kipo kijijini. Wilayani Meatu.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akiwa amembeba mmoja wa watoto aliyejifungua siku hiyo wakati ametembelea kituo hicho cha Mwandoya ambacho licha ya udogo wake, tayari wameweza kuwa na chumba cha upasuaji na kinatoa huduma bora safi licha ya kuwa pia kipo kijijini. Wilayani Meatu.
Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Meatu akimuonyesha Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla moja ya vitanda hivyo.
Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Meatu akimuonyesha Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla moja ya vitanda hivyo.

No comments: