Wednesday, August 10, 2016

Majaliwa azindua Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji Mkoani Mbeya

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao (kushoto) alipowasili katika banda la Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji (TAJATI) katika viwanja vya Nanenane John Mwakangale jana Jijini Mbeya. Katikati ni Mwenyekiti wa TAJATI Bw. Ulimboka Mwakilili
 Mwenyekiti wa TAJATI Bw. Ulimboka Mwakilili (wapili kulia) akitambulisha baadhi ya wajumbe wa TAJATI kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa alipowasili katika banda la Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji (TAJATI) katika viwanja vya Nanenane John Mwakangale jana Jijini Mbeya kwa ajili ya kuzindua chama hicho
 Mwenyekiti wa TAJATI Bw. Ulimboka Mwakilili (kushoto) akimuonyesha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa picha yenye sura ya kufanana naye iliyochorwa na mmoja wa wanachama wa TAJATI baada ya kuzindua chama hicho jana Jijini Mbeya katika viwanja vya Nanenane John Mwakangale. Katikati ni mke wa Waziri Mkuu mama Mary Majaliwa
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akipokea zawadi ya saa ya uzinduzi wa Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji (TAJATI) kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao (wapili kushoto) baada ya kuzindua chama hicho jana Jijini Mbeya katika viwanja vya Nanenane John Mwakangale. Watatu kushoto ni mke wa Waziri Mkuu mama Mary Majaliwa
Moja ya burudani iliyokua ikiendelea kati banda la Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji (TAJATI) jana Jijini Mbeya katika viwanja vya Nanenane John Mwakangale.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akihutubia wananchi (hawapo pichani) walioshiriki maonyesho ya nanenane kutoka mikoa ya nyanda za juu kusini jana Jijini Mbeya katika viwanja vya Nanenane John Mwakangale.
 : Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao (wapili kushoto) akizungumza na viongozi wa Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji (TAJATI), alipowasili katika banda lao katika viwanja vya Nanenane John Mwakangale jana Jijini Mbeya. Chama hicho  kilizinduliwa rasmi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa
Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji (TAJATI) Bw. Venansi Matinya (kushoto) akielimisha umma uliotembelea banda la TAJATI baada ya chama hicho  kuzinduliwa rasmi  na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa jana Jijini Mbeya katika viwanja vya Nanenane John Mwakangale.

No comments: